< Matendo 7 >
1 Kuhani mkuu akasema,”mambo haya ni ya kweli”?
And the chief priest said: Are these things so?
2 Stephano akasema, “Ndugu na mababa zangu, nisikilizeni mimi: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Abrahamu wakati alipokuwa Mesopotamia, kabla hajaishi Harani,'
He replied: Brethren and fathers, hear: The God of glory appeared to our father Abraham, while he was in Mesopotamia, before he dwelt in Charran,
3 akamwambia,' Ondoka katika nchi yako na jamaa zako na uende katika nchi nitakayokuonyesha'.
and said to him: Get out from your land, and from your kindred, and come into a land that I will show you.
4 Kisha akaondoka katika nchi ya Ukaldayo akaishi Harani, kutoka hapo, baada ya baba yake kufa, Mungu akamleta kwenye nchi hii, wanayoishi sasa.
Then he departed from the land of the Chaldeans, and dwelt in Charran; and thence, after his father died, he removed into this land, in which you now dwell.
5 Hakumpa chochote kama urithi wake, hapakuwa na sehemu hata ya kuweka mguu. Lakini Abrahamu aliahidiwa hata kabla hajapata mtoto kuwa atapewa nchi kama miliki yake na uzao wake.
And he gave him no inheritance in it, not a foot breadth: and yet he promised to give it for a possession to him, and to his posterity after him, when as yet he had no child.
6 Mungu alinena naye hivi, ya kwamba wazao wake wangeishi katika nchi ya ugeni, na kwamba wenyeji wa huko watawafanya kuwa watumwa wao na kuwatenda vibaya kwa muda wa miaka mia nne.
And God spoke thus: That his posterity should sojourn in a strange land, and they should enslave them and afflict them, for four hundred years.
7 Na Mungu akasema, nitalihukumu taifa ambalo litawafanya mateka, na baada ya hapo watatoka na kuniabudu katika sehemu hii.'
And the nation to which they shall be in bondage I will judge, said God; and after that, they shall come forth and serve me in this place.
8 Na akampa Abrahamu agano la tohara, hivyo Abrahamu akawa baba wa Isaka akamtahiri siku ya nane; Isaka akawa baba wa Yakobo, na Yakobo akawa baba wa mababu zetu kumi na wawili.
And he gave him the covenant of circumcision, and thus he begot Isaac, and circumcised him the eighth day; and Isaac begot Jacob, and Jacob begot the twelve patriarchs.
9 Mababu zetu wakamwonea wivu Yusufu wakamuuza katika nchi ya Misri, na Mungu alikuwa pamoja naye,
And the patriarchs, moved with envy, sold Joseph into Egypt: but God was with him,
10 na akamwokoa katika mateso yake, na akampa fadhili na hekima mbele ya Farao mfalme wa Misri. Farao akamfanya awe mtawala juu ya Misri na juu ya nyumba yake yote.
and delivered him from all his afflictions, and gave him favor and wisdom in the sight of Pharoah, king of Egypt: and he made him governor over Egypt, and his whole house.
11 Basi kukawa na njaa kuu na mateso mengi katika nchi ya Misri na Kanani, na baba zetu hawakupata chakula.
And there came a famine, and great affliction on the whole land of Egypt, and of Chanaan: and our fathers found no sustenance.
12 Lakini Yakobo aliposikia kuna nafaka Misri, aliwatuma baba zetu kwa mara ya kwanza.
But when Jacob heard that there was grain in Egypt, he sent forth our fathers the first time:
13 Katika safari ya pili Yusufu akajionyesha kwa ndugu zake, familia ya Yusufu ikajulikana kwa Farao.
and, on their second visit, Joseph made himself known to his brothers, and the kindred of Joseph were made known to Pharaoh.
14 Yusufu akawatuma ndugu zake kwenda kumwambia Yakobo baba yao aje Misri, pamoja na jamaa yake, jumla ya watu wote ni sabini na tano.
And Joseph sent and called to him his father Jacob, and all his kindred, seventy-five souls.
15 Hivyo Yakobo akashuka Misri; kisha akafa yeye pamoja na baba zetu.
And Jacob went down into Egypt, and died, himself and our fathers;
16 Wakachukuliwa hata Shekemu wakazikwa katika kaburi ambalo Abrahamu alilinunua kwa vipande vya fedha kutoka kwa wana wa Hamori huko Shekemu.
and they were carried over into Sychem, and laid in the sepulcher which Abraham bought for its value in silver, from the sons of Emmor, the father of Sychem.
17 Wakati wa ile ahadi ambayo Mungu alimwahidi Abrahamu ulipokaribia, watu wakiwa wameongezeka huko Misri,
And as the time of the promise which God had made with an oath to Abraham drew near, the people increased and multiplied in Egypt,
18 wakati huo aliinuka mfalme mwingine juu ya Misri, mfalme asiyejua kuhusu Yusufu.
till another king arose, who knew not Joseph.
19 Huyo mfalme mwingine akawadanganya watu wetu na kuwatenda mabaya baba zetu, na kuwatupa watoto wao wachanga ili wasiishi.
He dealt insidiously with our race, and afflicted our fathers, so that they exposed their infants, in order that they might not live.
20 Katika kipindi kile Musa alizaliwa; alikuwa mzuri mbele za Mungu, akalelewa miezi mitatu katika nyumba ya baba yake.
At which time Moses was born; and he was exceedingly beautiful, and was nursed three months in his father’s house.
21 Wakati alipotupwa, binti wa Farao alimchukua akamlea kama mwanaye.
But having been exposed, the daughter of Pharaoh took him up, and educated him as her own son.
22 Musa alifundishwa mafundisho yote ya Kimisri; alikuwa na nguvu katika maneno na matendo.
And Moses was instructed in all the wisdom of the Egyptians, and was mighty in words and in deeds.
23 Lakini baada ya kutimiza miaka arobaini, ikamjia katika moyo wake kuwatembelea ndugu zake, wana wa Israeli.
When he had completed his fortieth year, it came into his heart to visit his brethren, the sons of Israel.
24 Alipomwona Mwisraeli akitendewa mabaya, Musa alimtetea na kulipiza kisasi aliyekuwa akimwonea kwa kumpiga Mmisiri:
And seeing one of them unjustly treated, he defended and avenged him that was oppressed, and smote the Egyptian.
25 akifikiri kuwa ndugu zake watafahamu kwamba Mungu anawaokoa kwa mkono wake, lakini hawakufahamu.
And he supposed that his brethren would understand that, by his hand, God would give them salvation: but they understood not.
26 Siku iliyofuata akaenda kwa baadhi ya Waisraeli waliokuwa wanagombana; akajaribu kuwapatanisha; akisema,' Mabwana, Ninyi ni ndugu; mbona mnakoseana ninyi kwa ninyi?
And on the next day he showed himself to them, as they were fighting, and endeavored to persuade them to peace, saying, Men, you are brothers: why do you injure one another?
27 Lakini aliyemkosea jirani yake akamsukumia mbali, na kusema, 'Nani kakufanya mtawala na muhukumu wetu?
But he that was doing the injury to his neighbor, thrust him away, saying, Who made you a ruler or a judge over us?
28 Wewe unataka kuniua, kama ulivyomuua Mmisri jana?”
Do you intend to kill me, as you killed the Egyptian yesterday?
29 Musa akakimbia baada ya kusikia hivyo; akawa mgeni katika nchi ya Midiani, ambapo akawa baba wa wana wawili.
And at that saying Moses fled, and became a resident in the land of Midian, where he begot two sons.
30 Baada ya miaka arobaini kupita, malaika akamtokea katika jangwa la mlima Sinai, katika mwali wa moto ndani ya kichaka.
And when forty years were completed, there appeared to him, in the wilderness of Mount Sinai, an angel of the Lord in a flame of fire in a bush.
31 Wakati Musa alipoona moto, alishangaa na kustaajabia kile alichokiona, na alipojaribu kukisogelea ili kukitazama, sauti ya Bwana ikamjia Ikisema,
When Moses saw it, he wondered at the sight, and as he was drawing near to observe it, the voice of the Lord came to him:
32 'Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Abrahamu, na wa Isaka, na wa Yakobo'. Musa alitetemeka na hakuthubutu kuangalia.
I am the God of your fathers, the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob. And Moses trembled, and durst not observe it.
33 Bwana akamwambia, 'Vua viatu vyako, sehemu uliposimama ni mahali patakatifu.
Then said the Lord to him: Loose your shoes from your feet; for the place in which you stand is holy ground.
34 Nimeona mateso ya watu wangu waliopo Misri; Nimesikia kuugua kwao, nami nimeshuka ili niwaokoe; sasa njoo, nitakutuma wewe Misri.'
I have surely seen the affliction of my people who are in Egypt, and I have heard their groaning, and I have come down to deliver them; and now come, and I will send you into Egypt.
35 Huyu Musa ambaye waliyemkataa, wakati waliposema, 'nani kakufanya kuwa mtawala na mwamuzi wetu?' alikuwa ndiye ambaye Mungu alimtuma awe mtawala na mkombozi. Mungu alimtuma kwa mkono wa malaika ambaye alimtokea Musa kichakani.
This Moses, whom they rejected, saying, Who made you a ruler and a judge? him God sent as a ruler and as a redeemer, by the hand of the angel that appeared to him in the bush.
36 Musa aliwaongoza kutoka Misri baada ya kufanya miujiza na ishara katika Misri na katika bahari ya Shamu, na katika jangwa kwa kipindi cha miaka arobaini.
He brought them out, after he had performed wonders and signs in the land of Egypt, and at the Red Sea, and in the wilderness, forty years.
37 Ni Musa huyu ndiye aliyewambia watu wa Isiraeli kuwa, 'Mungu atawainulieni nabii kutoka miongoni mwa ndugu zenu, nabii kama mimi'.
This is that Moses, who said to the sons of Israel, A prophet like me will the Lord your God raise up for you from among your brethren; him shall you hear.
38 Huyu ni mtu ambaye alikuwa katika mkutano jangwani na malaika ambaye aliongea naye katika mlima Sinai. Huyu ndiye mtu ambaye alikuwa na baba zetu, huyu ni mtu ambaye alipokea neno lililo hai na kutupatia sisi.
This is he who was in the congregation in the wilderness with the angel that spoke to him in the mount Sina, and with our fathers; he received the living oracles, that he might give them to us.
39 Huyu ni mtu ambaye baba zetu walikataa kumtii; walimsukumia mbali, na katika mioyo yao waligeukia Misri.
To him our fathers were not willing to be obedient; but they rejected him, and turned back in their hearts to Egypt,
40 Katika kipindi hicho walimwambia Haruni.'tutengenezee miungu itakayotuongoza. Huyo Musa, aliyekuwa akituongoza kutoka katika nchi ya Misri, hatujui kilichompata.'
saying to Aaron: Make us gods that shall go before us; for, as for this Moses, who brought us out of the land of Egypt, we know not what has become of him.
41 Hivyo wakatengeneza ndama kwa siku hizo na wakatoa sadaka kwa hiyo sananmu na wakafurahi kwa sababu ya kazi ya mikono yao.
And they made a calf in those days, and offered sacrifice to the idol, and rejoiced in the works of their own hands.
42 Lakini Mungu aliwageuza na kuwapa waabudu nyota wa angani, kama ilivyoandikwa kwenye kitabu cha manabii, 'Je Mmenitolea mimi sadaka za wanyama mliowachinja jangwani kwa muda wa miaka arobaini, nyumba ya Israeli?
But God turned and delivered them up to serve the host of heaven, as it is written in the book of the prophets: Your victims and your sacrifices did you offer to me for forty years in the wilderness, O house of Israel?
43 Mmekubali hema ya kukutania ya Moleki na nyota ya mungu refani, na picha mliyoitengeneza na kuwaabudu wao: na nitawapeleka mbali zaidi ya Babeli.'
Yes, you took up the tabernacle of Moloch, and the star of your God Remphan, images which you made to worship; and I will carry you away beyond Babylon.
44 Baba zetu walikuwa na hema ya kukutania ya ushuhuda jangwani, kama Mungu alivyoamuru alipoongea na Musa, kwamba angeitengeneza kwa mfano wa ule aliouona.
The tabernacle of the testimony was with our fathers in the wilderness, built as he who spoke to Moses commanded him to build it, according to the pattern which he had seen:
45 Hili ni hema ambalo baba zetu, kwa wakati wao, waliletwa katika nchi na Joshua. Hii ilitokea wakati walipoingia kumiliki taifa ambalo Mungu aliwafukuza kabla ya uwepo wa baba zetu. Hii ilikuwa hivi hadi siku za Daudi,
which our fathers, who were with Joshua, received by succession, and brought into the land possessed by the Gentiles, whom God continued to drive out from the face of our fathers till the days of David,
46 ambaye alipata kibali machoni pa Mungu,' na akaomba kutafuta makao kwa Mungu wa Yakobo.
who found favor before God, and desired to find a dwelling-place for the God of Jacob.
47 Lakini Selemani alimjengea nyumba ya Mungu.
But Solomon built him a house.
48 Hata hivyo Aliye Juu haishi kwenye nyumba zilizojengwa kwa mikono; hii ni kama nabii alivyosema,
Yet the Most High dwells not in temples made with hands, as says the prophet:
49 Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni sehemu ya kuwekea miguu yangu. Nyumba ya aina gani mtanijengea?, asema Bwana: au ni wapi sehemu yangu ya kupumzikia?
Heaven is my throne, and the earth is my footstool. What house will you build me? says the Lord; or what is the place of my rest?
50 Siyo mkono wangu uliofanya hivi vitu vyote?'
Has not my hand made all these things?
51 Enyi watu wenye shingo ngumu msiotahiriwa mioyo na masikio, kila mara mnampinga Roho Mtakatifu,' mnatenda kama baba zenu walivyotenda.
You stiff-necked, and uncircumcised in heart and in ears, you do always resist the Holy Spirit; as your fathers did, so also do you.
52 Ni nabii gani katika manabii ambaye baba zenu hawakumtesa? Waliwaua manabii wote waliotokea kabla ya ujio wa Mmoja mwenye Haki,'na sasa mmekuwa wasaliti na wauaji wake pia,
Which of the prophets did not your fathers persecute? They slew also those who foretold the coming of the Just One, of whom you have now become the betrayers and murderers;
53 enyi watu mliopokea sheria ile iliyoagizwa na malaika lakini hamkuishika.”
who received the law by the appointment of angels, and have not kepi, it.
54 Kisha wajumbe wa baraza waliposikia mambo haya, walichomwa mioyo yao, wakamsagia meno Stefano.
When they heard these things, they were enraged in their hearts, and gnashed upon him with their teeth.
55 Lakini yeye, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alitazama mbinguni kwa makini na akauona utukufu wa Mungu,' na kumwona Yesu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
But being full of the Holy Spirit, he looked earnestly up into heaven, and saw the glory of God, and Jesus standing at the right hand of God;
56 Stefano akasema, “Angalia nimeona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adam amesimama mkono wa kuume wa Mungu.”
and he said: Behold, I see the heavens opened, and the Son of man standing at the right hand of God.
57 Lakini wajumbe wa baraza wakapiga kelele kwa sauti za juu, wakaziba masikio yao, wakamkimbilia kwa pamoja,
And they cried out with a loud voice, and stopped their ears, and, with one consent, rushed upon him,
58 wakamtupa nje ya mji na wakampiga mawe: na mashahidi wakavua nguo zao za nje na kuweka chini karibu na miguu ya kijana aliyeitwa Sauli.
and drove him out of the city, and stoned him. And the witnesses laid down their clothes at the feet of a young man called Saul.
59 Walipokuwa wakimpiga mawe Stefano, aliendelea kumwita Bwana na kusema, “Bwana Yesu, pokea roho yangu,”.
And they stoned Stephen while he was calling on the Lord, and saying: Lord Jesus, receive my spirit.
60 Akapiga magoti na kuita kwa sauti kubwa, “Bwana, usiwahesabie dhambi hii. “Aliposema haya, akakata roho.
And he kneeled down and cried with a loud voice: Lord, let not this sin stand against them. And when he had said this, he fell asleep. And Saul was well pleased with his death.