< Matendo 27 >
1 Ilipoamuliwa kwamba tunatakiwa tusafiri kwa maji kwenda Italia, walimkabidhi Paulo na wafungwa wengine kwa afisa mmoja wa jeshi la Kiroma aliyeitwa Julio, wa Kikosi cha Agustani.
Men da det var besluttet, at vi skulde afsejle til Italien, overgave de både Paulus og nogle andre Fanger til en Høvedsmand ved Navn Julius af den kejserlige Afdeling.
2 Tukapanda meli kutoka Adramitamu, ambayo ilikuwa isafiri kandokando ya pwani ya Asia. Hivyo tukaingia baharini. Aristaka kutoka Thesolanike ya Makedonia akaenda pamoja nasi.
Vi gik da om Bord på et adramyttisk Skib, som skulde gå til Stederne langs med Asiens Kyster, og vi sejlede af Sted; og Aristarkus, en Makedonier fra Thessalonika, var med os.
3 Siku iliyofuata tukatua nanga katika mji wa Sidoni, ambapo Julio alimtendea Paulo kwa ukarimu na akamruhusu kwenda kwa rafiki zake kupokea ukarimu wao.
Og den næste Dag anløb vi Sidon. Og Julius, som behandlede Paulus venligt. tilstedte ham at gå hen til sine Venner og nyde Pleje.
4 Kutoka hapo tukaenda baharini tukasafiri kuzunguka kisiwa cha Kipro ambacho kilikuwa kimeukinga upepo, kwa sababu upepo ulikuwa ukitukabili.
Og vi fore bort derfra og sejlede ind under Kypern, fordi Vinden var imod.
5 Baada ya kuwa tumesafiri katika maji yaliyo karibu na Kilikia na Pamfilia, tukaja Mira, mji wa Lisia.
Og vi sejlede igennem Farvandet ved Kilikien og Pamfylien og kom til Myra i Lykien.
6 Pale yule afisa wa jeshi la Kiroma, akaikuta meli kutoka Alexandria ambayo ilikuwa isafiri kuelekea Italia. Akatupandisha ndani yake.
Og der fandt Høvedsmanden et aleksandrinsk Skib, som sejlede til Italien, og bragte os over i det.
7 Baada ya kuwa tumesafiri polepole kwa siku nyingi na hatimaye tukawa tumefika kwa taabu karibu na Kinidas, upepo haukuturuhusu tena kuelekea njia hiyo, hivyo tukasafiri kandokando ya kivuli cha Krete tukiukinga upepo, mkabala na Salmone.
Men da Sejladsen i mange Dage gik langsomt, og vi med Nød og næppe nåede henimod Knidus (thi Vinden føjede os ikke), holdt vi ned under Kreta ved Salmone.
8 Tukasafiri kandokando ya pwani kwa ugumu, mpaka tukafika mahali palipoitwa Fari Haveni ambayo iko karibu na mji wa Lasi.
Med Nød og næppe sejlede vi der forbi og kom til et Sted, som kaldes "Gode Havne", nær ved Byen Lasæa.
9 Tulikuwa tumechukua muda mwingi sana, na muda wa mfungo wa Kiyahudi ulikuwa umepita pia, na sasa ilikuwa ni hatari kuendelea kusafiri. Hivyo Paulo akatuonya,
Men da en rum Tid var forløben, og Sejladsen allerede var farlig, såsom endog Fasten allerede var forbi, formanede Paulus dem og sagde:
10 na kusema, “Wanaume, naona safari ambayo tunataka tuichukue itakuwa na madhara na hasara nyingi, siyo tu ya mizigo na meli, lakini pia ya maisha yetu.”
"I Mænd! jeg ser, at Sejladsen vil medføre Ulykke og megen Skade, ikke alene på Ladning og Skib, men også på vort Liv."
11 Lakini afisa wa jeshi la Kiroma akamsikiliza zaidi bwana wake na mmiliki wa meli, kuliko mambo yale ambayo yalizungumzwa na Paulo.
Men Høvedsmanden stolede mere på Styrmanden og Skipperen end på det, som Paulus sagde.
12 Kwa sababu bandari haikuwa sehemu rahisi kukaa wakati wa baridi, mabaharia wengi wakashauri tusafiri kutoka pale, ili kwa namna yoyote tukiweza kuufikia mji wa Foinike, tukae pale wakati wa baridi. Foinike ni bandari huko Krete, na inatazama kaskazini mashariki na kusini mashariki.
Og da Havnen ikke egnede sig til Vinterleje, besluttede de fleste, at man skulde sejle derfra, om man muligt kunde nå hen og overvintre i Føniks, en Havn på Kreta, som vender imod Sydvest og Nordvest,
13 Upepo wa kusini ulipoanza kuvuma polepole, mabaharia wakafikiri wamepata kile ambacho walikuwa wanakihitaji. Wakang'oa nanga na kusafiri kandokando ya Krete karibu na pwani.
Da der nu blæste en Sønden: vind op, mente de at have nået deres Hensigt, lettede Anker og sejlede langs med og nærmere ind under Kreta.
14 Lakini baada ya muda mfupi upepo mkali, ulioitwa Wa kaskazini mashariki, ukaanza kutupiga kutoka ng'ambo ya kisiwa.
Men ikke længe derefter for der en heftig Storm ned over den, den såkaldte "Eurakvilo".
15 Wakati meli ilipolemewa na kushindwa kuukabili upepo, tukakubaliana na hali hiyo, tukasafirishwa nao.
Og da Skibet reves med og ikke kunde holde op imod Vinden, opgave vi det og lode os drive.
16 Tukakimbia kupitia ule upande uliokuwa unaukinga upepo wa kisiwa kiitwacho Kauda; na kwa taabu sana tulifanikiwa kuuokoa mtumbwi.
Men da vi løb ind under en lille Ø, som kaldes Klavde, formåede vi med Nød og næppe at bjærge Båden.
17 Baada ya kuwa wameivuta, walitumia kamba kuifunga meli. Waliogopa kwamba tungeweza kwenda kwenye eneo la mchanga mwingi la Syiti, hivyo wakashusha nanga na waliendeshwa kandokando.
Men efter at have trukket den op, anvendte de Nødmidler og omsurrede Skibet; og da de frygtede for, at de skulde blive kastede ned i Syrten, firede de Sejlene ned og lode sig således drive.
18 Tulipigwa kwa nguvu sana na dhoruba, hivyo siku iliyofuata mabaharia wakaanza kutupa mizigo kutoka melini.
Og da vi måtte kæmpe hårdt med Stormen, begyndte de næste Dag at kaste over Bord.
19 Siku ya tatu, mabaharia wakaanza kuyatoa maji kwa mikono yao wenyewe.
Og på den tredje Dag udkastede de med egne Hænder Skibets Redskaber.
20 Wakati ambapo jua na nyota hazikutuangazia kwa siku nyingi, bado dhoruba kubwa ilitupiga, na matumaini kwamba tungeokolewa yalitoweka.
Men da hverken Sol eller Stjerner lode sig se i flere Dage, og vi havde et Uvejr over os; som ikke var ringe, blev fra nu af alt Håb om Redning os betaget.
21 Baada ya kuwa wameenda muda mrefu bila chakula, hapo Paulo akasimama katikati ya mabaharia akasema, “Wanaume, mlipaswa mnisikilize, na tusingengo'a nanga kutoka Krete, ili kupata haya madhara na hasara.
Og da man længe ikke havde taget Føde til sig, så stod Paulus frem midt iblandt dem og sagde: "I Mænd! man burde have adlydt mig og ikke været sejlet bort fra Kreta og have sparet os denne Ulykke og Skade.
22 Na sasa nawafariji mjitie moyo, kwa sababu hakutakuwa upotevu maisha kati yenu, isipokuwa hasara ya meli tu.
Og nu formaner jeg eder til at være ved godt Mod; thi ingen Sjæl af eder skal forgå, men alene Skibet.
23 Kwa sababu usiku uliopita malaika wa Mungu, ambaye huyo Mungu mimi ni wake, na ambaye ninamwabudu pia - malaika wake alisimama pembeni mwangu
Thi i denne Nat stod der en Engel hos mig fra den Gud, hvem jeg tilhører, hvem jeg også tjener, og sagde:
24 na kusema, “Usiogope Paulo. Lazima usimame mbele ya Kaisari, na tazama, Mungu katika wema wake amekupa hawa wote ambao wanasafiri pamoja nawe.
"Frygt ikke, Paulus! du skal blive stillet for Kejseren; og se, Gud har skænket dig alle dem, som sejle med dig."
25 Hivyo, wanaume, jipeni moyo, kwa sababu namwamini Mungu, kwamba itakuwa kama nilivyoambiwa.
Derfor, I Mænd! værer ved godt Mod; thi jeg har den Tillid til Gud, at det skal ske således, som der er blevet talt til mig.
26 Lakini lazima tuumie kwa kupigwa katika baadhi ya visiwa.”
Men vi må strande på en Ø."
27 Ulipofika usiku wa kumi na nne, tulipokuwa tukiendeshwa huko na huko kwenye bahari ya Adratik, kama usiku wa manane hivi, mabaharia walifikiri kwamba wamekaribia nchi kavu.
Men da den fjortende Nat kom, og vi dreve i det adriatiske Hav, kom det Skibsfolkene for ved Midnatstid, at der var Land i Nærheden.
28 Walitumia milio kupima kina cha maji na wakapata mita thelathini na sita, baada ya muda mfupi wakapima tena wakapata mita ishirini na saba.
Og da de loddede, fik de tyve Favne, og da de lidt længere fremme atter loddede, fik de femten Favne.
29 Waliogopa kwanza tunaweza kugonga miamba, hivyo wakashusha nanga nne kutoka katika sehemu ya kuwekea nanga na wakaomba kwamba asubuhi ingekuja mapema.
Og da de frygtede, at vi skulde støde på Skær, kastede de fire Ankre ud fra Bagstavnen og bade til, at det måtte blive Dag.
30 Wale mabaharia walikuwa wanatafuta namna ya kuitelekeza ile meli na walizishusha majini boti ndogo ndogo za kuokolea maisha, na wakajifanya kwamba wanatupa nanga kutoka sehemu ya mbele ya boti.
Men da Skibsfolkene gjorde Forsøg på at flygte fra Skibet og firede Båden ned i Søen under Påskud af, at de vilde lægge Ankre ud fra Forstavnen,
31 Lakini Paulo akamwambia yule askari wa jeshi la Kiroma na wale askari, “Hamuwezi kuokoka isipokuwa hawa watu wanabaki kwenye meli”.
da sagde Paulus til Høvedsmanden og til Stridsmændene: "Dersom disse ikke blive i Skibet, kunne I ikke reddes."
32 Kisha wale askari wakakata kamba za ile boti na ikaachwa ichukuliwe na maji.
Da kappede Stridsmændene Bådens Tove og lode den falde ned.
33 Wakati mwanga wa asubuhi ulipokuwa unajitokeza, Paulo akawasihi wote angalau wale kidogo. Akasema, “Hii ni siku ya kumi na nne mnasuburi bila kula, hamjala kitu.
Men indtil det vilde dages, formanede Paulus alle til at tage Næring til sig og sagde: "Det er i Dag den fjortende Dag, I have ventet og tilbragt uden at spise og intet taget til eder.
34 Hivyo nawasihi mchukue chakula kidogo, kwa sababu hii ni kwa ajili ya kuishi kwenu; na hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Derfor formaner jeg eder til at tage Næring til eder, thi dette hører med til eders Redning; ikke et Hår på Hovedet skal gå tabt for nogen af eder."
35 Alipokwisha kusema hayo, akachukua mkate akamshukuru Mungu mbele ya macho ya kila mtu. Kisha akaumega mkate akaanza kula.
Men da han havde sagt dette, tog han Brød og takkede Gud for alles Øjne og brød det og begyndte at spise.
36 Kisha wote wakatiwa moyo na wao wakachukua chakula.
Da bleve de alle frimodige og toge også Næring til sig.
37 Tulikuwa watu 276 ndani ya meli.
Men vi vare i Skibet i alt to Hundrede og seks og halvfjerdsindstyve Sjæle.
38 Walipokwisha kula vya kutosha, waliifanya meli nyepesi kwa kutupa ngano ndani ya bahari.
Og da de vare blevne mættede med Føde, lettede de Skibet ved at kaste Levnedsmidlerne i Søen.
39 Ilipokuwa mchana, hawakuitambua nchi kavu, lakini wakaona sehemu ya nchi kavu iliyoingia majini iliyokuwa na mchanga mwingi. wakajadiliana kama wanaweza kuiendesha meli kuelekea hapo.
Men da det blev Dag, kendte de ikke Landet; men de bemærkede en Vig med en Forstrand, som de besluttede, om muligt, at sætte Skibet ind på.
40 Hivyo wakazilegeza nanga wakaziacha baharini. Katika muda huo huo wakazilegeza kamba za tanga na wakaiinua sehemu ya mbele kuelekea kwenye upepo, hivyo wakaelekea kwenye hiyo sehemu ya mchanga mwingi.
Og de kappede Ankrene, som de lode blive i Søen, og løste tillige Rortovene, og idet de satte Råsejlet til for Vinden, holdt de ind på Strandbredden.
41 Lakini wakaja mahali ambapo mikondo miwili ya maji inakutana, na meli ikaelekea mchangani. Na ile sehemu ya mbele ya meli ikakwama pale na haikuweza kutoka, lakini sehemu ya mbele ya meli ikaanza kuvunjika kwa sababu ya ukali wa mawimbi.
Men de stødte på en Grund med dybt Vand på begge Sider, og der satte de Skibet, og Forstavnen borede sig fast og stod urokkelig, men Bagstavnen sloges sønder af Bølgernes Magt.
42 Mpango wa wale askari ulikuwa ni kuwaua wafungwa, ili kwamba hakuna ambaye angeogelea na kutoroka.
Det var nu Stridsmændenes Råd, at man skulde ihjelslå Fangerne, for at ingen skulde svømme bort og undkomme.
43 Lakini yule askari wa jeshi la Kiroma alitaka kumwokoa Paulo, hivyo akausimamisha mpango wao; na akawaamuru wale ambao wanaweza kuogelea, waruke kutoka melini kwanza na waende nchi kavu.
Men Høvedsmanden, som vilde frelse Paulus, forhindrede dem i dette Forehavende og bød, at de, som kunde svømme, skulde først kaste sig ud og slippe i Land,
44 Kisha wanaume wengine watafuata, wengine juu ya vipande vya mbao na wengine juu ya vitu vingine kutoka kwenye meli. Kwa njia hii ikatokea kwamba wote tutafika salama nchi kavu.
og de andre bjærge sig, nogle på Brædder, andre på Stykker af Skibet. Og således skete det, at alle bleve reddede i Land.