< Matendo 5 >
1 Hivyo, mtu mmoja aliyeitwa Anania, na Safira mkewe, waliuza sehemu ya mali,
But a man named Ananias who, with his wife Sapphira, sold a farm of his,
2 na akaficha sehemu ya fedha waliyouza (mke wake pia alilijua hili), na akaleta sehemu iliyobakia na kuiweka kwenye miguu ya mitume.
kept back some of the purchase price, with the connivance of his wife. He brought only a part and laid it at the apostles’ feet.
3 Lakini Petro akasema, “Anania, kwa nini shetani ameujaza moyo wako kusema uongo kwa Roho Mtakatifu na kuficha sehemu ya mali ya shamba?
"Ananias," said Peter, "why has Satan so filled your heart that you are lying to the Holy Spirit, and keeping back part of the price of the land?
4 Wakati lilipokuwa halijauzwa, halikuwa ni mali yako? Na baada ya kuuzwa, halikuwa chini ya uamuzi wako? Ilikuwaje uwaze jambo hili moyoni mwako? Hujawadanganya wanadamu, bali umemdanganya Mungu.”
"While it remained unsold, was it not your own? And after it was sold, was not the price at your own disposal? How could you conceive this act in your heart? You have not lied unto men, but unto God."
5 Katika kusikia maneno haya, Anania alidondoka chini na akakata roho. Na hofu kubwa iliwajia wote waliolisikia hili.
As Ananias heard these words he fell down and expired, and all who heard were awe-struck.
6 Vijana wakaja mbele na kumtia katika sanda, na kumpeleka nje na kumzika.
But the younger men rose, wrapped the body up, and carried it out to bury it.
7 Baada ya masaa matatu hivi, mke wake aliingia ndani, asijue ni nini kilichokuwa kimetokea.
About three hours later his wife came in, not knowing what had happened;
8 Petro akamwambia, “Niambie, kama mliuza shamba kwa thamani hiyo.” Akasema, “Ndiyo, kwa thamani hiyo.”
and Peter said to her, "Tell me if you got so much for the land." "Yes," she said, "so much."
9 Kisha Petro akamwambia, “Inakuwaje kwamba mmepatana kwa pamoja kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu ya wale waliomzika mme wako iko mlangoni, na watakubeba na kukupeleka nje.”
"Why was it," said Peter, "that you both agreed to tempt the Spirit of the Lord? Lo, the feet of those who buried your husband are at the door, and they shall carry you out."
10 Ghafla akadondoka miguuni pa Petro, akakata roho, na wale vijana wakaja ndani wakamkuta ameshakufa. Wakambeba kumpeleka nje, na kumzika karibu na mmewe.
Instantly she fell down at his feet and expired, and when the young men came in they found her dead, and carried her out and buried her husband.
11 Hofu kubwa ikaja juu ya kanisa zima, na juu ya wote walioyasikia mambo haya.
And great fear fell on all the church and upon all who had heard it.
12 Ishara nyingi na maajabu vilikuwa vinatokea miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume. Walikuwa pamoja katika ukumbi wa Sulemani.
Many signs and wonders continued to be wrought among the people by the hands of the apostles, and by common consent they all would meet in Solomon’s Porch,
13 Lakini, hakuna mtu mwingine tofauti aliyekuwa na ujasiri wa kuambatana nao; hata hivyo, walipewa heshima ya juu na watu.
but none of the rest dared to associate with them.
14 Na pia, waamini wengi walikuwa wakiongezeka kwa Bwana, idadi kubwa ya wanaume na wanawake,
Yet the people continued to hold them in high honor, and more and more believers in the Lord were joining them, both men and women.
15 kiasi kwamba hata waliwabeba wagonjwa mitaani, na kuwalaza vitandani na kwenye makochi, ili kwamba Petro akiwa anapita, kivuli chake kiweze kushuka juu yao.
In consequence people would even bring out their sick into the streets, and place them upon beds and pallets as Peter was passing, that at least his shadow might fall upon some of them.
16 Hapo pia, idadi kubwa ya watu walikuja kutoka miji iliyozunguka Yerusalem, wakiwaleta wagonjwa na wote waliopagawa na roho wachafu, na wote waliponywa.
The people of the towns near Jerusalem also continued to come in crowds, bringing their sick and those who were harried by unclean spirits, and all of them were healed.
17 Lakini kuhani mkuu aliinuka, na wote waliokuwa pamoja naye (ambao ni wa dhehebu la masadukayo); na walijawa na wivu
This aroused bitter indignation among the high priest and his followers who were of the sect of the Sadducees,
18 wakanyosha mikono yao kuwakamata mitume na kuwaweka ndani ya gereza la jumla.
and they apprehended the apostles, and threw them into the public prison.
19 Na wakati wa usiku malaika wa Bwana akaifungua milango ya gereza na kuwaongoza nje na kusema,
But an angel of the Lord opened the prison doors during the night, and let them out.
20 “Nendeni, mkasimame hekaluni na kuwaambia watu maneno yote ya Uzima huu.”
He said to them, "Go take your stand in the Temple, and continue to tell the people all the words of this Life."
21 Waliposikia hili, waliingia hekaluni wakati wa kupambazuka na kufundisha. Lakini, kuhani mkuu alikuja na wote waliokuwa naye, na kuitisha baraza lote kwa pamoja, na wazee wote wa watu wa Israeli, na kuwatuma gerezani ili kuwaleta mitume.
When they heard this they went at early dawn to the Temple, and began to teach. Meantime when the high priest and his followers arrived, they summoned the Sanhedrin and all the Council of the Elders of the sons of Israel, and sent to the prison to fetch the apostles.
22 Lakini watumishi waliokwenda, hawakuwakuta gerezani, walirudi na kutoa taarifa,
But the officers who went did not find them in the prison; so they came back and reported,
23 “Tumekuta gereza limefungwa vizuri salama, na walinzi wamesimama langoni, lakini tulipokuwa tukifungua, hatukuona mtu ndani.”
"The prison we found locked fast, with the guards stationed at the doors, but when they were opened we found no one inside."
24 Sasa wakati jemedari wa hekalu na makuhani wakuu waliposikia maneno haya, waliingiwa na shaka kubwa kwa ajili yao wakiwaza litakuwaje jambo hili.
When the officer in charge of the Temple and the high priest heard these words, they were perplexed concerning them, wondering what would come of it.
25 Kisha mmoja akaja na kuwaambia, “Watu mliowaweka gerezani wamesimama hekaluni na wanafundisha watu.”
And some one came and told them that the very men whom they had put in prison were standing in the Temple, and teaching to the people.
26 Hivyo jemedari alienda pamoja na watumishi, na wakawaleta, lakini bila ya kufanya vurugu, kwa sababu waliwaogopa watu wangeweza kuwapiga kwa mawe.
On this the officer went off with his men and fetched them, not, however, by force, for they were afraid that the people would stone them.
27 Walipokwisha kuwaleta, waliwaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu aliwahoji
So they brought them, and stood them before the Sanhedrin. Then the high priest questioned them.
28 akisema, “Tuliwaamuru msifundishe kwa jina hili, na bado mmeijaza Yerusalemu kwa fundisho lenu, na kutamani kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
"We strictly forbade you, did we not, to teach about this Name, and here you have filled Jerusalem with your teaching, and intend to bring this man’s blood upon us."
29 Lakini Petro na mitume wakajibu, “Lazima tumtii Mungu kuliko watu.
But Peter and the apostles said in reply.
30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, mliyemuua, kwa kumtundika juu ya mti.
"We must obey God rather than man. The God of our fathers has raised up Jesus, whom you slew by hanging him on a tree.
31 Mungu alimtukuza katika mkono wake wa kuume, na kumfanya kuwa Mkuu na mwokozi, kutoa toba kwa Israeli, na msamaha wa dhambi.
"Him God has exalted at his right hand as Prince and Saviour, to give Israel repentance and forgiveness of sins.
32 Sisi ni mashahidi wa mambo haya, na Roho Mtakatifu, ambaye Mungu amemtoa kwa wale wanaomtii.”
"And we are witnesses of these things, and so is the Holy Spirit whom God has given to those who obey him."
33 Wajumbe wa baraza waliposikia hivi, walishikwa na hasira wakataka kuwaua mitume.
When they heard this they were infuriated, and were minded to kill the apostles;
34 Lakini pharisayo aliyeitwa Gamalieli, mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, alisimama na kuwaamuru mitume wachukuliwe nje kwa muda mfupi.
but Gamaliel, a Pharisee, a teacher of the law, and held in honor by all the people, rose from his seat, and ordered the apostles to be put outside for a little while.
35 Kisha akawaambia, “Wanaume wa Israeli, iweni makini sana na kile mnachopendekeza kuwafanyia watu hawa.
He said. "Men of Israel, take care what you are about to do with these men.
36 Kwa sababu, zamani zilizopita, Theuda aliinuka na kujidai kuwa mtu mkuu, na idadi ya watu, wapata mia nne walimfuata. Aliuawa, na wote waliokuwa wanamtii walitawanyika na kupotea.
"Years ago Theudas arose, claiming to be somebody, and was joined by about four hundred men. He was killed, and all of his followers dispersed and annihilated.
37 Baada ya mtu huyu, Yuda mgalilaya, aliinuka siku zile za kuandikwa sensa, akavuta watu wengi nyuma yake. Naye pia alipotea na wote waliokuwa wakimtii walitawanyika.
"After him Judas of Galilee rose up in the days of the enrollment, and drew away some of the people after him. He also perished, and all his followers were scattered.
38 Sasa nawaambia, jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe, kwa sababu, kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa.
"And now, I say to you, hold aloof from these men. Let them alone; for if this scheme or work be of human origin it will come to nothing;
39 Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia; mnaweza mkajikuta hata mnashindana na Mungu.” Hivyo, walishawishika na maneno yake.
"but if it is from God, you cannot put it down; you may even find yourselves fighting against God."
40 Kisha, waliwaita mitume ndani na kuwachapa na kuwaamuru wasinene kwa jina la Yesu, na wakawaacha waende zao.
They gave in to him; and called the apostles in, and after flogging them, released them, with instructions not to speak about the name of Jesus.
41 Waliondoka mbele ya baraza wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuteseka na kutoheshimiwa kwa ajili ya Jina hilo.
So they left Sanhedrin, rejoicing that they had been deemed worthy to suffer disgrace for the sake of the Name;
42 Kwa hiyo, kila siku, ndani ya hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba waliendelea kufundisha na kuhubiri Yesu kuwa ni Masihi.
but not for a single day did they desist from teaching and preaching in the Temple, and in private houses, the Gospel of Jesus, the Messiah.