< Matendo 5 >

1 Hivyo, mtu mmoja aliyeitwa Anania, na Safira mkewe, waliuza sehemu ya mali,
But a certain man named Ananias, with Saphira his wife, sold a piece of land,
2 na akaficha sehemu ya fedha waliyouza (mke wake pia alilijua hili), na akaleta sehemu iliyobakia na kuiweka kwenye miguu ya mitume.
And by fraud kept back part of the price of the land, his wife being privy thereunto: and bringing a certain part of it, laid it at the feet of the apostles.
3 Lakini Petro akasema, “Anania, kwa nini shetani ameujaza moyo wako kusema uongo kwa Roho Mtakatifu na kuficha sehemu ya mali ya shamba?
But Peter said: Ananias, why hath Satan tempted thy heart, that thou shouldst lie to the Holy Ghost, and by fraud keep part of the price of the land?
4 Wakati lilipokuwa halijauzwa, halikuwa ni mali yako? Na baada ya kuuzwa, halikuwa chini ya uamuzi wako? Ilikuwaje uwaze jambo hili moyoni mwako? Hujawadanganya wanadamu, bali umemdanganya Mungu.”
Whilst it remained, did it not remain to thee? and after it was sold, was it not in thy power? Why hast thou conceived this thing in thy heart? Thou hast not lied to men, but to God.
5 Katika kusikia maneno haya, Anania alidondoka chini na akakata roho. Na hofu kubwa iliwajia wote waliolisikia hili.
And Ananias hearing these words, fell down, and gave up the ghost. And there came great fear upon all that heard it.
6 Vijana wakaja mbele na kumtia katika sanda, na kumpeleka nje na kumzika.
And the young men rising up, removed him, and carrying him out, buried him.
7 Baada ya masaa matatu hivi, mke wake aliingia ndani, asijue ni nini kilichokuwa kimetokea.
And it was about the space of three hours after, when his wife, not knowing what had happened, came in.
8 Petro akamwambia, “Niambie, kama mliuza shamba kwa thamani hiyo.” Akasema, “Ndiyo, kwa thamani hiyo.”
And Peter said to her: Tell me, woman, whether you sold the land for so much? And she said: Yea, for so much.
9 Kisha Petro akamwambia, “Inakuwaje kwamba mmepatana kwa pamoja kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu ya wale waliomzika mme wako iko mlangoni, na watakubeba na kukupeleka nje.”
And Peter said unto her: Why have you agreed together to tempt the Spirit of the Lord? Behold the feet of them who have buried thy husband are at the door, and they shall carry thee out.
10 Ghafla akadondoka miguuni pa Petro, akakata roho, na wale vijana wakaja ndani wakamkuta ameshakufa. Wakambeba kumpeleka nje, na kumzika karibu na mmewe.
Immediately she fell down before his feet, and gave up the ghost. And the young men coming in, found her dead: and carried her out, and buried her by her husband.
11 Hofu kubwa ikaja juu ya kanisa zima, na juu ya wote walioyasikia mambo haya.
And there came great fear upon the whole church, and upon all that heard these things.
12 Ishara nyingi na maajabu vilikuwa vinatokea miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume. Walikuwa pamoja katika ukumbi wa Sulemani.
And by the hands of the apostles were many signs and wonders wrought among the people. And they were all with one accord in Solomon’s porch.
13 Lakini, hakuna mtu mwingine tofauti aliyekuwa na ujasiri wa kuambatana nao; hata hivyo, walipewa heshima ya juu na watu.
But of the rest no man durst join himself unto them; but the people magnified them.
14 Na pia, waamini wengi walikuwa wakiongezeka kwa Bwana, idadi kubwa ya wanaume na wanawake,
And the multitude of men and women who believed in the Lord, was more increased:
15 kiasi kwamba hata waliwabeba wagonjwa mitaani, na kuwalaza vitandani na kwenye makochi, ili kwamba Petro akiwa anapita, kivuli chake kiweze kushuka juu yao.
Insomuch that they brought forth the sick into the streets, and laid them on beds and couches, that when Peter came, his shadow at the least, might overshadow any of them, and they might be delivered from their infirmities.
16 Hapo pia, idadi kubwa ya watu walikuja kutoka miji iliyozunguka Yerusalem, wakiwaleta wagonjwa na wote waliopagawa na roho wachafu, na wote waliponywa.
And there came also together to Jerusalem a multitude out of the neighboring cities, bringing sick persons, and such as were troubled with unclean spirits; who were all healed.
17 Lakini kuhani mkuu aliinuka, na wote waliokuwa pamoja naye (ambao ni wa dhehebu la masadukayo); na walijawa na wivu
Then the high priest rising up, and all they that were with him, (which is the heresy of the Sadducees, ) were filled with envy.
18 wakanyosha mikono yao kuwakamata mitume na kuwaweka ndani ya gereza la jumla.
And they laid hands on the apostles, and put them in the common prison.
19 Na wakati wa usiku malaika wa Bwana akaifungua milango ya gereza na kuwaongoza nje na kusema,
But an angel of the Lord by night opening the doors of the prison, and leading them out, said:
20 “Nendeni, mkasimame hekaluni na kuwaambia watu maneno yote ya Uzima huu.”
Go, and standing speak in the temple to the people all the words of this life.
21 Waliposikia hili, waliingia hekaluni wakati wa kupambazuka na kufundisha. Lakini, kuhani mkuu alikuja na wote waliokuwa naye, na kuitisha baraza lote kwa pamoja, na wazee wote wa watu wa Israeli, na kuwatuma gerezani ili kuwaleta mitume.
Who having heard this, early in the morning, entered into the temple, and taught. And the high priest coming, and they that were with him, called together the council, and all the ancients of the children of Israel; and they sent to the prison to have them brought.
22 Lakini watumishi waliokwenda, hawakuwakuta gerezani, walirudi na kutoa taarifa,
But when the ministers came, and opening the prison, found them not there, they returned and told,
23 “Tumekuta gereza limefungwa vizuri salama, na walinzi wamesimama langoni, lakini tulipokuwa tukifungua, hatukuona mtu ndani.”
Saying: The prison indeed we found shut with all diligence, and the keepers standing before the doors; but opening it, we found no man within.
24 Sasa wakati jemedari wa hekalu na makuhani wakuu waliposikia maneno haya, waliingiwa na shaka kubwa kwa ajili yao wakiwaza litakuwaje jambo hili.
Now when the officer of the temple and the chief priests heard these words, they were in doubt concerning them, what would come to pass.
25 Kisha mmoja akaja na kuwaambia, “Watu mliowaweka gerezani wamesimama hekaluni na wanafundisha watu.”
But one came and told them: Behold, the men whom you put in prison are in the temple standing, and teaching the people.
26 Hivyo jemedari alienda pamoja na watumishi, na wakawaleta, lakini bila ya kufanya vurugu, kwa sababu waliwaogopa watu wangeweza kuwapiga kwa mawe.
Then went the officer with the ministers, and brought them without violence; for they feared the people, lest they should be stoned.
27 Walipokwisha kuwaleta, waliwaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu aliwahoji
And when they had brought them, they set them before the council. And the high priest asked them,
28 akisema, “Tuliwaamuru msifundishe kwa jina hili, na bado mmeijaza Yerusalemu kwa fundisho lenu, na kutamani kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
Saying: Commanding we commanded you, that you should not teach in this name; and behold, you have filled Jerusalem with your doctrine, and you have a mind to bring the blood of this man upon us.
29 Lakini Petro na mitume wakajibu, “Lazima tumtii Mungu kuliko watu.
But Peter and the apostles answering, said: We ought to obey God, rather than men.
30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, mliyemuua, kwa kumtundika juu ya mti.
The God of our fathers hath raised up Jesus, whom you put to death, hanging him upon a tree.
31 Mungu alimtukuza katika mkono wake wa kuume, na kumfanya kuwa Mkuu na mwokozi, kutoa toba kwa Israeli, na msamaha wa dhambi.
Him hath God exalted with his right hand, to be Prince and Saviour, to give repentance to Israel, and remission of sins.
32 Sisi ni mashahidi wa mambo haya, na Roho Mtakatifu, ambaye Mungu amemtoa kwa wale wanaomtii.”
And we are witnesses of these things and the Holy Ghost, whom God hath given to all that obey him.
33 Wajumbe wa baraza waliposikia hivi, walishikwa na hasira wakataka kuwaua mitume.
When they had heard these things, they were cut to the heart, and they thought to put them to death.
34 Lakini pharisayo aliyeitwa Gamalieli, mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, alisimama na kuwaamuru mitume wachukuliwe nje kwa muda mfupi.
But one in the council rising up, a Pharisee, named Gamaliel, a doctor of the law, respected by all the people, commanded the men to be put forth a little while.
35 Kisha akawaambia, “Wanaume wa Israeli, iweni makini sana na kile mnachopendekeza kuwafanyia watu hawa.
And he said to them: Ye men of Israel, take heed to yourselves what you intend to do, as touching these men.
36 Kwa sababu, zamani zilizopita, Theuda aliinuka na kujidai kuwa mtu mkuu, na idadi ya watu, wapata mia nne walimfuata. Aliuawa, na wote waliokuwa wanamtii walitawanyika na kupotea.
For before these days rose up Theodas, affirming himself to be somebody, to whom a number of men, about four hundred, joined themselves: who was slain; and all that believed him were scattered, and brought to nothing.
37 Baada ya mtu huyu, Yuda mgalilaya, aliinuka siku zile za kuandikwa sensa, akavuta watu wengi nyuma yake. Naye pia alipotea na wote waliokuwa wakimtii walitawanyika.
After this man, rose up Judas of Galilee, in the days of the enrolling, and drew away the people after him: he also perished; and all, even as many as consented to him, were dispersed.
38 Sasa nawaambia, jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe, kwa sababu, kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa.
And now, therefore, I say to you, refrain from these men, and let them alone; for if this council or this work be of men, it will come to nought;
39 Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia; mnaweza mkajikuta hata mnashindana na Mungu.” Hivyo, walishawishika na maneno yake.
But if it be of God, you cannot overthrow it, lest perhaps you be found even to fight against God. And they consented to him.
40 Kisha, waliwaita mitume ndani na kuwachapa na kuwaamuru wasinene kwa jina la Yesu, na wakawaacha waende zao.
And calling in the apostles, after they had scourged them, they charged them that they should not speak at all in the name of Jesus; and they dismissed them.
41 Waliondoka mbele ya baraza wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuteseka na kutoheshimiwa kwa ajili ya Jina hilo.
And they indeed went from the presence of the council, rejoicing that they were accounted worthy to suffer reproach for the name of Jesus.
42 Kwa hiyo, kila siku, ndani ya hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba waliendelea kufundisha na kuhubiri Yesu kuwa ni Masihi.
And every day they ceased not in the temple, and from house to house, to teach and preach Christ Jesus.

< Matendo 5 >