< Matendo 6 >

1 Sasa katika siku hizi, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa inaongezeka, lalamiko la Wayahudi wa Kiyunani lilianza dhidi ya Waebrania, kwa sababu wajane wao walikuwa wanasahaulika katika mgao wa kila siku wa chakula.
En ce temps-là, le nombre des disciples s'étant accru, les hellénistes élevèrent des plaintes contre les hébreux, parce que leurs veuves étaient négligées dans l'assistance journalière.
2 Mitume kumi na wawili waliwaita kusanyiko lote la wanafunzi na kusema, “Siyo sahihi kwetu kuliacha neno la Mungu na kuhudumia mezani.
Les Douze ayant convoqué la multitude des disciples, dirent: «Il ne convient pas que nous abandonnions la prédication de la parole de Dieu pour servir aux tables;
3 Kwa hiyo, ndugu, chagueni, wanaume saba, kutoka miongoni mwenu, watu wema, waliojaa Roho na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi huduma hii.
cherchez donc parmi vous, frères, sept hommes de bon renom, pleins d'esprit et de sagesse, que nous préposerons à cet emploi,
4 Na sisi, tutaendelea daima katika kuomba na katika huduma ya neno.”
tandis que nous continuerons de vaquer à la prière et au ministère de la Parole.»
5 Hotuba yao ikaupendeza mkutano wote. Hivyo, wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena, na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
Cette proposition plut à toute l'assemblée, et l'on élut Etienne, homme plein de foi et d'Esprit saint, Philippe, Prochore, Nicanor, Timon, Parménas, et Nicolas, prosélyte d'Antioche;
6 Waumini waliwaleta watu hawa mbele ya mitume, walioomba na badaye wakawawekea mikono yao.
on les présenta aux apôtres, qui, après avoir prié, leur imposèrent les mains.
7 Hivyo, neno la Mungu lilienea; na idadi ya wanafunzi ilizidi kuongezeka huko Yesrusalem; na idadi kubwa ya makuhani wakaitii imani.
La parole de Dieu se répandait de plus en plus, et le nombre des disciples s'augmentait considérablement à Jérusalem: une multitude de sacrificateurs embrassaient la foi.
8 Na Stefano, aliyejaa neema na nguvu, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa miongoni mwa watu.
Etienne, plein de grâce et de force, faisait des prodiges et de grands miracles parmi le peuple.
9 Lakini hapo wakainuka baadhi ya watu wafuasi wa Sinagogi liitwalo Sinagogi la Mahuru, na la Wakirene na la Waeskanderia, na baadhi kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa walikuwa wakihojiana na Stefano.
Quelques Juifs de la synagogue dite des Affranchis, de celle des Cyrénéens et de celle des Alexandrins, ainsi que des Juifs venus de Cilicie et d'Asie étant entrés en dispute avec lui,
10 Lakini, hawakuweza kushindana na hekima na Roho ambayo Stefano alikuwa akitumia katika kuzungumza.
ne purent résister à la sagesse et à l'esprit avec lesquels il parlait.
11 Kisha waliwashawishi baadhi ya watu kwa siri kusema, “Tumesikia Stefano akizungumza maneno ya kufuru dhidi ya Musa na dhidi ya Mungu.”
Alors ils subornèrent des gens qui dirent: «Nous l'avons entendu tenir des propos blasphématoires contre Moïse et contre Dieu.»
12 Waliwashurutisha watu, wazee, na waandishi, na kumwendea Stefano, wakamkamata, na kumleta mbele ya baraza.
Ils ameutèrent le peuple, ainsi que les anciens et les scribes, puis, se jetant sur lui, ils l'entraînèrent et l'emmenèrent au sanhédrin.
13 waliwaleta mashahidi wa uongo, waliosema, “mtu huyu haachi kunena maneno mabaya dhidi ya eneo hili takatifu na sheria.
Ils produisirent de faux témoins qui dirent: «Cet homme ne cesse de tenir des propos contre le lieu saint et contre la Loi;
14 Kwani tumemsikia akisema kwamba huyu Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali hapa na kuzibadili desturi tulizokabidhiwa na Musa.”
nous l’avons entendu dire que Jésus, ce Nazaréen, détruira ce lieu, et changera les institutions que Moïse nous a données.»
15 Kila mmoja aliyekuwa katika baraza, akaelekeza macho yake kumwangalia Stefano, nao wakauona uso wake ulikuwa kama uso wa malaika.
Et comme tous les membres du sanhédrin avaient les yeux fixés sur lui, son vidage leur parut comme celui d'un ange.

< Matendo 6 >