< Matendo 3 >

1 Sasa Peter na Yohana walikuwa wanaelekea katika hekalu wakati wa maombi, saa tisa.
Now Peter and John were going up together into the temple at the hour of prayer, which was the ninth hour.
2 Mtu fulani, kiwete tangu kuzaliwa, alikuwa akibebwa kila siku na alikuwa akilazwa katika mlango wa hekalu uitwao mzuri, ili aweze kuomba sadaka kutoka kwa watu waliokuwa wakielekea hekaluni.
And a certain man, lame from his mother’s womb, was carried along, whom they laid daily at that gate of the temple which is called Beautiful, that he might ask charity of those who were going into the temple.
3 Alipowaona Petro na Yohana wanakaribia kuingia hekaluni, aliomba sadaka.
This man, seeing Peter and John about to go into the temple, asked charity.
4 Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, alisema,”tutazame sisi.”
But Peter, fixing his eyes on him with John, said: Look on us.
5 Kiwete akawatazama, akitazamia kupokea kitu fulani kutoka kwao.
And he gave heed to them, expecting to receive something from them.
6 Lakini Petro akasema, “fedha na dhahabu mimi sina, lakini kile nilichonacho nitatoa kwako. Katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth, tembea.”
But Peter said: Silver and gold I have none: but what I have, this I give you. In the name of Jesus Christ the Nazarene, arise and walk.
7 Petro akamchukua kwa mkono wake wa kulia, na akamwinua juu: mara moja miguu yake na vifundo vya mifupa yake vikapata nguvu.
And he took him by his right hand and raised him up: and immediately his feet and ankles received strength.
8 Akiruka juu, mtu kiwete alisimama na akaanza kutembea; akaingia hekaluni pamoja na Petro na Yohana, akitembea, akiruka, na kumsifu Mungu.
And leaping up, he stood and walked, and went with them into the temple, walking and leaping and praising God.
9 Watu wote walimwona akitembea na akimsifu Mungu.
And all the people saw him walking and praising God;
10 Wakatambua kwamba alikuwa ni yule mtu ambaye alikuwa akikaa akiomba sadaka kwenye mlango mzuri wa hekalu; walijawa na mshangao na kustaajabu kwa sababu ya kile kilichotokea kwake.
and they recognized him, that it was he that had sat for charity at the Beautiful gate of the temple. And they were filled with wonder and amazement at what had happened to him.
11 Namna alivyokuwa amewashikilia Petro na Yohana, watu wote kwa pamoja wakakimbilia kwenye ukumbi uitwao wa Sulemani, wakishangaa sana.
And while he was holding to Peter and John, all the people ran together to them in the porch called Solomon’s, greatly astonished.
12 Petro alipoliona hili, yeye akawajibu watu, “Enyi watu wa Israel, kwa nini mnashangaa? Kwa nini mnayaelekeza macho yenu kwetu, kama kwamba tumemfanya huyu atembee kwa nguvu zetu wenyewe au uchaji wetu?”
But when Peter saw it, he answered the people: Men of Israel, why are you astonished at this? or, why do you look so earnestly on us, as if by our own power or godliness we had caused this man to walk?
13 Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Yakobo, Mungu wa Baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu. Huyu ndiye ambaye ninyi mlimkabidhi na kumkataa mbele ya uso wa Pilato, japo yeye alikuwa ameamua kumwachia huru.
The God of Abraham, and of Isaac, and of Jacob, the God of our fathers, has glorified his Son Jesus, whom you delivered up, and whom you rejected in the presence of Pilate, when he was determined to release him.
14 Mlimkataa Mtakatifu na Mwenye Haki, na badala yake mkataka muuaji aachwe huru.
But you rejected the Holy and Just One, and demanded that a murderer should be given to you;
15 Ninyi mlimuua Mfalme wa uzima, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu - Sisi ni mashahidi wa hili.
and you slew the Author of life, whom God has raised from the dead, of which we are witnesses.
16 Sasa, kwa imani katika jina lake, mtu huyu ambaye mnamwona na kujua, alifanywa kuwa na nguvu. Imani ambayo inapitia kwa Yesu imempa yeye afya hii kamilifu, mbele yenu ninyi nyote.
And his name, by faith in his name, has made this man strong whom you see and know; even the faith which is by him, has given him this entire soundness in the presence of you all.
17 Sasa, Ndugu, najua kwamba mlitenda katika ujinga, ndivyo pia walivyofanya viongozi wenu.
And now, brethren, I know that through ignorance you did this, as did also your rulers.
18 Lakini mambo ambayo Mungu aliwaambia mapema kwa vinywa vya manabii wote, kwamba huyu Kristo atateseka, sasa ameyatimiza.
But the things which God foretold by the mouth of all his prophets, that the Christ should suffer, he has thus fulfilled.
19 Kwa hiyo, tubuni na mgeuke, ili kwamba dhambi zenu ziweze kuondolewa kabisa, kusudi zije nyakati za kuburudika kutokana na uwepo wa Bwana;
Repent, therefore, and turn, in order that your sins may be blotted out, so that seasons of refreshing may come from the presence of the Lord,
20 na kwamba aweze kumtuma Kristo ambaye ameshateuliwa kwa ajili yenu, Yesu.
and that he may send Jesus Christ, who was destined for you;
21 Yeye ndiye ambaye lazima mbingu zimpokee mpaka wakati wa kurejeshwa kwa vitu vyote, ambavyo Mungu alizungumzia zamani za kale kwa vinywa vya manabii watakatifu. (aiōn g165)
whom heaven must retain, till the time for restoring all things that God has spoken by the mouth of his holy prophets of ancient times. (aiōn g165)
22 Hakika Musa alisema, 'Bwana Mungu atainua nabii kama mimi kutoka katika ndugu zenu. Mtamsikiliza kila kitu ambacho atawaambia ninyi.
For Moses said to the fathers, A prophet like me shall the Lord your God raise up for you from among your brethren; him shall you hear in all things that he shall say to you.
23 Itatokea kwamba kila mtu ambaye hasikilizi kwa nabii huyo ataangamizwa kabisa atoke kati ya watu.'
And it shall come to pass, that every soul that will not hear that prophet, shall be destroyed from among the people.
24 Ndiyo, na manabii wote tokea Samweli na wale waliofuata baada yake, walizungumza na walitangaza siku hizi.
And all the prophets, from Samuel and those that follow after, as many as have spoken, have also foretold these days.
25 Ninyi ni wana wa manabii na wa agano ambalo Mungu alilifanya pamoja na mababu, kama alivyosema kwa Abrahamu, 'Katika mbegu yako familia zote za dunia zitabarikiwa.'
You are the sons of the prophets, and of the covenant that God made with our fathers, saying to Abraham, And in your offspring shall all the families of the earth be blessed.
26 Baada ya Mungu kumwinua mtumishi wake, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki ninyi kwa kugeuka kutoka katika uovu wenu.”
To you first, God, having raised up his Son Jesus, has sent him to bless you, in turning every one of you away from his iniquities.

< Matendo 3 >