< Matendo 28 >

1 Tulipofikishwa salama, tulitambua kwamba kisiwa kinaitwa Malta.
And when we were escaped, we ascertained that the island was called Malta.
2 Watu wenyeji wa pale si tu kwamba walitupa ukarimu wa kawaida, bali waliwasha moto na kutukaribisha sote, kwa sababu ya mvua na baridi iliyokuwa ikiendelea.
The foreign-speaking people showed us uncommon kindness, for they lighted a fire and made us all welcome, because of the rain and because of the cold.
3 Lakini Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni na kuuweka motoni, nyoka mdogo mwenye sumu akatoka kwenye zile kuni kwa sababu ya lile joto, na akajizungusha kwenye mkono wake.
Now when Paul had gathered a bundle of sticks and thrown them on the fire, a viper crawled out because of the heat, and fastened on his hand.
4 Watu wenyeji wa pale walipoona mnyama ananing'inia kutoka kwenye mkono wake, wakasemezana wao kwa wao, “Mtu huyu hakika ni muuaji ambaye ametoroka baharini, lakini haki haimuruhusu kuishi.”
When the natives saw the reptile hanging on his hand, they began saying to one another, "No doubt this man is a murderer, whom, though he has escaped from the sea, yet justice does not allow him to live."
5 Lakini yeye akamtupia huyo mnyama katika moto na hakupata madhara yoyote.
However, he shook off the reptile into the fire and received no harm.
6 Wao walimngojea avimbe kwa homa au aanguke ghafla na kufa. Lakini baada ya kumwangalia kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna jambo ambalo si la kawaida kwake, walibadilisha mawazo yao na kusema alikuwa mungu.
But they kept expecting him to swell up or fall down dead suddenly. But after waiting a long time, and seeing no harm come to him, they changed their minds, and said over and over that he was a god.
7 Basi mahali pale karibu palikuwa na ardhi ambayo ilikuwa mali ya mkuu wa kisiwa, mtu aliyeitwa Pablio. Alitukaribisha na kutukarimu kwa siku tatu.
Now in the neighborhood there were estates belonging to the governor of the island, whose name was Publius. He received us and entertained us for three days courteously.
8 Ilitokea kwamba baba wa Pablio alishikwa na homa na ugonjwa wa kuhara. Na Paulo alipomwendea, aliomba, akaweka mikono juu yake, na kumponya.
It happened however that the father of Publius was lying ill of fever and dysentery. So Paul went to see him and prayed and laid his hands on him and healed him.
9 Baada ya hili kutokea, watu wengine pale kisiwani waliokuwa wanaumwa pia walikwenda na waliponywa.
After this all the other sick people on the island came, and continued to be restored to health.
10 Watu wakatuheshimu kwa heshima nyingi. Tulipokuwa tunajiandaa kusafiri, walitupa vile tulivyovihitaji.
These loaded us with many honors and, when at last we set sail, they put on board such things as we needed.
11 Baada ya miezi mitatu, tulisafiri ndani ya meli ya Iskanda ambayo ilikuwa imepigwa baridi hapo kisiwani, ambayo viongozi wake walikuwa ndugu wawili mapacha.
Three months passed before we set sail an Alexandrian ship which had wintered in the island. Its name was "The Twin Brothers."
12 Baada ya kuwa tumetua katika mji wa Sirakusa, tulikaa pale siku tatu.
And touching at Syracuse, we stayed there three days.
13 Kutokea pale tulisafiri tukafika katika mji wa Regio. Baada ya siku moja upepo wa kusini ulitokea ghafla, na baada ya siku mbili tukafika katika mji wa Putoli.
From thence, tacking round, we reached Rhegium. Next day a south wind sprang up, which brought us in a day to Puteoli.
14 Huko tuliwakuta baadhi ya ndugu na tulikaribishwa kukaa nao kwa siku saba. Kwa njia hii tukaja Rumi.
There we found brothers who invited us to stay a week with them. Then we reached Rome.
15 Kutoka huko wale ndugu, baada ya kuwa wamesikia habari zetu, walikuja kutupokea huko soko la Apias na Hotel tatu. Paulo alipowaona wale ndugu alimshukuru Mungu akajitia ujasiri.
From there the brothers, when they heard about us, came out to meet us as far as the Appian Forum and the Three Taverns. When Paul saw them he thanked God and took courage.
16 Tulipoingia Roma, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake pamoja na yule askari aliyekuwa akimlinda.
When we finally entered Rome, Paul was allowed to live by himself with the soldier to guard him.
17 Basi ilikuwa baada ya siku tatu Paulo aliwaita pamoja wale wanume waliokuwa viongozi kati ya Wayahudi. Walipokuja pamoja, alisema kwao, “Ndugu, pamoja na kwamba sijafanya kosa lolote kwa watu hawa au kufanya kinyume na taratibu za mababa zetu waliotutangulia, nilitolewa kama mfungwa kutoka Yerusalemu hadi kwenye mikono ya Warumi.
Now three days later he called the leading Jews together, and when they were come together he said to them. "Brothers, I was delivered a prisoner from Jerusalem into the hands of the Romans, though I had done nothing against the people or the customs of your fathers.
18 Baada ya kunihoji, walitamani kuniacha huru, kwa sababu kulikuwa hakuna sababu kwangu mimi ya kustahili adhabu ya kifo.
"Then when they had examined me they wanted to set me at liberty because there was no cause of death in me.
19 Lakini wale Wayahudi walipoongea kinyume cha shauku yao, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisaria, japokuwa haikuwa kana kwamba naleta mashtaka juu ya taifa langu.
"But when the Jews objected I was forced to appeal to Caesar, not that I had anything to accuse my nation of.
20 Kwa sababu ya kukata kwangu rufaa, hivyo, niliomba kuwaona na kuongea nanyi. Ni kwa sababu ya kile ambacho Israel anaujasiri kwacho, nimefungwa na kifungo hiki.
This is the reason why I begged you to see and speak with me. For because of the hope of Israel I am bound with this chain."
21 Kisha wakamwambia, “Hatujawahi kupokea barua kutoka Yudea kukuhusu wewe, wala hakuna ndugu aliyekuja na kutoa taarifa au kusema neno lolote baya kuhusu wewe.
They said to him. "We neither received any letters about you from Judea nor has any brother come hither to report or speak any harm of you.
22 Lakini tunataka kusikia kutoka kwako unafikiri nini kuhusu hili kundi la watu hawa, kwa sababu inajulikana kwetu kwamba linaongea kinyume kila mahali.”
"But we are eager to hear from you what it is that you believe; for we all know that as for this sect it is everywhere spoken against."
23 Walipokuwa wametenga siku kwa ajili yake, watu wengi zaidi walimwijia mahali alipokuwa anaishi. Alisema lile jambo kwao na kushuhudia kuhusu ufalme wa Mungu. Alijaribu kuwashawishi kuhusu Yesu, kwa namna zote mbili kutoka katika sheria za Musa na kutoka kwa manabii, kuanzia asubuhi hadi jioni.
So they arranged a day with him and came to him in his lodgings in great numbers. He expounded the matter to them; testifying to the Kingdom of God, and persuading them about Jesus, from morning till evening, both from the Law of Moses and from the Prophets.
24 Baadhi yao walishawishika kuhusu mambo yale yaliyosemwa, wakati wengine hawakuamini.
Some began to believe what he said, but some were unbelieving.
25 Waliposhindwa kukubaliana wao kwa wao, waliondoka baada ya Paulo kulisema jambo hili moja, “Roho Mtakatifu alisema vyema kupitia Isaya nabii kwa baba zenu.
Unable to agree among themselves, they began to go, but not before Paul had spoken a word to them, saying. "Right well did the Holy Spirit say to your ancestors, through the prophet Isaiah.
26 Alisema, 'Nenda kwa watu hawa useme, “Kwa masikio yenu mtasikia, lakini hamtaelewa; Na kwa macho yenu mtaona lakini hamtatambua.
"Go to the people and tell them, You will hear and hear, and by no means understand; And will look, and by no means see.
27 Kwa ajili ya mioyo ya watu hawa imekuwa dhaifu, masikio yao yamesikia kwa taabu, wamefumba macho yao; ili kwamba wasijekutambua kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kuelewa kwa mioyo yao, na kugeuka tena, na ningeliwaponya.”'
For this people’s heart is grown obtuse, Their ears are heavy of hearing, Their eyes have they closed, Lest they should see with their eyes And hear with their ears, Lest they understand with their heart, And turn again, and heal them.
28 Kwa hiyo, mnapaswa kujua kwamba huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, na watasikiliza.” (Zingatia: Mstari huu
"Be fully assured, therefore, that this salvation of God is now sent unto the Gentiles. They will listen to it."
29 “Wakati alipokuwa amesema mambo haya, wayahudi waliondoka, wakiwa na mashindano makubwa kati yao.,” haumo kwenye nakala bora za kale).
When he finished speaking, the Jews departed, and reasoned among themselves.
30 Paulo alikaa katika nyumba yake ya kupanga kwa miaka yote miwili, na aliwakaribisha wote waliokuja kwake.
After this Paul lived for two whole years in his own rented house, and used to receive all who came to see him.
31 Alikuwa akihubiri ufalme wa Mungu na alikuwa akifundisha mambo juu ya Bwana Yesu Kristo kwa ujasiri wote. Hakuna aliyemzuia.
He continued to preach the kingdom of God, and to teach about the Lord Jesus Christ with all boldness, quite unmolested.

< Matendo 28 >