< Matendo 28 >

1 Tulipofikishwa salama, tulitambua kwamba kisiwa kinaitwa Malta.
After we [(exc)] had arrived safely [on the shore], we learned that it was an island called Malta.
2 Watu wenyeji wa pale si tu kwamba walitupa ukarimu wa kawaida, bali waliwasha moto na kutukaribisha sote, kwa sababu ya mvua na baridi iliyokuwa ikiendelea.
The people who lived there received us kindly. They lit a fire and invited us to come and warm ourselves, because it was raining and it was cold.
3 Lakini Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni na kuuweka motoni, nyoka mdogo mwenye sumu akatoka kwenye zile kuni kwa sababu ya lile joto, na akajizungusha kwenye mkono wake.
Paul gathered some sticks and put them on the fire. But [among those sticks was] a snake that had come out [from the fire to escape] from the heat, and it fastened itself on Paul’s hand.
4 Watu wenyeji wa pale walipoona mnyama ananing'inia kutoka kwenye mkono wake, wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu hakika ni muuaji ambaye ametoroka baharini, lakini haki haimuruhusu kuishi.”
[The islanders knew that the snake was poisonous, so] when they saw it hanging from Paul’s hand, they said to each other, “Probably this man has murdered someone. Although he has escaped from being drowned, [the god] ([who] pays [people back/who punishes people]) for their [MTY] sins will cause him to die.”
5 Lakini yeye akamtupia huyo mnyama katika moto na hakupata madhara yoyote.
But Paul simply shook the snake off into the fire, and nothing happened to him.
6 Wao walimngojea avimbe kwa homa au aanguke ghafla na kufa. Lakini baada ya kumwangalia kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna jambo ambalo si la kawaida kwake, walibadilisha mawazo yao na kusema alikuwa mungu.
The people were expecting that Paul’s body would soon swell up or that he would suddenly fall down and die. But after they had waited a long time, they saw [that the snake] had not harmed him [at all]. So then the people changed their minds and said [to one another], “This man is not a murderer! Probably he is a god!”
7 Basi mahali pale karibu palikuwa na ardhi ambayo ilikuwa mali ya mkuu wa kisiwa, mtu aliyeitwa Pablio. Alitukaribisha na kutukarimu kwa siku tatu.
Near where the people had made the fire, there were some fields that belonged to a man whose name was Publius. He was the chief official on the island. He invited us to [come and stay in] his home. He took care of us for three days.
8 Ilitokea kwamba baba wa Pablio alishikwa na homa na ugonjwa wa kuhara. Na Paulo alipomwendea, aliomba, akaweka mikono juu yake, na kumponya.
[At that time] Publius’ father had a fever and dysentery, and he was lying [in bed]. So Paul visited him and prayed [for him. Then] Paul placed his hands on him and healed him.
9 Baada ya hili kutokea, watu wengine pale kisiwani waliokuwa wanaumwa pia walikwenda na waliponywa.
After Paul had done that, the other people on the island who were sick came [to him] and [he] healed them, too.
10 Watu wakatuheshimu kwa heshima nyingi. Tulipokuwa tunajiandaa kusafiri, walitupa vile tulivyovihitaji.
They brought us gifts and [showed in other ways that] they greatly respected us. When we were [ready] to leave [three months later], they brought us food and other things that we would need [for the trip].
11 Baada ya miezi mitatu, tulisafiri ndani ya meli ya Iskanda ambayo ilikuwa imepigwa baridi hapo kisiwani, ambayo viongozi wake walikuwa ndugu wawili mapacha.
After [we had stayed there] three months, we [got on] a ship [that was going to Italy and] sailed away. The ship had been in [a harbor on] the island during the months when there are many storms. It had come from Alexandria [city]. On the front of the ship there were carved images of the twin gods [whose names were Castor and Pollux].
12 Baada ya kuwa tumetua katika mji wa Sirakusa, tulikaa pale siku tatu.
We [sailed from the island and] arrived at Syracuse [city on Sicily island] and stayed there three days.
13 Kutokea pale tulisafiri tukafika katika mji wa Regio. Baada ya siku moja upepo wa kusini ulitokea ghafla, na baada ya siku mbili tukafika katika mji wa Putoli.
Then we traveled on by ship and arrived at Rhegium [port in Italy]. The next day, the wind was blowing from behind us, [so we sailed along fast]. The day after that, we reached Puteoli [town, where we left the ship].
14 Huko tuliwakuta baadhi ya ndugu na tulikaribishwa kukaa nao kwa siku saba. Kwa njia hii tukaja Rumi.
In Puteoli we met some believers who invited us to stay with them for a week. [After visiting them], we [left there and started to travel by land] to Rome.
15 Kutoka huko wale ndugu, baada ya kuwa wamesikia habari zetu, walikuja kutupokea huko soko la Apias na Hotel tatu. Paulo alipowaona wale ndugu alimshukuru Mungu akajitia ujasiri.
[A group of] believers [who lived in Rome] had heard that we [(exc) were coming]. So they came out [from Rome] to meet us. [Some of] them met us at [the town called] ‘The Market on Appian [Road’, ] and others met us at [the town called] ‘The Three Inns’. When Paul saw those believers, he thanked God and was encouraged.
16 Tulipoingia Roma, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake pamoja na yule askari aliyekuwa akimlinda.
After we [(exc)] arrived in Rome, Paul was permitted {[a Roman official who was responsible for guarding Paul] permitted Paul} to live [in a house] by himself. But [there was always] a soldier there to guard him.
17 Basi ilikuwa baada ya siku tatu Paulo aliwaita pamoja wale wanume waliokuwa viongozi kati ya Wayahudi. Walipokuja pamoja, alisema kwao, “Ndugu, pamoja na kwamba sijafanya kosa lolote kwa watu hawa au kufanya kinyume na taratibu za mababa zetu waliotutangulia, nilitolewa kama mfungwa kutoka Yerusalemu hadi kwenye mikono ya Warumi.
After [Paul had been there] three days, he sent a message to the Jewish leaders [to come and talk with him. So] they came, and Paul said to them, “My fellow Jews, although I have not opposed our people nor spoken against the customs of our ancestors, [our leaders] in Jerusalem [seized] [MTY] [me. But before they could kill me, a Roman commander rescued me and later sent me] to Caesarea for Roman [authorities/officials to put me on trial].
18 Baada ya kunihoji, walitamani kuniacha huru, kwa sababu kulikuwa hakuna sababu kwangu mimi ya kustahili adhabu ya kifo.
The Roman authorities/officials questioned me and wanted to release me, because I had not done any [bad] thing for which I should be executed {they should kill me}.
19 Lakini wale Wayahudi walipoongea kinyume cha shauku yao, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisaria, japokuwa haikuwa kana kwamba naleta mashtaka juu ya taifa langu.
But when the Jewish [leaders] [SYN] there opposed [what the Roman authorities wanted to do], I had to formally request that the Emperor [judge me here in Rome]. But my reason for doing that was not that I wanted to accuse our leaders about anything.
20 Kwa sababu ya kukata kwangu rufaa, hivyo, niliomba kuwaona na kuongea nanyi. Ni kwa sababu ya kile ambacho Israel anaujasiri kwacho, nimefungwa na kifungo hiki.
So I have requested you [to come] here so that I can tell you why I am a prisoner. It is because I believe in [MTY] our Messiah, the one [God long ago promised to send] to us [(inc)] Jews.”
21 Kisha wakamwambia, “Hatujawahi kupokea barua kutoka Yudea kukuhusu wewe, wala hakuna ndugu aliyekuja na kutoa taarifa au kusema neno lolote baya kuhusu wewe.
Then [the Jewish leaders] said, “We [(exc)] have not received any letters from [our fellow Jews] in Judea about you. Also, none of our fellow Jews who have arrived [here from Judea] has said anything bad about you.
22 Lakini tunataka kusikia kutoka kwako unafikiri nini kuhusu hili kundi la watu hawa, kwa sababu inajulikana kwetu kwamba linaongea kinyume kila mahali.”
But we [(exc)] want to hear what you [(sg)] think about this [Christian] sect/group, because we know that in many places [HYP] bad things are being said {people are saying bad things} about it.”
23 Walipokuwa wametenga siku kwa ajili yake, watu wengi zaidi walimwijia mahali alipokuwa anaishi. Alisema lile jambo kwao na kushuhudia kuhusu ufalme wa Mungu. Alijaribu kuwashawishi kuhusu Yesu, kwa namna zote mbili kutoka katika sheria za Musa na kutoka kwa manabii, kuanzia asubuhi hadi jioni.
So they [talked with Paul and decided that they would come back on another day to hear him. When that day arrived], those Jews came back to the place where Paul was staying, and they brought more Jews with them. Paul talked to them from morning until evening. He talked to them about how God wants to rule [people’s lives] [MET]. He tried to convince them that Jesus [is the Messiah] by reminding them what Moses and the other prophets had written [MTY].
24 Baadhi yao walishawishika kuhusu mambo yale yaliyosemwa, wakati wengine hawakuamini.
Some of those Jews believed that what was said [by Paul] {what [Paul] said} about Jesus [was true], but others did not believe [that it was true].
25 Waliposhindwa kukubaliana wao kwa wao, waliondoka baada ya Paulo kulisema jambo hili moja, “Roho Mtakatifu alisema vyema kupitia Isaya nabii kwa baba zenu.
So they began to argue with one another. [Paul realized that some of them did not want to listen to him, so] when they were about to leave, he said, “The Holy Spirit said something to your/our(incl) ancestors. He spoke these words to Isaiah the prophet, [and what he said is also true about you]:
26 Alisema, 'Nenda kwa watu hawa useme, “Kwa masikio yenu mtasikia, lakini hamtaelewa; Na kwa macho yenu mtaona lakini hamtatambua.
Go to your fellow Israelites and tell them, ‘You repeatedly listen [to the message of God], but you never understand [what God is saying]. You repeatedly look at and see [the things that God is doing], but you never understand [what they mean].
27 Kwa ajili ya mioyo ya watu hawa imekuwa dhaifu, masikio yao yamesikia kwa taabu, wamefumba macho yao; ili kwamba wasijekutambua kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kuelewa kwa mioyo yao, na kugeuka tena, na ningeliwaponya.”'
God also said to the prophet, These people do not understand, because they have become stubborn. They have ears, but they do not understand what they hear, and they have closed their eyes [because they do not want to see]. If they wanted to obey what I say to them, they might understand what they see [me doing] and what they hear [me saying]. Then they might turn from their sinful behavior and I would save them.’
28 Kwa hiyo, mnapaswa kujua kwamba huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, na watasikiliza.” (Zingatia: Mstari huu
[That is what God said to the prophet Isaiah about our ancestors. But you Jews today do not want to believe God’s message]. Therefore, I am telling you that [God] has sent to the non-Jews this message about how he saves people, and they will listen [and accept it]!”
29 “Wakati alipokuwa amesema mambo haya, wayahudi waliondoka, wakiwa na mashindano makubwa kati yao.,” haumo kwenye nakala bora za kale).
30 Paulo alikaa katika nyumba yake ya kupanga kwa miaka yote miwili, na aliwakaribisha wote waliokuja kwake.
For two whole years Paul stayed [there] in a house that he rented. Many people came to see him, and he received them all gladly [and talked with them].
31 Alikuwa akihubiri ufalme wa Mungu na alikuwa akifundisha mambo juu ya Bwana Yesu Kristo kwa ujasiri wote. Hakuna aliyemzuia.
He preached [and taught people] about how God could rule [their lives] [MET] and taught them about the Lord Jesus Christ. He did that without being afraid, and no one tried to stop him.

< Matendo 28 >