< Matendo 8 >

1 Sauli alikuwa kwenye makubaliano ya kifo chake. siku hiyo ndipo alipoanza kuwatesa kinyume cha kanisa lililokuwa Yerusalemu; na waaminio wote waliotawanyika katika majimbo ya Yudea na Samaria, isipokuwa mitume.
Or Saul consentait à la mort d'Etienne, et en ce temps-là il se fit une grande persécution contre l'Eglise qui était à Jérusalem, et tous furent dispersés dans les quartiers de la Judée et de la Samarie; excepté les Apôtres.
2 Watu wachamungu walimzika Stefano na kufanya maombolezo makubwa juu yake.
Et quelques hommes craignant Dieu emportèrent Etienne pour l'ensevelir, et menèrent un grand deuil sur lui.
3 Lakini Sauli alilidhuru sana kanisa. Alikwenda nyumba kwa nyumba na kuwaburuza nje wanawake na waume, na kuwatupia gerezani.
Mais Saul ravageait l'Eglise, entrant dans toutes les maisons, et traînant par force hommes et femmes, il les mettait en prison.
4 waaminio ambao walikuwa wametawanyika bado walilihubiri neno.
Ceux donc qui furent dispersés allaient çà et là annonçant la parole de Dieu.
5 Filipo akashuka katika mji wa Samaria na akamtangaza Kristo huko.
Et Philippe étant descendu en une ville de Samarie, leur prêcha Christ.
6 Baada ya makutano kusikia na kuona ishara alizofanya Filipo; wakaweka umakini juu ya kile alichosema.
Et les troupes étaient toutes ensemble attentives à ce que Philippe disait, l'écoutant, et voyant les miracles qu'il faisait.
7 Kutoka hapo watu wengi waliosikia, pepo wachafu waliwatoka watu huku wakilia kwa sauti kubwa, na wengi waliopooza na viwete waliponywa.
Car les esprits immondes sortaient, en criant à haute voix, hors de plusieurs qui en étaient possédés, et beaucoup de paralytiques et de boiteux furent guéris.
8 Na kulikuwa na furaha kubwa katika mji.
Ce qui causa une grande joie dans cette ville-là.
9 Lakini palikuwa na mtu mmoja katika mji ule jina lake Simon, ambaye alikuwa akifanya uchawi; ambao aliutumia kuwashangaza watu wa taifa la Samaria, wakati akisema kuwa yeye ni mtu wa muhimu.
Or il y avait auparavant dans la ville un homme nommé Simon qui exerçait l'art d'enchanteur, et ensorcelait le peuple de Samarie, se disant être quelque grand personnage.
10 Wasamaria wote tangu mdogo hata mkubwa, wakamsikiliza; wakasema;”mtu huyu ni ile nguvu ya Mungu ambayo ni kuu.”
Auquel tous étaient attentifs, depuis le plus petit jusques au plus grand, disant: celui-ci est la grande vertu de Dieu.
11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mrefu kwa uchawi wake.
Et ils étaient attachés à lui, parce que depuis longtemps il les avait éblouis par sa magie.
12 Lakini wakati walipoamini kuwa Filipo alihubiri juu ya ufalme wa Mungu na juu ya jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanaume kwa wanawake.
Mais quand ils eurent cru ce que Philippe leur annonçait touchant le Royaume de Dieu, et le Nom de Jésus-Christ, et les hommes et les femmes furent baptisés.
13 Na Simoni mwenyewe aliamini: baada ya kubatizwa, aliendelea kuwa na Filipo; alipoona ishara na miujiza iliyokuwa ikitendeka, alishangaa.
Et Simon crut aussi lui-même, et après avoir été baptisé, il ne bougeait d'auprès de Philippe; et voyant les prodiges et les grands miracles qui se faisaient, il était comme ravi hors de lui même.
14 Wakati mitume wa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria imepokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana.
Or quand les Apôtres qui étaient à Jérusalem, eurent entendu que la Samarie avaient reçu la parole de Dieu, ils leur envoyèrent Pierre et Jean;
15 Wakati walipokuwa wakishuka wakawaombea; kwamba wampokee Roho Mtakatifu.
Qui y étant descendus prièrent pour eux, afin qu'ils reçussent le Saint-Esprit:
16 Mpaka muda huo, Roho Mtakatifu alikuwa hajawashukia hata mmoja wao; walikuwa tu wamebatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
Car il n'était pas encore descendu sur aucun d'eux, mais seulement ils étaient baptisés au Nom du Seigneur Jésus.
17 Ndipo Petro na Yohana wakawawekea mikono, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Puis ils leur imposèrent les mains, et ils reçurent le Saint-Esprit.
18 Wakati Simoni alipoona kwamba Roho Mtakatifu ametolewa kupitia kuwekewa mikono na mitume; akataka kuwapa pesa,
Alors Simon ayant vu que le Saint-Esprit était donné, par l'imposition des mains des Apôtres, il leur présenta de l'argent,
19 Akasema, “Nipeni hii nguvu, ili kila nitakayemwekea mikono apokee Roho Mtakatifu.”
En leur disant: donnez-moi aussi cette puissance, que tous ceux à qui j'imposerai les mains reçoivent le Saint-Esprit.
20 Lakini Petro akamwambia; pesa yako pamoja na wewe ipotelee mbali, kwa sababu umedhani kuwa karama ya Mungu inapatikana kwa pesa.
Mais Pierre lui dit: que ton argent périsse avec toi, puisque tu as estimé que le don de Dieu s'acquiert avec de l'argent.
21 Hauna sehemu katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mnyoofu mbele za Mungu.
Tu n'as point de part ni d'héritage en cette affaire: car ton cœur n'est point droit devant Dieu.
22 Hivyo basi tubu maovu yako na kumwomba Mungu labda utasamehewe fikra za moyo wako.
Repens-toi donc de cette méchanceté, et prie Dieu, afin que s'il est possible, la pensée de ton cœur te soit pardonnée.
23 Kwa maana naona uko katika sumu ya uchungu na kifungo cha dhambi.”
Car je vois que tu es dans un fiel très amer, et dans un lien d'iniquité.
24 Simoni akajibu na kusema, “Mwombeni Bwana kwa ajili yangu, kwa kuwa mambo yote mliyozungumza yaweza kunitokea.
Alors Simon répondit, et dit: vous, priez le Seigneur pour moi, afin que rien ne vienne sur moi des choses que vous avez dites.
25 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wameshuhudia na kuhubiri neno la Bwana, walirudi Yerusalemu kwa njia hiyo; walihubiri injili katika vijiji vingi vya Wasamaria.
Eux donc après avoir prêché et annoncé la parole du Seigneur, retournèrent à Jérusalem, et annoncèrent l'Evangile en plusieurs bourgades des Samaritains.
26 Basi malaika wa Bwana akanena na Filipo na kusema, “Angaza na uende kusini katika njia iendayo chini ya Yerusalemu kuelekea Gaza.” ( Njia hii iko katika jangwa).
Puis l'Ange du Seigneur parla à Philippe, en disant: lève-toi, et t'en va vers le Midi, au chemin qui descend de Jérusalem à Gaza, celle qui est déserte.
27 Akaangaza na kwenda. Tazama, kulikuwa na mtu wa Ethiopia, towashi mwenye mamlaka kuu chini ya kandase; malkia wa Ethiopia. Aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu.
Lui donc se levant, s'en alla; et voici un homme Ethiopien, Eunuque, qui était un des principaux Seigneurs de la Cour de Candace, Reine des Ethiopiens, commis sur toutes ses richesses, et qui était venu pour adorer à Jérusalem;
28 Alikuwa akirejea ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
S'en retournait, assis dans son chariot; et il lisait le Prophète Esaïe.
29 Roho akasema na Filipo, “Sogea karibu na gari hili ukashikamane nalo.
Et l'Esprit dit à Philippe: approche-toi, et te joins à ce chariot.
30 “Hivyo Filipo akaenda mbio, akamsikia akisoma katika chuo cha nabii Isaya; akasema, Je unafahamu unachosoma?”
Et Philippe y étant accouru, il l'entendit lisant le Prophète Esaïe; et il lui dit: mais comprends-tu ce que tu lis?
31 Muethiopia akasema, “nitawezaje mtu asiponiongoza?” Akamsihi Filipo apande garini na kuketi pamoja naye.
Et il lui dit: mais comment le pourrais-je comprendre, si quelqu'un ne me guide? et il pria Philippe de monter et s'asseoir avec lui.
32 Sasa fungu la maandiko alilokuwa akisoma Muethiopia ni hili; Aliongozwa kama kondoo kwenda machinjioni kuchinjwa; na kama kondoo alinyamaza kimya, hakufungua kinywa chake:
Or le passage de l'Ecriture qu'il lisait était celui-ci: il a été mené comme une brebis à la boucherie, et comme un agneau muet devant celui qui le tond; en sorte qu'il n'a point ouvert sa bouche.
33 Kwa kuhuzunishwa kwake hukumu yake iliondolewa: Nani ataeleza kizazi chake? maisha yake yameondolewa katika nchi.”
En son abaissement son jugement a été haussé; mais qui racontera sa durée? car sa vie est enlevée de la terre.
34 Hivyo towashi akamwuliza Filipo, na kusema, “nakuomba, ni nabii yupi ambaye anaongelewa habari zake, ni kuhusu yeye, au za mtu mwingine”?
Et l'Eunuque prenant la parole, dit à Philippe: je te prie, de qui est-ce que le Prophète dit cela: est-ce de lui-même, ou de quelque autre?
35 Filipo alianza kuongea, alianza kwa andiko hili la Isaya kumhubiria habari za Yesu.
Alors Philippe ouvrant sa bouche, et commençant par cette Ecriture, lui annonça Jésus.
36 Wakiwa njiani, wakafika penye maji,' towashi akasema, “Tazama, pana maji hapa nini kinazuia nisibatizwe?,
Et comme ils continuaient leur chemin, ils arrivèrent à [un lieu où il y avait] de l'eau; et l'Eunuque dit: voici de l'eau, qu'est-ce qui empêche que je ne sois baptisé?
37 maneno haya, “Hivyo Muethiopia akajibu “naamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,” hayamo kwenyemaandiko ya kale). Ndipo Muethiopia akaamuru gari lisimame.
Et Philippe dit: si tu crois de tout ton cœur, cela t'est permis; et [l'Eunuque] répondant, dit: Je crois que Jésus-Christ est le Fils de Dieu.
38 Walikwenda ndani ya maji, pamoja Filipo na towashi, Filipo akambatiza.
Et ayant commandé qu'on arrêtât le chariot, ils descendirent tous deux dans l'eau, Philippe et l'Eunuque; et [Philippe] le baptisa.
39 Wakati walipotoka kwenye maji, Roho wa Bwana ikampeleka Filipo mbali; towashi hakumwona, akaenda njia yake akishangilia.
Et quand ils furent remontés hors de l'eau, l'Esprit du Seigneur enleva Philippe, et l'Eunuque ne le vit plus; et tout joyeux il continua son chemin.
40 Lakini Philipo akatokea Azoto. Alipita katika mkoa ule na kuhubiri injili katika miji yote mpaka alipofika Kaisaria.
Mais Philippe se trouva dans Azote, et en passant il annonça l'Evangile dans toutes les villes, jusqu'à ce qu'il fût arrivé à Césarée.

< Matendo 8 >