< Matendo 3 >

1 Sasa Peter na Yohana walikuwa wanaelekea katika hekalu wakati wa maombi, saa tisa.
One day Peter and John were going up together to the temple at the hour of prayer, the ninth hour.
2 Mtu fulani, kiwete tangu kuzaliwa, alikuwa akibebwa kila siku na alikuwa akilazwa katika mlango wa hekalu uitwao mzuri, ili aweze kuomba sadaka kutoka kwa watu waliokuwa wakielekea hekaluni.
And a man who was lame from his mother's womb was being carried in. Every day people would lay him at the gate of the temple called the Beautiful Gate so that he could ask for alms from those who were entering the temple courts.
3 Alipowaona Petro na Yohana wanakaribia kuingia hekaluni, aliomba sadaka.
When he saw Peter and John about to enter the temple courts, he began asking for alms.
4 Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, alisema,”tutazame sisi.”
But Peter, along with John, looked at him intently and said, “Look at us.”
5 Kiwete akawatazama, akitazamia kupokea kitu fulani kutoka kwao.
So the man gave them his attention, expecting to receive something from them.
6 Lakini Petro akasema, “fedha na dhahabu mimi sina, lakini kile nilichonacho nitatoa kwako. Katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth, tembea.”
But Peter said, “I have no silver or gold, but what I do have I give to yoʋ. In the name of Jesus Christ of Nazareth, rise up and walk.”
7 Petro akamchukua kwa mkono wake wa kulia, na akamwinua juu: mara moja miguu yake na vifundo vya mifupa yake vikapata nguvu.
Then Peter took hold of him by the right hand and raised him up, and at once his feet and ankles were made strong.
8 Akiruka juu, mtu kiwete alisimama na akaanza kutembea; akaingia hekaluni pamoja na Petro na Yohana, akitembea, akiruka, na kumsifu Mungu.
Leaping up, he stood and began walking. Then he entered the temple courts with them, walking and leaping and praising God.
9 Watu wote walimwona akitembea na akimsifu Mungu.
When all the people saw him walking and praising God,
10 Wakatambua kwamba alikuwa ni yule mtu ambaye alikuwa akikaa akiomba sadaka kwenye mlango mzuri wa hekalu; walijawa na mshangao na kustaajabu kwa sababu ya kile kilichotokea kwake.
they recognized him as the man who used to sit at the Beautiful Gate of the temple asking for alms. And they were filled with wonder and amazement at what had happened to him.
11 Namna alivyokuwa amewashikilia Petro na Yohana, watu wote kwa pamoja wakakimbilia kwenye ukumbi uitwao wa Sulemani, wakishangaa sana.
As the lame man who had been healed clung to Peter and John, all the people ran together to them at the portico called Solomon's, utterly astonished.
12 Petro alipoliona hili, yeye akawajibu watu, “Enyi watu wa Israel, kwa nini mnashangaa? Kwa nini mnayaelekeza macho yenu kwetu, kama kwamba tumemfanya huyu atembee kwa nguvu zetu wenyewe au uchaji wetu?”
When Peter saw this, he addressed the people: “Men of Israel, why are you amazed at this, or why are you staring at us as though by our own power or godliness we have made this man walk?
13 Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Yakobo, Mungu wa Baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu. Huyu ndiye ambaye ninyi mlimkabidhi na kumkataa mbele ya uso wa Pilato, japo yeye alikuwa ameamua kumwachia huru.
The God of Abraham, Isaac, and Jacob—the God of our fathers—has glorified his servant Jesus, whom you delivered up and denied in the presence of Pilate, even though Pilate had decided to release him.
14 Mlimkataa Mtakatifu na Mwenye Haki, na badala yake mkataka muuaji aachwe huru.
Yes, you denied the Holy and Righteous One and asked for a murderer to be granted to you.
15 Ninyi mlimuua Mfalme wa uzima, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu - Sisi ni mashahidi wa hili.
You put to death the Author of life, whom God raised from the dead, of which we are witnesses.
16 Sasa, kwa imani katika jina lake, mtu huyu ambaye mnamwona na kujua, alifanywa kuwa na nguvu. Imani ambayo inapitia kwa Yesu imempa yeye afya hii kamilifu, mbele yenu ninyi nyote.
By faith in his name, his name has given strength to this man whom you see and know, and the faith that is through Jesus has given him this perfect health in the presence of you all.
17 Sasa, Ndugu, najua kwamba mlitenda katika ujinga, ndivyo pia walivyofanya viongozi wenu.
“Now, brothers, I know that you acted in ignorance, as did your rulers also.
18 Lakini mambo ambayo Mungu aliwaambia mapema kwa vinywa vya manabii wote, kwamba huyu Kristo atateseka, sasa ameyatimiza.
But in this way God fulfilled what he had foretold through the mouths of all his prophets, that the Christ would suffer.
19 Kwa hiyo, tubuni na mgeuke, ili kwamba dhambi zenu ziweze kuondolewa kabisa, kusudi zije nyakati za kuburudika kutokana na uwepo wa Bwana;
Therefore repent and turn back so that your sins may be wiped away, that times of refreshing may come from the presence of the Lord,
20 na kwamba aweze kumtuma Kristo ambaye ameshateuliwa kwa ajili yenu, Yesu.
and that he may send Jesus, the Christ who has been appointed for you.
21 Yeye ndiye ambaye lazima mbingu zimpokee mpaka wakati wa kurejeshwa kwa vitu vyote, ambavyo Mungu alizungumzia zamani za kale kwa vinywa vya manabii watakatifu. (aiōn g165)
Heaven must receive him until the time comes for the restoration of all things, which God declared by the mouths of all his holy prophets long ago. (aiōn g165)
22 Hakika Musa alisema, 'Bwana Mungu atainua nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu. Mtamsikiliza kila kitu ambacho atawaambia ninyi.
For Moses said to our fathers, ‘The Lord our God will raise up for you a prophet like me from among your brothers. You must listen to everything he tells you.
23 Itatokea kwamba kila mtu ambaye hasikilizi kwa nabii huyo ataangamizwa kabisa atoke kati ya watu.'
Every soul who does not listen to that prophet will be utterly destroyed from among the people.’
24 Ndiyo, na manabii wote tokea Samweli na wale waliofuata baada yake, walizungumza na walitangaza siku hizi.
Indeed, all the prophets who have spoken, beginning with Samuel and continuing with those who came afterward, also proclaimed these days.
25 Ninyi ni wana wa manabii na wa agano ambalo Mungu alilifanya pamoja na mababu, kama alivyosema kwa Abrahamu, 'Katika mbegu yako familia zote za dunia zitabarikiwa.'
You are the sons of the prophets and of the covenant that God made with our fathers when he said to Abraham, ‘In yoʋr offspring all the families of the earth will be blessed.’
26 Baada ya Mungu kumwinua mtumishi wake, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki ninyi kwa kugeuka kutoka katika uovu wenu.”
God raised up his servant Jesus and sent him first to you, to bless you by turning each of you from your evil ways.”

< Matendo 3 >