< Matendo 8 >

1 Sauli alikuwa kwenye makubaliano ya kifo chake. siku hiyo ndipo alipoanza kuwatesa kinyume cha kanisa lililokuwa Yerusalemu; na waaminio wote waliotawanyika katika majimbo ya Yudea na Samaria, isipokuwa mitume.
BUT Saul was delighted with his execution. Now on that very day commenced a great persecution against the church which was at Jerusalem; and all, besides the apostles, were dispersed through the regions of Judea and Samaria.
2 Watu wachamungu walimzika Stefano na kufanya maombolezo makubwa juu yake.
Then some pious men assembling, carried Stephen to his grave, and made great lamentation over him.
3 Lakini Sauli alilidhuru sana kanisa. Alikwenda nyumba kwa nyumba na kuwaburuza nje wanawake na waume, na kuwatupia gerezani.
But Saul ravaged the church, entering into the houses, and dragging men and women, cast them into prison.
4 waaminio ambao walikuwa wametawanyika bado walilihubiri neno.
Those therefore who were dispersed, travelled through the country, preaching the word.
5 Filipo akashuka katika mji wa Samaria na akamtangaza Kristo huko.
But Philip, going down to a city of Samaria, preached Christ unto them.
6 Baada ya makutano kusikia na kuona ishara alizofanya Filipo; wakaweka umakini juu ya kile alichosema.
And the multitudes with united minds were very attentive to the things spoken by Philip, when they heard him, and saw the miracles which he did.
7 Kutoka hapo watu wengi waliosikia, pepo wachafu waliwatoka watu huku wakilia kwa sauti kubwa, na wengi waliopooza na viwete waliponywa.
For the unclean spirits, roaring with great cries, came forth out of many who were possessed: and many who were paralytic and lame were healed.
8 Na kulikuwa na furaha kubwa katika mji.
And there was great joy in that city.
9 Lakini palikuwa na mtu mmoja katika mji ule jina lake Simon, ambaye alikuwa akifanya uchawi; ambao aliutumia kuwashangaza watu wa taifa la Samaria, wakati akisema kuwa yeye ni mtu wa muhimu.
But a certain man, named Simon, lived previously in that city, who practised magic, and astonished the nation of Samaria, giving out himself as an extraordinary great personage:
10 Wasamaria wote tangu mdogo hata mkubwa, wakamsikiliza; wakasema;”mtu huyu ni ile nguvu ya Mungu ambayo ni kuu.”
to whom all gave heed from the small to the great, saying, This man is the great power of God.
11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mrefu kwa uchawi wake.
And to him they attended, because he had of a considerable time astonished them by his magical tricks.
12 Lakini wakati walipoamini kuwa Filipo alihubiri juu ya ufalme wa Mungu na juu ya jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanaume kwa wanawake.
But when they believed Philip, who preached the glad tidings of the things which related to the kingdom of God, and the name of Jesus Christ, they were baptised both men and women.
13 Na Simoni mwenyewe aliamini: baada ya kubatizwa, aliendelea kuwa na Filipo; alipoona ishara na miujiza iliyokuwa ikitendeka, alishangaa.
Then Simon also himself believed: and being baptised, he attached himself to Philip, and beholding the signs and great miracles which were performed, he was astonished.
14 Wakati mitume wa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria imepokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana.
But when the apostles who were at Jerusalem heard that Samaria had received the word of God, they sent unto them Peter and John:
15 Wakati walipokuwa wakishuka wakawaombea; kwamba wampokee Roho Mtakatifu.
who, when they were come down, prayed for them, that they might receive the Holy Ghost:
16 Mpaka muda huo, Roho Mtakatifu alikuwa hajawashukia hata mmoja wao; walikuwa tu wamebatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
for as yet he had not fallen on any one of them: only they had been baptised into the name of the Lord Jesus.
17 Ndipo Petro na Yohana wakawawekea mikono, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Then they laid their hands upon them, and they received the Holy Ghost.
18 Wakati Simoni alipoona kwamba Roho Mtakatifu ametolewa kupitia kuwekewa mikono na mitume; akataka kuwapa pesa,
Now when Simon saw, that by the imposition of the apostles’ hands, the Holy Ghost was given, he offered them money,
19 Akasema, “Nipeni hii nguvu, ili kila nitakayemwekea mikono apokee Roho Mtakatifu.”
saying, Confer on me also this power, that on whomsoever I lay my hands, they may receive the Holy Ghost.
20 Lakini Petro akamwambia; pesa yako pamoja na wewe ipotelee mbali, kwa sababu umedhani kuwa karama ya Mungu inapatikana kwa pesa.
But Peter said unto him, May thy silver with thyself go into perdition, because thou hast imagined that the gift of God can be purchased with money.
21 Hauna sehemu katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mnyoofu mbele za Mungu.
There is for thee neither part nor lot in this word: for thy heart is not right before God.
22 Hivyo basi tubu maovu yako na kumwomba Mungu labda utasamehewe fikra za moyo wako.
Repent therefore of this thy wickedness, and pray to God, if haply this thought of thy heart may be forgiven thee.
23 Kwa maana naona uko katika sumu ya uchungu na kifungo cha dhambi.”
For I see that thou art in the gall of bitterness, and the bond of iniquity.
24 Simoni akajibu na kusema, “Mwombeni Bwana kwa ajili yangu, kwa kuwa mambo yote mliyozungumza yaweza kunitokea.
Then Simon answering said, Pray ye for me unto the Lord, that none of the things which ye have spoken may come upon me.
25 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wameshuhudia na kuhubiri neno la Bwana, walirudi Yerusalemu kwa njia hiyo; walihubiri injili katika vijiji vingi vya Wasamaria.
Then they, after bearing their testimony, and speaking the word of the Lord, returned towards Jerusalem, and preached the gospel in many villages of the Samaritans.
26 Basi malaika wa Bwana akanena na Filipo na kusema, “Angaza na uende kusini katika njia iendayo chini ya Yerusalemu kuelekea Gaza.” ( Njia hii iko katika jangwa).
Now the angel of the Lord spake to Philip, saying, Arise, and go towards the south, on the road which leads down from Jerusalem to Gaza: it is a wilderness.
27 Akaangaza na kwenda. Tazama, kulikuwa na mtu wa Ethiopia, towashi mwenye mamlaka kuu chini ya kandase; malkia wa Ethiopia. Aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu.
And he arose and went: and lo! an Ethiopian man, an eunuch, a person in power under Candace queen of the Ethiopians, who was over all her treasury; he had gone to worship unto Jerusalem,
28 Alikuwa akirejea ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
and was returning, and sitting in his chariot, was reading the prophet Isaiah.
29 Roho akasema na Filipo, “Sogea karibu na gari hili ukashikamane nalo.
Then said the Spirit to Philip, Go up, and approach close to that chariot.
30 “Hivyo Filipo akaenda mbio, akamsikia akisoma katika chuo cha nabii Isaya; akasema, Je unafahamu unachosoma?”
Then Philip running up to him, heard him reading the prophet Isaiah; and he said, Well! but dost thou understand what thou art reading?
31 Muethiopia akasema, “nitawezaje mtu asiponiongoza?” Akamsihi Filipo apande garini na kuketi pamoja naye.
He replied, How indeed can I, except some person guide me in the way? And he besought Philip to come up and sit with him.
32 Sasa fungu la maandiko alilokuwa akisoma Muethiopia ni hili; Aliongozwa kama kondoo kwenda machinjioni kuchinjwa; na kama kondoo alinyamaza kimya, hakufungua kinywa chake:
The portion of scripture which he had been reading was this: “He was led as a sheep to the slaughter; and as a lamb before him who sheareth it is dumb, so he opened not his mouth:
33 Kwa kuhuzunishwa kwake hukumu yake iliondolewa: Nani ataeleza kizazi chake? maisha yake yameondolewa katika nchi.”
in his humiliation his judgment was taken away: but his generation who can describe? for his life was taken away from the earth.”
34 Hivyo towashi akamwuliza Filipo, na kusema, “nakuomba, ni nabii yupi ambaye anaongelewa habari zake, ni kuhusu yeye, au za mtu mwingine”?
Then the eunuch addressing himself to Philip, said, I pray thee, of whom doth the prophet thus speak? of himself, or of some other person?
35 Filipo alianza kuongea, alianza kwa andiko hili la Isaya kumhubiria habari za Yesu.
Then Philip opening his mouth, and beginning from that scripture, preached to him Jesus.
36 Wakiwa njiani, wakafika penye maji,' towashi akasema, “Tazama, pana maji hapa nini kinazuia nisibatizwe?,
But as they went on the road, they came to some water: and the eunuch said, Here is water, what forbids my being baptised?
37 maneno haya, “Hivyo Muethiopia akajibu “naamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,” hayamo kwenyemaandiko ya kale). Ndipo Muethiopia akaamuru gari lisimame.
And Philip said, If thou believest with the whole heart, it is allowable. Then he answered and said, I believe that Jesus Christ is the Son of God.
38 Walikwenda ndani ya maji, pamoja Filipo na towashi, Filipo akambatiza.
And he bid the carriage stop: and they went down both into the water, both Philip and the eunuch; and he baptised him.
39 Wakati walipotoka kwenye maji, Roho wa Bwana ikampeleka Filipo mbali; towashi hakumwona, akaenda njia yake akishangilia.
But when they were come up out of the water, the Spirit of the Lord caught up Philip, and the eunuch saw him no more: then he went on his way rejoicing.
40 Lakini Philipo akatokea Azoto. Alipita katika mkoa ule na kuhubiri injili katika miji yote mpaka alipofika Kaisaria.
But Philip found himself at Azotus: and passing through he preached the gospel in all the cities, until he came to Caesarea.

< Matendo 8 >