< Matendo 4 >

1 Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
While they were speaking to the people, the priests, and the captain of the temple, and the Sadducees came upon them,
2 Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
being vexed because they taught the people, and preached through Jesus the resurrection from the dead.
3 Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
And they laid hands on them, and put them in prison till the next day, for it was already evening.
4 Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
But many of those who heard the word, believed: and the number of the men was about five thousand.
5 Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
And it came to pass, on the next day, that their rulers and elders and scribes,
6 Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
and Annas the chief priest, and Caiaphas and John and Alexander, and as many as were of the family of the chief priest, met together in Jerusalem.
7 Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
And when they had made them stand in the midst, they asked: By what power, or by what name have you done this?
8 Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
Then Peter, filled with the Holy Spirit, said to them: Rulers of the people, and elders of Israel,
9 kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
if we are this day examined with respect unto the good deed done to the infirm man, by what means he has been saved,
10 Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
be it known to you all, and to all the people of Israel, that by the name of Jesus Christ the Nazarene, whom you crucified, whom God raised from the dead, by him does this man stand before you in health.
11 Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
This is the stone that was rejected with contempt by you builders, which has become the head of the corner.
12 Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
And there is salvation in no other; nor, indeed, is there another name under heaven, given among men, by which we must be saved.
13 Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
Now, when they saw the boldness of Peter and John, and perceived that they were unlearned and plain men, they were astonished; and they also recognized them, that they had been with Jesus;
14 Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
and, seeing the man who had been cured standing with them, they had nothing to say in reply.
15 Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
But, having commanded them to go aside out of the Sanhedrim, they consulted with one another,
16 Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
saying: What shall we do with these men? For that an evident sign has been done by them, is manifest to all that dwell in Jerusalem, and we can not deny it.
17 Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
But that it may spread no further among the people, let us severely threaten them, so that they speak no more to any man in this name.
18 Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
And they called them in, and commanded them to speak no more at all, nor to teach, in the name of Jesus.
19 Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
But Peter and John answering them, said: Whether it is right in the sight of God to obey you rather than God, judge you.
20 Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
For we can not but speak the things that we have seen and heard.
21 Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
And when they had further threatened them, they let them go, finding nothing for which they could punish them, because of the people; for they all glorified God on account of that which had been done;
22 Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
for the man on whom this sign of healing had been performed was more than forty years old.
23 Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
And having been released, they went to their own, and told all that the chief priests and elders had said to them.
24 Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
And when they heard it, they lifted up their voice with one consent to God, and said: Lord, thou art God, who didst make the heaven and the earth and the sea, and all things that are in them; who, by the mouth of David thy servant, didst say,
25 wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
Why did the heathen rage, and the people devise vain things?
26 Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
The kings of the land stood up, and the rulers met together against the Lord and against his anointed.
27 Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
For, in truth, against thy holy child Jesus, whom thou didst anoint, both Herod and Pontius Pilate, with the Gentiles and the people of Israel, did meet together,
28 Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
to do whatever thy hand and thy counsel determined to be done.
29 Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
And now, Lord, look upon their threatenings, and grant to thy servants that they may speak thy word with all boldness,
30 kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
by stretching out thy hand to heal, that both signs and wonders may be done through the name of thy holy child Jesus.
31 Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
And when they had prayed, the place in which they were assembled was shaken; and they were all filled with the Holy Spirit, and spoke the word of God with boldness.
32 Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
And the multitude of believers were of one heart and of one soul; and no one said that any part of his possessions was his own; but they had all things in common.
33 Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
And with great power did the apostles bear testimony to the resurrection of the Lord Jesus, and great grace was on them all.
34 Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
Nor, indeed, was there any needy person among them; for as many as were owners of lands or houses, sold them, and brought the prices of what had been sold,
35 na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
and laid them down at the feet of the apostles; and distribution was made to every one as he had need.
36 Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
And Joses, who, by the apostles, was surnamed Barnabas, (which name, when translated, is, Son of consolation, ) a Levite, by birth a Cyprian,
37 Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.
having land, sold it, and brought the money and laid it at the feet of the apostles.

< Matendo 4 >