< Matendo 5 >
1 Hivyo, mtu mmoja aliyeitwa Anania, na Safira mkewe, waliuza sehemu ya mali,
But a certain man named Ananias, with Sapphira his wife, sold property,
2 na akaficha sehemu ya fedha waliyouza (mke wake pia alilijua hili), na akaleta sehemu iliyobakia na kuiweka kwenye miguu ya mitume.
and kept back from the price, his wife also having joint awareness. And having brought a certain part, he placed it at the apostles' feet.
3 Lakini Petro akasema, “Anania, kwa nini shetani ameujaza moyo wako kusema uongo kwa Roho Mtakatifu na kuficha sehemu ya mali ya shamba?
But Peter said, Ananias, why did Satan fill thy heart for thee to lie to the Holy Spirit, and to keep back from the price of the land?
4 Wakati lilipokuwa halijauzwa, halikuwa ni mali yako? Na baada ya kuuzwa, halikuwa chini ya uamuzi wako? Ilikuwaje uwaze jambo hili moyoni mwako? Hujawadanganya wanadamu, bali umemdanganya Mungu.”
While it remained, did it not remain to thee? And after it was sold, it was in thine authority. Why is it that thou have placed this matter in thy heart? Thou have not lied to men, but to God.
5 Katika kusikia maneno haya, Anania alidondoka chini na akakata roho. Na hofu kubwa iliwajia wote waliolisikia hili.
And Ananias hearing these words, after falling down he expired. And great fear developed in all who heard these things.
6 Vijana wakaja mbele na kumtia katika sanda, na kumpeleka nje na kumzika.
And after rising the young men wrapped him, and having carried him out they buried him.
7 Baada ya masaa matatu hivi, mke wake aliingia ndani, asijue ni nini kilichokuwa kimetokea.
And it came to pass after an interval of three hours, his wife also came in, not knowing that which happened.
8 Petro akamwambia, “Niambie, kama mliuza shamba kwa thamani hiyo.” Akasema, “Ndiyo, kwa thamani hiyo.”
And Peter responded to her, Tell me whether ye sold the land for so much. And she said, Yes, for so much.
9 Kisha Petro akamwambia, “Inakuwaje kwamba mmepatana kwa pamoja kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu ya wale waliomzika mme wako iko mlangoni, na watakubeba na kukupeleka nje.”
But Peter said to her, How is it that it was agreed by you to challenge the Spirit of the Lord? Behold, the feet of those who buried thy husband are at the door, and they will carry thee out.
10 Ghafla akadondoka miguuni pa Petro, akakata roho, na wale vijana wakaja ndani wakamkuta ameshakufa. Wakambeba kumpeleka nje, na kumzika karibu na mmewe.
And immediately she fell down at his feet and expired. And after coming in the young men found her dead, and having carried her out, they buried her by her husband.
11 Hofu kubwa ikaja juu ya kanisa zima, na juu ya wote walioyasikia mambo haya.
And great fear developed in the whole church, and in all who heard these things.
12 Ishara nyingi na maajabu vilikuwa vinatokea miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume. Walikuwa pamoja katika ukumbi wa Sulemani.
And by the hands of the apostles many signs and wonders happened among the people. And they were all with one accord in Solomon's porch.
13 Lakini, hakuna mtu mwingine tofauti aliyekuwa na ujasiri wa kuambatana nao; hata hivyo, walipewa heshima ya juu na watu.
But of the rest no man dared join them, but the people magnified them.
14 Na pia, waamini wengi walikuwa wakiongezeka kwa Bwana, idadi kubwa ya wanaume na wanawake,
And more who believe were added to the Lord, multitudes both of men and women,
15 kiasi kwamba hata waliwabeba wagonjwa mitaani, na kuwalaza vitandani na kwenye makochi, ili kwamba Petro akiwa anapita, kivuli chake kiweze kushuka juu yao.
so as to bring the feeble to the thoroughfares, and to place them on cots and mats, so that while coming, the shadow of Peter might at the least overshadow some of them.
16 Hapo pia, idadi kubwa ya watu walikuja kutoka miji iliyozunguka Yerusalem, wakiwaleta wagonjwa na wote waliopagawa na roho wachafu, na wote waliponywa.
And also the populace of the cities round about came together to Jerusalem bringing the feeble, and those tormented by unclean spirits, who were all healed.
17 Lakini kuhani mkuu aliinuka, na wote waliokuwa pamoja naye (ambao ni wa dhehebu la masadukayo); na walijawa na wivu
But after rising up, the high priest and all those with him (being the sect of the Sadducees) were filled of envy.
18 wakanyosha mikono yao kuwakamata mitume na kuwaweka ndani ya gereza la jumla.
And they threw their hands on the apostles, and put them in the public prison.
19 Na wakati wa usiku malaika wa Bwana akaifungua milango ya gereza na kuwaongoza nje na kusema,
But an agent of the Lord opened the prison doors by night, and after leading them out, he said,
20 “Nendeni, mkasimame hekaluni na kuwaambia watu maneno yote ya Uzima huu.”
Go ye, and after standing in the temple, speak to the people all the sayings of this Life.
21 Waliposikia hili, waliingia hekaluni wakati wa kupambazuka na kufundisha. Lakini, kuhani mkuu alikuja na wote waliokuwa naye, na kuitisha baraza lote kwa pamoja, na wazee wote wa watu wa Israeli, na kuwatuma gerezani ili kuwaleta mitume.
And having heard, they entered into the temple at early morning, and taught. But the high priest having arrived, and those with him, they called the council together, and all the senate of the sons of Israel. And they sent to the prison for them to be brought.
22 Lakini watumishi waliokwenda, hawakuwakuta gerezani, walirudi na kutoa taarifa,
But the subordinates who came did not find them in the prison. And having returned, they reported,
23 “Tumekuta gereza limefungwa vizuri salama, na walinzi wamesimama langoni, lakini tulipokuwa tukifungua, hatukuona mtu ndani.”
saying, We found the prison indeed shut in all security, and the guards standing before the doors, but after opening, we found no man inside.
24 Sasa wakati jemedari wa hekalu na makuhani wakuu waliposikia maneno haya, waliingiwa na shaka kubwa kwa ajili yao wakiwaza litakuwaje jambo hili.
Now when they heard these words, the high priest, and the captain of the temple, and the chief priests, were perplexed about them, whatever this would become.
25 Kisha mmoja akaja na kuwaambia, “Watu mliowaweka gerezani wamesimama hekaluni na wanafundisha watu.”
But a certain man who arrived, reported to them, Behold, the men whom ye put in the prison are standing in the temple and teaching the people.
26 Hivyo jemedari alienda pamoja na watumishi, na wakawaleta, lakini bila ya kufanya vurugu, kwa sababu waliwaogopa watu wangeweza kuwapiga kwa mawe.
Then after departing, the captain with the subordinates brought them, not with violence, for they feared the people, lest they would be stoned.
27 Walipokwisha kuwaleta, waliwaweka mbele ya baraza. Kuhani mkuu aliwahoji
And having brought them, they placed them in the council. And the high priest demanded them,
28 akisema, “Tuliwaamuru msifundishe kwa jina hili, na bado mmeijaza Yerusalemu kwa fundisho lenu, na kutamani kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.”
saying, Did we not command by an order for you not to teach in this name? And behold, ye have filled Jerusalem of your doctrine, and intend to bring upon us this man's blood.
29 Lakini Petro na mitume wakajibu, “Lazima tumtii Mungu kuliko watu.
And Peter and the apostles having answered, they said, We must obey God rather than men.
30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, mliyemuua, kwa kumtundika juu ya mti.
The God of our fathers raised up Jesus, whom ye murdered, having hung on a tree.
31 Mungu alimtukuza katika mkono wake wa kuume, na kumfanya kuwa Mkuu na mwokozi, kutoa toba kwa Israeli, na msamaha wa dhambi.
God exalted this man with his right hand, a Pathfinder and a Savior to give repentance to Israel and remission of sins.
32 Sisi ni mashahidi wa mambo haya, na Roho Mtakatifu, ambaye Mungu amemtoa kwa wale wanaomtii.”
And we are his witnesses of these things, and also the Holy Spirit whom God has given to those who obey him.
33 Wajumbe wa baraza waliposikia hivi, walishikwa na hasira wakataka kuwaua mitume.
And when they heard this, they were as being split with a saw, and wanted to annihilate them.
34 Lakini pharisayo aliyeitwa Gamalieli, mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote, alisimama na kuwaamuru mitume wachukuliwe nje kwa muda mfupi.
But after standing up in the council, a certain Pharisee named Gamaliel, a law teacher, esteemed by all the people, commanded to make the apostles be outside a little while.
35 Kisha akawaambia, “Wanaume wa Israeli, iweni makini sana na kile mnachopendekeza kuwafanyia watu hawa.
And he said to them, Men, Israelites, take heed to yourselves what ye are going to do against these men.
36 Kwa sababu, zamani zilizopita, Theuda aliinuka na kujidai kuwa mtu mkuu, na idadi ya watu, wapata mia nne walimfuata. Aliuawa, na wote waliokuwa wanamtii walitawanyika na kupotea.
For before these days Theudas rose up saying himself to be somebody, to whom a number of men, about four hundred, bonded themselves, who was killed. And all, as many as were persuaded by him, were dispersed and developed into nothing.
37 Baada ya mtu huyu, Yuda mgalilaya, aliinuka siku zile za kuandikwa sensa, akavuta watu wengi nyuma yake. Naye pia alipotea na wote waliokuwa wakimtii walitawanyika.
After this man Judas the Galilean rose up in the days of the registration, and drew a considerable crowd behind him. That man was also destroyed, and all, as many as were persuaded by him, were scattered.
38 Sasa nawaambia, jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe, kwa sababu, kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa.
And now I say to you, keep away from these men, and let them go, because if the project or this work is from men, it will be overthrown,
39 Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia; mnaweza mkajikuta hata mnashindana na Mungu.” Hivyo, walishawishika na maneno yake.
but if it is from God, ye cannot overthrow it, and perhaps ye may be found to be fighting against God.
40 Kisha, waliwaita mitume ndani na kuwachapa na kuwaamuru wasinene kwa jina la Yesu, na wakawaacha waende zao.
And they were persuaded by him. And after summoning the apostles, having beat them, they commanded them not to speak in the name of Jesus, and released them.
41 Waliondoka mbele ya baraza wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuteseka na kutoheshimiwa kwa ajili ya Jina hilo.
Indeed therefore they departed from the presence of the council, rejoicing that they were considered worthy to be treated shamefully for the name of Jesus.
42 Kwa hiyo, kila siku, ndani ya hekalu na kutoka nyumba hadi nyumba waliendelea kufundisha na kuhubiri Yesu kuwa ni Masihi.
And every day, in the temple and from house to house, they ceased not teaching and preaching good news, Jesus, the Christ.