< Matendo 4 >
1 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
While they were addressing the people the priests, the commander of the Temple, and the Sadducees came upon them,
2 Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
incensed at their teaching the people, and proclaiming, in the case of Jesus, the resurrection from the dead.
3 Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
They arrested them, and put them in prison till the next day, for it was already evening.
4 Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
But many of those who had heard the message believed, and the number of the men came to be about five thousand.
5 Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
There was held in Jerusalem, next morning, a meeting of their rulers, the elders and scribes,
6 Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
and Annas, the high priest, Caiaphas, John, Alexander, and all the members of the high priests family were present.
7 Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
Then they made the men stand before them and demanded, "By what power, or in what name, have you fellows done this?"
8 Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
Then Peter, filled with the Holy Spirit, answered them.
9 kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
"Rulers and elders of the people, if we are being examined today concerning a benefit conferred upon a cripple, as to how has this man been cured,
10 Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
"be it known to all of you, and to all the people of Israel, that in the name of Jesus Christ, the Nazarene, whom you crucified, whom God raised from the dead, in him does this man stand before you strong and well.
11 Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
"For he is the Stone, cast aside by you builders, which has become the head stone of the corner.
12 Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
"There is no salvation in any other, for there is no other name under heaven given among men, in which we must be saved."
13 Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
Now when they beheld the glad fearlessness of Peter and John and had perceived that they were amazed; and they began to recognize them, that they were companions of Jesus.
14 Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
But since they saw the man standing with them who had been healed, they had nothing to answer.
15 Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
So they bade them withdraw from the Sanhedrin, while they conferred together.
16 Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
"What," said they, "shall we do with these men? For it is well known throughout Jerusalem that a notable miracle has been performed by them, and we cannot deny it.
17 Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
"But that the matter may spread no further among the people, let us threaten them not to speak to any one hereafter about this name."
18 Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
So they summoned them, and ordered them not to speak at all, nor to teach in the name of Jesus.
19 Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
But Peter and John said in reply. "Do you decide whether in the sight of God it is right to obey you rather than God;
20 Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
but for our part, we cannot help speaking about what we have seen and heard."
21 Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
So when they had further threatened them they let the apostles go, being quite unable to find any way of punishing them because of the people, for everybody was glorifying God over what had happened.
22 Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
For the man on whom this miracle of healing had been wrought was over forty years old.
23 Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
As soon as the apostles were released, they went to their friends, and told what the high priests and elders had said.
24 Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
And when they heard it they all lifted up their voices in prayer to God, saying. "O Sovereign Lord, who madest heaven and earth and sea, and all that in them is,
25 wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
"who saidest through the Holy Spirit, by the lips of thy servant David, our forefather. "Why did the Gentiles rage, And the peoples form futile plans?
26 Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
"The kings of the earth set themselves in array, And the rulers were gathered together Against the Lord and against his Christ.
27 Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
"In this very city they did gather together against thy holy Servant, Jesus whom thou hast anointed - Herod and Pontius Pilate, with the Gentiles and also the tribes of Israel -
28 Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
"to do all that thy power and thy will had predetermined should be done.
29 Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
"And now Lord, listen to their threats, and grant to thy slaves to proclaim thy message with all boldness,
30 kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
"whilst thou stretchest forth thy hand to heal; grant too, that signs and wonders may be done through the name of thy holy Servant, Jesus."
31 Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
When they had prayed, the place where they were gathered was shaken; and they were all filled with the Holy Spirit, and began to speak the message of the Lord with boldness.
32 Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
Now the multitude of the believers was of one heart and one soul, nor did any one of them say that any of his possessions was his own; but they had all things common.
33 Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
And the apostles continued with great power to give their witness concerning the resurrection of the Lord Jesus, and great grace was upon them all.
34 Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
Nor was there any one of them in want, for all who owned houses or lands would sell them and bring the price of the things that were sold, and lay it at the apostles’ feet;
35 na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
and distribution would be made to each according to his need.
36 Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
In this way Joseph, whom the apostles called Barnabas ("Son of Encouragement" is what it means), who was a native Cyprus,
37 Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.
sold a farm which he had, and brought the price, and laid it at the apostles’ feet.