< Matendo 6 >
1 Sasa katika siku hizi, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa inaongezeka, lalamiko la Wayahudi wa Kiyunani lilianza dhidi ya Waebrania, kwa sababu wajane wao walikuwa wanasahaulika katika mgao wa kila siku wa chakula.
In those dayes as the nombre of the disciples grewe ther arose a grudge amonge the Grekes agaynst the Ebrues be cause their wyddowes were despysed in the dayly mynystracion.
2 Mitume kumi na wawili waliwaita kusanyiko lote la wanafunzi na kusema, “Siyo sahihi kwetu kuliacha neno la Mungu na kuhudumia mezani.
Then the twelve called the multitude of the disciples to gether and sayde: it is not mete that we shuld leave the worde of God and serve at the tables.
3 Kwa hiyo, ndugu, chagueni, wanaume saba, kutoka miongoni mwenu, watu wema, waliojaa Roho na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi huduma hii.
Wherfore brethren loke ye out amoge you seven men of honest reporte and full of the holy goost and wysdome which we maye apoynte to this nedfull busynes.
4 Na sisi, tutaendelea daima katika kuomba na katika huduma ya neno.”
But we will geve oure selves cotinually to prayer and to the ministracion of ye worde.
5 Hotuba yao ikaupendeza mkutano wote. Hivyo, wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena, na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia.
And the sayinge pleased the whoale multitude. And they chose Steven a man full of fayth and of the holy goost and Philip and Prochorus and Nichanor and Timon and Permenas and Nicholas a converte of Antioche.
6 Waumini waliwaleta watu hawa mbele ya mitume, walioomba na badaye wakawawekea mikono yao.
Which they set before the Apostles and they prayed and layde their hondes on them.
7 Hivyo, neno la Mungu lilienea; na idadi ya wanafunzi ilizidi kuongezeka huko Yesrusalem; na idadi kubwa ya makuhani wakaitii imani.
And the worde of God encreased and the noubre of the disciples multiplied in Ierusalem greatly and a great company of the prestes were obedient to the faythe.
8 Na Stefano, aliyejaa neema na nguvu, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa miongoni mwa watu.
And Steven full of faythe and power dyd great wondres and myracles amoge ye people.
9 Lakini hapo wakainuka baadhi ya watu wafuasi wa Sinagogi liitwalo Sinagogi la Mahuru, na la Wakirene na la Waeskanderia, na baadhi kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa walikuwa wakihojiana na Stefano.
Then ther arose certayne of the synagoge which are called Lybertines and Syrenites and of Alexandria and of Cilicia and Asia and disputed with Steven.
10 Lakini, hawakuweza kushindana na hekima na Roho ambayo Stefano alikuwa akitumia katika kuzungumza.
And they coulde not resist the wysdome and the sprete with which he spake.
11 Kisha waliwashawishi baadhi ya watu kwa siri kusema, “Tumesikia Stefano akizungumza maneno ya kufuru dhidi ya Musa na dhidi ya Mungu.”
Then sent they in men which sayd: we have hearde him speake blasphemous wordes agaynst Moses and agaynst God.
12 Waliwashurutisha watu, wazee, na waandishi, na kumwendea Stefano, wakamkamata, na kumleta mbele ya baraza.
And they moved ye people and the elders and the scribes: and came apon him and caught him and brought him to the counsell
13 waliwaleta mashahidi wa uongo, waliosema, “mtu huyu haachi kunena maneno mabaya dhidi ya eneo hili takatifu na sheria.
and brought forth falce witnesses which sayde. This ma ceasith not to speake blasphemous wordes agaynst this holy place and the lawe:
14 Kwani tumemsikia akisema kwamba huyu Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali hapa na kuzibadili desturi tulizokabidhiwa na Musa.”
for we hearde him saye: this Iesus of Nazareth shall destroye this place and shall chaunge the ordinaunces which Moses gave vs.
15 Kila mmoja aliyekuwa katika baraza, akaelekeza macho yake kumwangalia Stefano, nao wakauona uso wake ulikuwa kama uso wa malaika.
And all that sate in ye counsell loked stedfastly on him and sawe his face as it had bene the face of an angell.