< Matendo 7 >

1 Kuhani mkuu akasema,”mambo haya ni ya kweli”?
And the prynce of prestis seide to Steuene, Whethir these thingis han hem so?
2 Stephano akasema, “Ndugu na mababa zangu, nisikilizeni mimi: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Abrahamu wakati alipokuwa Mesopotamia, kabla hajaishi Harani,'
Which seide, Britheren and fadris, here ye. God of glorie apperide to oure fadir Abraham, whanne he was in Mesopotamie, bifor that he dwelte in Carram, and seide to hym,
3 akamwambia,' Ondoka katika nchi yako na jamaa zako na uende katika nchi nitakayokuonyesha'.
Go out of thi loond, and of thi kynrede, and come in to the loond, which Y schal schewe to thee.
4 Kisha akaondoka katika nchi ya Ukaldayo akaishi Harani, kutoka hapo, baada ya baba yake kufa, Mungu akamleta kwenye nchi hii, wanayoishi sasa.
Thanne he wente out of the loond of Caldeis, and dwelte in Carram. And fro thens aftir that his fader was deed, he translatide him in to this loond, in which ye dwellen now.
5 Hakumpa chochote kama urithi wake, hapakuwa na sehemu hata ya kuweka mguu. Lakini Abrahamu aliahidiwa hata kabla hajapata mtoto kuwa atapewa nchi kama miliki yake na uzao wake.
And he yaf not to hym eritage in it, nethir a paas of a foot, but he bihiyte to yyue hym it in to possessioun, and to his seed aftir hym, whanne he hadde not a sone.
6 Mungu alinena naye hivi, ya kwamba wazao wake wangeishi katika nchi ya ugeni, na kwamba wenyeji wa huko watawafanya kuwa watumwa wao na kuwatenda vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
And God spak to hym, That his seed schal be comling in an alien lond, and thei schulen make hem suget to seruage, and schulen yuel trete hem, foure hundrid yeris and thritti;
7 Na Mungu akasema, nitalihukumu taifa ambalo litawafanya mateka, na baada ya hapo watatoka na kuniabudu katika sehemu hii.'
and Y schal iuge the folk, to which thei schulen serue, seith the Lord. And after these thingis thei schulen go out, and thei schulen serue to me in this place.
8 Na akampa Abrahamu agano la tohara, hivyo Abrahamu akawa baba wa Isaka akamtahiri siku ya nane; Isaka akawa baba wa Yakobo, na Yakobo akawa baba wa mababu zetu kumi na wawili.
And he yaf to hym the testament of circumcisioun; and so he gendride Ysaac, and circumcidide hym in the eiyt dai. And Isaac gendride Jacob, and Jacob gendride the twelue patriarkis.
9 Mababu zetu wakamwonea wivu Yusufu wakamuuza katika nchi ya Misri, na Mungu alikuwa pamoja naye,
And the patriarkis hadden enuye to Joseph, and selden hym in to Egipt.
10 na akamwokoa katika mateso yake, na akampa fadhili na hekima mbele ya Farao mfalme wa Misri. Farao akamfanya awe mtawala juu ya Misri na juu ya nyumba yake yote.
And God was with hym, and delyuerede hym of alle hise tribulaciouns, and yaf to hym grace and wisdom in the siyt of Farao, king of Egipt. And he ordeynede hym souereyn on Egipt, and on al his hous.
11 Basi kukawa na njaa kuu na mateso mengi katika nchi ya Misri na Kanani, na baba zetu hawakupata chakula.
And hungur cam in to al Egipt, and Canaan, and greet tribulacioun; and oure fadris founden not mete.
12 Lakini Yakobo aliposikia kuna nafaka Misri, aliwatuma baba zetu kwa mara ya kwanza.
But whanne Jacob hadde herd, that whete was in Egipt, he sente oure fadris first.
13 Katika safari ya pili Yusufu akajionyesha kwa ndugu zake, familia ya Yusufu ikajulikana kwa Farao.
And in the secounde tyme Joseph was knowun of hise britheren, and his kyn was maad knowun to Farao.
14 Yusufu akawatuma ndugu zake kwenda kumwambia Yakobo baba yao aje Misri, pamoja na jamaa yake, jumla ya watu wote ni sabini na tano.
And Joseph sente, and clepide Jacob, his fadir, and al his kynrede, seuenti and fyue men.
15 Hivyo Yakobo akashuka Misri; kisha akafa yeye pamoja na baba zetu.
And Jacob cam doun in to Egipt, and was deed, he and oure fadris;
16 Wakachukuliwa hata Shekemu wakazikwa katika kaburi ambalo Abrahamu alilinunua kwa vipande vya fedha kutoka kwa wana wa Hamori huko Shekemu.
and thei weren translatid in to Sichen, and weren leid in the sepulcre, that Abraham bouyte bi prijs of siluer of the sones of Emor, the sone of Sichen.
17 Wakati wa ile ahadi ambayo Mungu alimwahidi Abrahamu ulipokaribia, watu wakiwa wameongezeka huko Misri,
And whanne the tyme of biheeste cam niy, which God hadde knoulechid to Abraham, the puple waxede, and multipliede in Egipt,
18 wakati huo aliinuka mfalme mwingine juu ya Misri, mfalme asiyejua kuhusu Yusufu.
til another kyng roos in Egipt, which knewe not Joseph.
19 Huyo mfalme mwingine akawadanganya watu wetu na kuwatenda mabaya baba zetu, na kuwatupa watoto wao wachanga ili wasiishi.
This bigilide oure kyn, and turmentide oure fadris, that thei schulden putte awey her yonge children, for thei schulden not lyue.
20 Katika kipindi kile Musa alizaliwa; alikuwa mzuri mbele za Mungu, akalelewa miezi mitatu katika nyumba ya baba yake.
In the same tyme Moyses was borun, and he was louyd of God; and he was norischid thre monethis in the hous of his fadir.
21 Wakati alipotupwa, binti wa Farao alimchukua akamlea kama mwanaye.
And whanne he was put out in the flood, the douyter of Farao took hym vp, and nurischide hym in to hir sone.
22 Musa alifundishwa mafundisho yote ya Kimisri; alikuwa na nguvu katika maneno na matendo.
And Moises was lerned in al the wisdom of Egipcians, and he was myyti in his wordis and werkis.
23 Lakini baada ya kutimiza miaka arobaini, ikamjia katika moyo wake kuwatembelea ndugu zake, wana wa Israeli.
But whanne the tyme of fourti yeer was fillid to hym, it roos vp `in to his herte, that he schulde visite hise britheren, the sones of Israel.
24 Alipomwona Mwisraeli akitendewa mabaya, Musa alimtetea na kulipiza kisasi aliyekuwa akimwonea kwa kumpiga Mmisiri:
And whanne he say a man suffringe wronge, he vengide hym, and dide veniaunce for hym that suffride the wronge, and he killide the Egipcian.
25 akifikiri kuwa ndugu zake watafahamu kwamba Mungu anawaokoa kwa mkono wake, lakini hawakufahamu.
For he gesside that his britheren schulden vndurstonde, that God schulde yyue to hem helthe bi the hoond of hym; but thei vndurstoden not.
26 Siku iliyofuata akaenda kwa baadhi ya Waisraeli waliokuwa wanagombana; akajaribu kuwapatanisha; akisema,' Mabwana, Ninyi ni ndugu; mbona mnakoseana ninyi kwa ninyi?
For in the dai suynge he apperide to hem chidinge, and he acordide hem in pees, and seide, Men, ye ben britheren; whi noyen ye ech othere?
27 Lakini aliyemkosea jirani yake akamsukumia mbali, na kusema, 'Nani kakufanya mtawala na muhukumu wetu?
But he that dide the wronge to his neiybore, puttide hym awey, and seide, Who ordeynede thee prince and domesman on vs?
28 Wewe unataka kuniua, kama ulivyomuua Mmisri jana?”
Whethir thou wolt sle me, as yistirdai thou killidist the Egipcian?
29 Musa akakimbia baada ya kusikia hivyo; akawa mgeni katika nchi ya Midiani, ambapo akawa baba wa wana wawili.
And in this word Moises flei, and was maad a comeling in the loond of Madian, where he bigat twei sones.
30 Baada ya miaka arobaini kupita, malaika akamtokea katika jangwa la mlima Sinai, katika mwali wa moto ndani ya kichaka.
And whanne he hadde fillid fourti yeer, an aungel apperide to hym in fier of flawme of a buysch, in desert of the mount of Syna.
31 Wakati Musa alipoona moto, alishangaa na kustaajabia kile alichokiona, na alipojaribu kukisogelea ili kukitazama, sauti ya Bwana ikamjia Ikisema,
And Moises siy, and wondride on the siyt. And whanne he neiyede to biholde, the vois of the Lord was maad to hym,
32 'Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, na wa Isaka, na wa Yakobo'. Musa alitetemeka na hakuthubutu kuangalia.
and seide, Y am God of youre fadris, God of Abraham, God of Ysaac, God of Jacob. Moises was maad tremblynge, and durste not biholde.
33 Bwana akamwambia, 'Vua viatu vyako, sehemu uliposimama ni mahali patakatifu.
But God seide to hym, Do of the schoon of thi feet, for the place in which thou stondist is hooli erthe.
34 Nimeona mateso ya watu wangu waliopo Misri; Nimesikia kuugua kwao, nami nimeshuka ili niwaokoe; sasa njoo, nitakutuma wewe Misri.'
Y seynge say the turmentyng of my puple that is in Egipt, and Y herde the mornyng of hem, and Y cam doun to delyuere hem. And now come thou, and Y schal sende thee in to Egipt.
35 Huyu Musa ambaye waliyemkataa, wakati waliposema, 'nani kakufanya kuwa mtawala na mwamuzi wetu?' alikuwa ndiye ambaye Mungu alimtuma awe mtawala na mkombozi. Mungu alimtuma kwa mkono wa malaika ambaye alimtokea Musa kichakani.
This Moises whom thei denyeden, seiynge, Who ordeynede thee prince and domesman on vs? God sente this prince and ayenbiere, with the hoond of the aungel, that apperide to hym in the busch.
36 Musa aliwaongoza kutoka Misri baada ya kufanya miujiza na ishara katika Misri na katika bahari ya Shamu, na katika jangwa kwa kipindi cha miaka arobaini.
This Moises ledde hem out, and dide wondris and signes in the loond of Egipt, and in the reed see, and in desert fourti yeeris.
37 Ni Musa huyu ndiye aliyewambia watu wa Isiraeli kuwa, 'Mungu atawainulieni nabii kutoka miongoni mwa ndugu zenu, nabii kama mimi'.
This is Moises, that seide to the sones of Israel, God schal reise to you a profete of youre bretheren, as me ye schulen here him.
38 Huyu ni mtu ambaye alikuwa katika mkutano jangwani na malaika ambaye aliongea naye katika mlima Sinai. Huyu ndiye mtu ambaye alikuwa na baba zetu, huyu ni mtu ambaye alipokea neno lililo hai na kutupatia sisi.
This it is, that was in the chirche in wildirnesse, with the aungel that spak to hym in the mount of Syna, and with oure fadris; which took words of lijf to yyue to vs.
39 Huyu ni mtu ambaye baba zetu walikataa kumtii; walimsukumia mbali, na katika mioyo yao waligeukia Misri.
To whom oure fadris wolden not obeie, but puttiden hym awei, and weren turned awei in hertis in to Egipt,
40 Katika kipindi hicho walimwambia Haruni.'tutengenezee miungu itakayotuongoza. Huyo Musa, aliyekuwa akituongoza kutoka katika nchi ya Misri, hatujui kilichompata.'
seiynge to Aaron, Make thou to vs goddis, that schulen go bifore vs; for to this Moyses that ledde vs out of the lond of Egipt, we witen not what is don to hym.
41 Hivyo wakatengeneza ndama kwa siku hizo na wakatoa sadaka kwa hiyo sananmu na wakafurahi kwa sababu ya kazi ya mikono yao.
And thei maden a calf in tho daies, and offriden a sacrifice to the mawmet; and thei weren glad in the werkis of her hondis.
42 Lakini Mungu aliwageuza na kuwapa waabudu nyota wa angani, kama ilivyoandikwa kwenye kitabu cha manabii, 'Je Mmenitolea mimi sadaka za wanyama mliowachinja jangwani kwa muda wa miaka arobaini, nyumba ya Israeli?
And God turnede, and bitook hem to serue to the knyythod of heuene, as it is writun in the book of profetis, Whether ye, hous of Israel, offriden to me slayn sacrificis, ether sacrificis, fourti yeris in desert?
43 Mmekubali hema ya kukutania ya Moleki na nyota ya mungu refani, na picha mliyoitengeneza na kuwaabudu wao: na nitawapeleka mbali zaidi ya Babeli.'
And ye han take the tabernacle of Moloc, and the sterre of youre god Renfam, figuris that ye han maad to worschipe hem; and Y schal translate you in to Babiloyn.
44 Baba zetu walikuwa na hema ya kukutania ya ushuhuda jangwani, kama Mungu alivyoamuru alipoongea na Musa, kwamba angeitengeneza kwa mfano wa ule aliouona.
The tabernacle of witnessing was with oure fadris in desert, as God disposide to hem, and spak to Moyses, that he schulde make it aftir the fourme that he say.
45 Hili ni hema ambalo baba zetu, kwa wakati wao, waliletwa katika nchi na Joshua. Hii ilitokea wakati walipoingia kumiliki taifa ambalo Mungu aliwafukuza kabla ya uwepo wa baba zetu. Hii ilikuwa hivi hadi siku za Daudi,
Which also oure fadris token with Jhesu, and brouyten in to the possessioun of hethene men, whiche God puttide awey fro the face of oure fadris, til in to the daies of Dauid,
46 ambaye alipata kibali machoni pa Mungu,' na akaomba kutafuta makao kwa Mungu wa Yakobo.
that fonde grace anentis God, and axide that he schulde fynde a tabernacle to God of Jacob.
47 Lakini Selemani alimjengea nyumba ya Mungu.
But Salomon bildide the hous `to hym.
48 Hata hivyo Aliye Juu haishi kwenye nyumba zilizojengwa kwa mikono; hii ni kama nabii alivyosema,
But the hiy God dwellith not in thingis maad bi hoond,
49 Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni sehemu ya kuwekea miguu yangu. Nyumba ya aina gani mtanijengea?, asema Bwana: au ni wapi sehemu yangu ya kupumzikia?
as he seith bi the profete, Heuene is a seete to me, and the erthe is the stool of my feet; what hous schulen ye bilde to me, seith the Lord, ether what place is of my restyng?
50 Siyo mkono wangu uliofanya hivi vitu vyote?'
Whether myn hoond made not alle these thingis?
51 Enyi watu wenye shingo ngumu msiotahiriwa mioyo na masikio, kila mara mnampinga Roho Mtakatifu,' mnatenda kama baba zenu walivyotenda.
With hard nol, and vncircumcidid hertis and eris ye withstoden eueremore the Hooli Goost; and as youre fadris, so ye.
52 Ni nabii gani katika manabii ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua manabii wote waliotokea kabla ya ujio wa Mmoja mwenye Haki,'na sasa mmekuwa wasaliti na wauaji wake pia,
Whom of the profetis han not youre fadris pursued, and han slayn hem that bifor telden of the comyng of the riytful man, whos traitouris and mansleeris ye weren now?
53 enyi watu mliopokea sheria ile iliyoagizwa na malaika lakini hamkuishika.”
Whiche token the lawe in ordynaunce of aungels, and han not kept it.
54 Kisha wajumbe wa baraza waliposikia mambo haya, walichomwa mioyo yao, wakamsagia meno Stefano.
And thei herden these thingis, and weren dyuersli turmentid in her hertis, and grenneden with teeth on hym.
55 Lakini yeye, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alitazama mbinguni kwa makini na akauona utukufu wa Mungu,' na kumwona Yesu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
But whanne Steuene was ful of the Hooli Goost, he bihelde in to heuene, and say the glorie of God, and Jhesu stondinge on the riythalf of the vertu of God.
56 Stefano akasema, “Angalia nimeona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adam amesimama mkono wa kuume wa Mungu.”
And he seide, Lo! Y se heuenes openyd, and mannus sone stondynge on the riythalf of the vertu of God.
57 Lakini wajumbe wa baraza wakapiga kelele kwa sauti za juu, wakaziba masikio yao, wakamkimbilia kwa pamoja,
And thei crieden with a greet vois, and stoppiden her eris, and maden with o wille an assauyt in to hym.
58 wakamtupa nje ya mji na wakampiga mawe: na mashahidi wakavua nguo zao za nje na kuweka chini karibu na miguu ya kijana aliyeitwa Sauli.
And thei brouyten hym out of the citee, and stonyden. And the witnessis diden of her clothis, bisidis the feet of a yong man, that was clepid Saule.
59 Walipokuwa wakimpiga mawe Stefano, aliendelea kumwita Bwana na kusema, “Bwana Yesu, pokea roho yangu,”.
And thei stonyden Steuene, that clepide God to help, seiynge, Lord Jhesu, resseyue my spirit.
60 Akapiga magoti na kuita kwa sauti kubwa, “Bwana, usiwahesabie dhambi hii. “Aliposema haya, akakata roho.
And he knelide, and criede with a greet vois, and seide, Lord, sette not to hem this synne. And whanne he hadde seid this thing, he diede.

< Matendo 7 >