< Matendo 8 >
1 Sauli alikuwa kwenye makubaliano ya kifo chake. siku hiyo ndipo alipoanza kuwatesa kinyume cha kanisa lililokuwa Yerusalemu; na waaminio wote waliotawanyika katika majimbo ya Yudea na Samaria, isipokuwa mitume.
And at that time there was a great persecution against the church that was in Jerusalem; and they were all dispersed throughout the regions of Judea and Samaria, except the apostles.
2 Watu wachamungu walimzika Stefano na kufanya maombolezo makubwa juu yake.
But devout men carried Stephen to his burial, and made great lamentation over him.
3 Lakini Sauli alilidhuru sana kanisa. Alikwenda nyumba kwa nyumba na kuwaburuza nje wanawake na waume, na kuwatupia gerezani.
But Saul attempted to destroy the church; entering every house, and dragging men and women, he delivered them up to prison.
4 waaminio ambao walikuwa wametawanyika bado walilihubiri neno.
Then they that were dispersed went everywhere preaching the word.
5 Filipo akashuka katika mji wa Samaria na akamtangaza Kristo huko.
And Philip went down to the city of Samaria, and preached the Christ to them.
6 Baada ya makutano kusikia na kuona ishara alizofanya Filipo; wakaweka umakini juu ya kile alichosema.
And the multitudes with one mind gave heed to the things which were spoken by Philip, when they heard, and saw the signs which he did.
7 Kutoka hapo watu wengi waliosikia, pepo wachafu waliwatoka watu huku wakilia kwa sauti kubwa, na wengi waliopooza na viwete waliponywa.
For unclean spirits, crying with a loud voice, came out of many that were possessed with them, and many paralytics and lame persons were cured.
8 Na kulikuwa na furaha kubwa katika mji.
And there was great joy in that city.
9 Lakini palikuwa na mtu mmoja katika mji ule jina lake Simon, ambaye alikuwa akifanya uchawi; ambao aliutumia kuwashangaza watu wa taifa la Samaria, wakati akisema kuwa yeye ni mtu wa muhimu.
But there was a certain man, named Simon, who had, before this time, been practicing magic in the city, and astonishing the people of Samaria, saying that he was some great one;
10 Wasamaria wote tangu mdogo hata mkubwa, wakamsikiliza; wakasema;”mtu huyu ni ile nguvu ya Mungu ambayo ni kuu.”
to whom they all gave heed, from the least to the greatest, saying: This man is the great power of God.
11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mrefu kwa uchawi wake.
And they gave heed to him because he had, for a long time, astonished them with his magic arts.
12 Lakini wakati walipoamini kuwa Filipo alihubiri juu ya ufalme wa Mungu na juu ya jina la Yesu Kristo, walibatizwa, wanaume kwa wanawake.
But when they believed Philip, who preached the good news concerning the kingdom of God and the name of Jesus Christ, they were immersed, both men and women.
13 Na Simoni mwenyewe aliamini: baada ya kubatizwa, aliendelea kuwa na Filipo; alipoona ishara na miujiza iliyokuwa ikitendeka, alishangaa.
And Simon himself also believed; and after he was immersed, he continued with Philip; and, seeing the mighty deeds and the signs which were done, he was astonished.
14 Wakati mitume wa Yerusalemu waliposikia kuwa Samaria imepokea neno la Mungu, wakawatuma Petro na Yohana.
Now when the apostles, who were in Jerusalem, heard that Samaria had received the word of God, they sent to them Peter and John;
15 Wakati walipokuwa wakishuka wakawaombea; kwamba wampokee Roho Mtakatifu.
who, when they had gone down, prayed for them, that they might receive the Holy Spirit.
16 Mpaka muda huo, Roho Mtakatifu alikuwa hajawashukia hata mmoja wao; walikuwa tu wamebatizwa kwa jina la Bwana Yesu.
For he had not yet fallen on any of them; only they had been immersed into the name of the Lord Jesus.
17 Ndipo Petro na Yohana wakawawekea mikono, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Then they laid their hands on them, and they received the Holy Spirit.
18 Wakati Simoni alipoona kwamba Roho Mtakatifu ametolewa kupitia kuwekewa mikono na mitume; akataka kuwapa pesa,
And when Simon saw that the Holy Spirit was given through the laying on of the hands of the apostles, he offered them money,
19 Akasema, “Nipeni hii nguvu, ili kila nitakayemwekea mikono apokee Roho Mtakatifu.”
saying: Give me, also, this authority, that whoever I shall lay my hands on, may receive the Holy Spirit.
20 Lakini Petro akamwambia; pesa yako pamoja na wewe ipotelee mbali, kwa sababu umedhani kuwa karama ya Mungu inapatikana kwa pesa.
But Peter said to him: Your money perish with you, because you thought that the gift of God might be purchased with money.
21 Hauna sehemu katika jambo hili, kwa sababu moyo wako si mnyoofu mbele za Mungu.
You have neither part nor share in this matter; for your heart is not right in the sight of God.
22 Hivyo basi tubu maovu yako na kumwomba Mungu labda utasamehewe fikra za moyo wako.
Repent, therefore, of this your wickedness, and pray God, if perhaps the purpose of your heart may be forgiven you.
23 Kwa maana naona uko katika sumu ya uchungu na kifungo cha dhambi.”
For I perceive that you are in the gall of bitterness, and in the bond of iniquity.
24 Simoni akajibu na kusema, “Mwombeni Bwana kwa ajili yangu, kwa kuwa mambo yote mliyozungumza yaweza kunitokea.
But Simon answered and said: Pray you both to the Lord for me, that none of the things which you have spoken come upon me.
25 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wameshuhudia na kuhubiri neno la Bwana, walirudi Yerusalemu kwa njia hiyo; walihubiri injili katika vijiji vingi vya Wasamaria.
Then, when they had given their testimony, and preached the word of the Lord, they returned to Jerusalem, and preached the gospel in many villages of the Samaritans.
26 Basi malaika wa Bwana akanena na Filipo na kusema, “Angaza na uende kusini katika njia iendayo chini ya Yerusalemu kuelekea Gaza.” ( Njia hii iko katika jangwa).
And an angel of the Lord spoke to Philip, saying: Arise, and go toward the south, to the road that leads from Jerusalem to Gaza; this is desert.
27 Akaangaza na kwenda. Tazama, kulikuwa na mtu wa Ethiopia, towashi mwenye mamlaka kuu chini ya kandase; malkia wa Ethiopia. Aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu.
And he arose and went. And behold, a man of Ethiopia, a eunuch of great authority under Candace, the queen of the Ethiopians, who had charge of all her treasure, and had come to Jerusalem to worship,
28 Alikuwa akirejea ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
was returning, and, sitting in his chariot, read the prophet Isaiah.
29 Roho akasema na Filipo, “Sogea karibu na gari hili ukashikamane nalo.
And the Spirit said to Philip: Go forward and join yourself to this chariot.
30 “Hivyo Filipo akaenda mbio, akamsikia akisoma katika chuo cha nabii Isaya; akasema, Je unafahamu unachosoma?”
And Philip ran forward, and heard him reading the prophet Isaiah; and he said: Do you understand what you are reading?
31 Muethiopia akasema, “nitawezaje mtu asiponiongoza?” Akamsihi Filipo apande garini na kuketi pamoja naye.
He answered: How can I, unless some one instruct me? And he invited Philip to come up and sit with him.
32 Sasa fungu la maandiko alilokuwa akisoma Muethiopia ni hili; Aliongozwa kama kondoo kwenda machinjioni kuchinjwa; na kama kondoo alinyamaza kimya, hakufungua kinywa chake:
The passage of the scripture which he was reading, was this: As a sheep for the slaughter was he led; and as a lamb before his shearer is dumb, so opened he not his mouth
33 Kwa kuhuzunishwa kwake hukumu yake iliondolewa: Nani ataeleza kizazi chake? maisha yake yameondolewa katika nchi.”
in his humiliation. The sentence against him was taken away; but who shall describe the men of his generation? For his life was taken from the earth.
34 Hivyo towashi akamwuliza Filipo, na kusema, “nakuomba, ni nabii yupi ambaye anaongelewa habari zake, ni kuhusu yeye, au za mtu mwingine”?
And the eunuch answered Philip, and said: I pray you, of whom speaks the prophet this? Of himself, or of some other man?
35 Filipo alianza kuongea, alianza kwa andiko hili la Isaya kumhubiria habari za Yesu.
And Philip opened his mouth, and began at the same scripture, and preached to him Jesus.
36 Wakiwa njiani, wakafika penye maji,' towashi akasema, “Tazama, pana maji hapa nini kinazuia nisibatizwe?,
And as they went along the road, they came to some water; and the eunuch said: See, here is water; what hinders me from being immersed?
37 maneno haya, “Hivyo Muethiopia akajibu “naamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,” hayamo kwenyemaandiko ya kale). Ndipo Muethiopia akaamuru gari lisimame.
38 Walikwenda ndani ya maji, pamoja Filipo na towashi, Filipo akambatiza.
And he commanded the chariot to stand still; and they both went down into the water, both Philip and the eunuch, and he immersed him.
39 Wakati walipotoka kwenye maji, Roho wa Bwana ikampeleka Filipo mbali; towashi hakumwona, akaenda njia yake akishangilia.
And when they came up out of the water, the Spirit of the Lord caught away Philip; and the eunuch saw him no more, for he went on his way rejoicing.
40 Lakini Philipo akatokea Azoto. Alipita katika mkoa ule na kuhubiri injili katika miji yote mpaka alipofika Kaisaria.
But Philip was found at Azotus, and, passing through, he preached the gospel in all the cities, till he came to Cæsarea