< Matendo 8 >
1 Sauli alikuwa kwenye makubaliano ya kifo chake. siku hiyo ndipo alipoanza kuwatesa kinyume cha kanisa lililokuwa Yerusalemu; na waaminio wote waliotawanyika katika majimbo ya Yudea na Samaria, isipokuwa mitume.
But Shaol willed to take part in his killing. And there was made in those days a great persecution against the church that was in Urishlem; and they were all dispersed in the country of Jihud and also among the Shomroyee, excepting only the apostles.
2 Watu wachamungu walimzika Stefano na kufanya maombolezo makubwa juu yake.
And faithful men laid Estephanos in his tomb, and mourned over him greatly.
3 Lakini Sauli alilidhuru sana kanisa. Alikwenda nyumba kwa nyumba na kuwaburuza nje wanawake na waume, na kuwatupia gerezani.
BUT Shaol persecuted the church of Aloha, going to the houses, and drawing men and women delivered them to the house of the bound.
4 waaminio ambao walikuwa wametawanyika bado walilihubiri neno.
And they who were dispersed went about and preached the word of Aloha.
5 Filipo akashuka katika mji wa Samaria na akamtangaza Kristo huko.
But Philipos descended to a city of the Shomroyee, and preached concerning the Meshiha.
6 Baada ya makutano kusikia na kuona ishara alizofanya Filipo; wakaweka umakini juu ya kile alichosema.
And when they heard his word, the men who were there attended to him, and were persuaded of all that he said: for they saw the signs that he wrought.
7 Kutoka hapo watu wengi waliosikia, pepo wachafu waliwatoka watu huku wakilia kwa sauti kubwa, na wengi waliopooza na viwete waliponywa.
For many whom unclean spirits possessed cried with a high voice, and they came out from them; and others, palsied and lame, were healed:
8 Na kulikuwa na furaha kubwa katika mji.
and great joy was in that city.
9 Lakini palikuwa na mtu mmoja katika mji ule jina lake Simon, ambaye alikuwa akifanya uchawi; ambao aliutumia kuwashangaza watu wa taifa la Samaria, wakati akisema kuwa yeye ni mtu wa muhimu.
But a certain man was there whose name was Simon, who had dwelt in that city much time, and with his sorceries had deceived the people of the Shomroyee, magnifying himself, and saying, I am the Great.
10 Wasamaria wote tangu mdogo hata mkubwa, wakamsikiliza; wakasema;”mtu huyu ni ile nguvu ya Mungu ambayo ni kuu.”
And all inclined to him, great and small, and said, This is the great Power of Aloha.
11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mrefu kwa uchawi wake.
And they were persuaded by him, because that much time by his sorceries he had astonished them.
12 Lakini wakati walipoamini kuwa Filipo alihubiri juu ya ufalme wa Mungu na juu ya jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanaume kwa wanawake.
But when they believed Philipos, who evangelized the kingdom of Aloha in the name of our Lord Jeshu Meshiha, they were baptized, men and women.
13 Na Simoni mwenyewe aliamini: baada ya kubatizwa, aliendelea kuwa na Filipo; alipoona ishara na miujiza iliyokuwa ikitendeka, alishangaa.
And Simon also himself believed, and was baptized, and adhered to Philipos. And when he saw the signs and great works which were done by his hands, he wondered and was astonished.
14 Wakati mitume wa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria imepokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana.
AND when the apostles who were at Urishlem heard that the people of the Shomroyee had received the word of Aloha, they sent to them Kipha and Juhanon.
15 Wakati walipokuwa wakishuka wakawaombea; kwamba wampokee Roho Mtakatifu.
And they went down and prayed for them, that they might receive the Spirit of Holiness:
16 Mpaka muda huo, Roho Mtakatifu alikuwa hajawashukia hata mmoja wao; walikuwa tu wamebatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
for he was not upon one of them yet; but they were only baptized in the name of our Lord Jeshu.
17 Ndipo Petro na Yohana wakawawekea mikono, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Then they laid upon them the hand, and they received the Spirit of Holiness.
18 Wakati Simoni alipoona kwamba Roho Mtakatifu ametolewa kupitia kuwekewa mikono na mitume; akataka kuwapa pesa,
And when Simon saw that by the hand-laying of the apostles the Spirit of Holiness was given, he offered to them silver,
19 Akasema, “Nipeni hii nguvu, ili kila nitakayemwekea mikono apokee Roho Mtakatifu.”
saying, Give also to me this power, that he on whom I shall lay the hand may receive the Spirit of Holiness.
20 Lakini Petro akamwambia; pesa yako pamoja na wewe ipotelee mbali, kwa sababu umedhani kuwa karama ya Mungu inapatikana kwa pesa.
Shemun Kipha said to him, Thy silver go with thee into perdition, because thou thoughtest that the gift of Aloha with the possessions of the world might he obtained.
21 Hauna sehemu katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mnyoofu mbele za Mungu.
Thou hast neither part nor lot in this faith, because thine heart hath not been right before Aloha.
22 Hivyo basi tubu maovu yako na kumwomba Mungu labda utasamehewe fikra za moyo wako.
Nevertheless, repent of this thy wickedness, and pray of Aloha, that the guile of thy heart may haply be forgiven thee;
23 Kwa maana naona uko katika sumu ya uchungu na kifungo cha dhambi.”
for in bitter gall and in the bonds of iniquity I see that thou art.
24 Simoni akajibu na kusema, “Mwombeni Bwana kwa ajili yangu, kwa kuwa mambo yote mliyozungumza yaweza kunitokea.
Simon answered and said, Pray you on my behalf, of Aloha, that not any of these things which you have spoken may come upon me.
25 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wameshuhudia na kuhubiri neno la Bwana, walirudi Yerusalemu kwa njia hiyo; walihubiri injili katika vijiji vingi vya Wasamaria.
But Shemun and Juhanon, when they had testified and taught the word of Aloha, returned to Urishlem, and evangelized in many villages of the Shomroyee.
26 Basi malaika wa Bwana akanena na Filipo na kusema, “Angaza na uende kusini katika njia iendayo chini ya Yerusalemu kuelekea Gaza.” ( Njia hii iko katika jangwa).
AND the angel of the Lord spake with Philipos, and said to him, Arise, go to the south, in the desert way which goeth down from Urishlem to Gaza.
27 Akaangaza na kwenda. Tazama, kulikuwa na mtu wa Ethiopia, towashi mwenye mamlaka kuu chini ya kandase; malkia wa Ethiopia. Aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu.
And arising he went. And there met him a certain eunuch who had come from Cush, an officer of Kandak, queen of the Cushoyee; and he was officer over all her treasure. And he had been to worship at Urishlem;
28 Alikuwa akirejea ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
and while returning that he might go, he sat in the chariot and read in Eshaia the prophet.
29 Roho akasema na Filipo, “Sogea karibu na gari hili ukashikamane nalo.
And the Spirit of Holiness said to Philipos, Approach, and join the chariot.
30 “Hivyo Filipo akaenda mbio, akamsikia akisoma katika chuo cha nabii Isaya; akasema, Je unafahamu unachosoma?”
And being near, he heard that he read in Eshaia the prophet; and he said to him, Understandest thou what thou readest?
31 Muethiopia akasema, “nitawezaje mtu asiponiongoza?” Akamsihi Filipo apande garini na kuketi pamoja naye.
And he said, How can I understand, unless one teach me? And he prayed of him, of Philipos, to ascend and sit with him.
32 Sasa fungu la maandiko alilokuwa akisoma Muethiopia ni hili; Aliongozwa kama kondoo kwenda machinjioni kuchinjwa; na kama kondoo alinyamaza kimya, hakufungua kinywa chake:
But the section (phosuka) of the scripture in which he was reading is this: As a lamb to the slaughter was he led; And as a sheep before the shearer is silent, So opened not he his mouth in his humiliation.
33 Kwa kuhuzunishwa kwake hukumu yake iliondolewa: Nani ataeleza kizazi chake? maisha yake yameondolewa katika nchi.”
From oppression and from judgment was he led; And his age who shall recount? For his life is taken from the earth.
34 Hivyo towashi akamwuliza Filipo, na kusema, “nakuomba, ni nabii yupi ambaye anaongelewa habari zake, ni kuhusu yeye, au za mtu mwingine”?
That eunuch said Unto Philipos, I pray thee, of whom speaketh this the prophet? of himself, or of another man?
35 Filipo alianza kuongea, alianza kwa andiko hili la Isaya kumhubiria habari za Yesu.
Then Philipos opened his mouth and began, from that very scripture, preaching to him concerning our Lord Jeshu.
36 Wakiwa njiani, wakafika penye maji,' towashi akasema, “Tazama, pana maji hapa nini kinazuia nisibatizwe?,
And as they went in the way they came to a certain place which had water in it, and that eunuch said, Behold the water; what is the hinderance that I should be baptized?
37 maneno haya, “Hivyo Muethiopia akajibu “naamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,” hayamo kwenyemaandiko ya kale). Ndipo Muethiopia akaamuru gari lisimame.
38 Walikwenda ndani ya maji, pamoja Filipo na towashi, Filipo akambatiza.
And he commanded that the chariot should stand; and they descended both of them to the water, and Philipos baptized that eunuch.
39 Wakati walipotoka kwenye maji, Roho wa Bwana ikampeleka Filipo mbali; towashi hakumwona, akaenda njia yake akishangilia.
And when they had ascended from the water, the Spirit of the Lord rapt away Philipos, and the eunuch again saw him not; but he went on his way rejoicing.
40 Lakini Philipo akatokea Azoto. Alipita katika mkoa ule na kuhubiri injili katika miji yote mpaka alipofika Kaisaria.
But Philipos was found at Azotos, and from thence he itinerated and evangelized in all the cities until he came to Cesarea.