< Matendo 21 >

1 Wakati tulipokua tumeachana nao, na tunasafiri baharini, tukafika moja kwa moja kwenye mji wa Kosi, na kesho yake tukafika mji wa Rodo, na kutoka huko tukafika mji wa Patara.
And when it came to pass, that we having been farewelled by them, embarked, sailing straight forward, we arrived at Cos, and on the following day to Rhodes, and thence to Patara.
2 Tulipopata meli inayovuka kwenda Foinike, tulipanda tukasafiri.
And finding a ship sailing into Phoenicia, having embarked, we moved out.
3 Tulipofika mbele ya kisiwa cha Kipro, tukaiacha upande wa kushoto, tukasafiri hadi Siria, tukaweka nanga katika mji wa Tiro, kwa sababu huko ndiko meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
And coming in sight of Cyprus, and leaving it on the left, we sailed to Syria, and disembarked at Tyre: for there the ship was delivering her cargo.
4 Baada ya kuwaona wanafunzi, tukakaa huko siku saba. Wanafunzi hawa wakamwambia Paulo kupitia kwa Roho kwamba yeye asikanyage Yerusalemu.
And finding disciples, we tarried there seven days: who continued to say to Paul through the Spirit, that he should not go to Jerusalem.
5 Hata tulipotimiza siku zile, sisi tukaondoka tukaenda zetu. Wote pamoja, na wanawake zao na watoto wao, walitusindikiza katika njia zetu hadi tulipotoka nje ya mji. Kisha tukapiga magoti pwani, tukaomba, tukaagana kila mmoja.
And when it came to pass that we refitted during those days, having come out, we departed, all sending us forth, along with the women and children, out of the city: and putting down the knees on the shore, having prayed,
6 Tukapanda meli, huku nao wakarudi nyumbani kwao tena.
we farewelled one another, and went up into the ship; and they returned to their own homes.
7 Hata tulipomaliza safari yetu kutoka Tiro, tukafika Tolemai. Pale tulisalimia ndugu, na kukakaa nao kwa siku moja.
And we continuing our voyage from Tyre, we arrived at Ptolemais, and having saluted the brethren, we remained with them one day.
8 Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisaria. Sisi tukaingia nyumbani mwa Filipo, mhubiri wa injili, aliyekuwa mmoja wa wale saba, nasi tukakaa pamoja naye.
And on the following day, having come out, we came into Caesarea: and having entered into the house of Philip the evangelist, being one of the seven, we abode with him.
9 Mtu huyu alikuwa na mabinti wanne mabikira ambao walitabiri.
And there were to him four virgin daughters, prophesying.
10 Baada ya kukaa huko kwa siku kadhaa, akashuka kutoka Uyahudi nabii mmoja aitwaye Agabo.
And we remaining many days, a certain prophet, by name Agabus, came down from Judea;
11 Yeye alikuja kwetu na akautwaa mkanda wa Paulo. kwa huo alijifunga miguu na mikono yake mwenyewe na kusema, “Roho Mtakatifu asema hivi,” “Wayahudi wa Yerusalemu watamfunga mtu anayemiliki mkanda huu, nao watamkabidhi mikononi mwa watu wa mataifa.”
and having come to us, and taking the girdle of Paul, binding his own feet and hands, said, These things says the Holy Ghost, The man whose girdle this is, will the Jews in Jerusalem bind and deliver into the hands of the Gentiles.
12 Tuliposikia mambo hayo, sisi na watu waliokuwa wakiishi mahali pale tulimsihi Paulo asipande kwende Yerusalemu.
And when we heard these words, both we, and the citizens, exhorted him not to go up to Jerusalem.
13 Ndipo Paulo alijibu, “Mnafanya nini, mnalia na kunivunja moyo wangu? Kwa maana niko tayari, siyo tu kufungwa, lakini pia kufia huko Yerusalemu kwa ajili ya jina la Bwana Yesu.”
Then Paul responded and said, What are you doing, weeping and breaking my heart? for I am ready not only to be bound, but to die in Jerusalem for the name of the Lord Jesus.
14 Kwa vile Paulo hakutaka kushawishiwa, tuliacha na kusema, “Basi mapenzi ya Bwana yafanyike.”
And he not being persuaded, we acquiesced, saying, Let the will of the Lord be done.
15 Baada ya siku hizi, tulichukua mifuko yetu na tukapanda Yerusalemu.
And after those days, taking our luggage, we went up to Jerusalem:
16 Baadhi ya wanafunzi kutoka Kaisaria pia walifuatana nasi. Wakamleta mtu mmoja aitwaye Mnasoni, mtu wa Kipro, mwanafunzi wa zamani, ambaye tulikaa naye.
and some of the disciples from Caesarea went along with us, bringing Mnason a certain Cyprian, an old disciple, with whom we should lodge.
17 Tulipofika Yerusalemu, ndugu walitukaribisha kwa furaha.
And we being in Jerusalem, the brethren received us gladly.
18 Kesho yake Paulo alienda pamoja nasi kwa Yakobo, na wazee wote walikuwepo.
And on the following day, Paul goes with us to James; and all the elders assembled.
19 Baada ya kuwasalimu, aliwapa taarifa moja baada ya nyingine ya mambo ambayo Mungu aliyotenda miongoni mwa mataifa kwa kupitia huduma yake.
And having saluted them, he related each one of those things which God did among the Gentiles through his ministry.
20 Wakati waliposikia hayo, wakamsifu Mungu, na wakamwambia, “Unaona, ndugu, kuna maelfu wangapi wameamini miongoni mwa Wayahudi. Wao wote wana nia ya kushika sheria.
And they hearing, continued to glorify God, and said to him, You see, brother, how many myriads there are of those who believe; and they are all zealots of the law:
21 Wameambiwa kuhusu wewe, kwamba unafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa kuachana na Musa, na kwamba unawaambia wasiwatahiri watoto wao, na wasifuate desturi za zamani.
and they have been informed concerning thee, that thou art teaching all the Jews who are among the Gentiles apostasy from Moses, saying that they are not to circumcise their children, nor to walk according to the customs.
22 Tunapaswa tufanye nini? Bila shaka watasikia kwamba wewe umekuja.
Then what is it? it is altogether necessary that the multitude come together: for they will hear that you have come.
23 Hivyo fanya kile sisi tunachokuambia sasa: tunao watu wanne ambao wameweka nadhiri.
Therefore do this which we tell thee. There are four men among us having a vow upon them;
24 Wachukue watu hawa na ujitakase mwenyewe pamoja nao, na uwalipie gharama zao, ili waweze kunyoa vichwa vyao. Hivyo kila mmoja apate kujua kwamba mambo waliyoambiwa kuhusu wewe ni ya uongo. Watajifunza kwamba wewe pia unafuata sheria.
taking them, be purified along with them, and be at charges for them, that they may shave their head: and all shall know that there is nothing of those things they have been informed concerning thee; but that thyself art walking, keeping the law.
25 Lakini kwa habari za mataifa ambao wamekuwa waumini, tuliandika na kutoa maagizo kwamba wanapaswa kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu, na damu, kutokana na kile kilichonyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
But concerning the Gentiles who have believed, we have sent to them, adjudicating that they keep themselves from idolatry, and blood, and strangulation, and fornication.
26 Ndipo, Paulo aliwatwaa wanaume, na siku ya pili, akajitakasa mwenyewe pamoja nao, akaingia Hekaluni, kutangaza kipindi cha siku za kujitakasa, hadi sadaka itolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
Then Paul, having taken the men, the next day being purified along with them, enters into the temple, proclaiming the fulfillment of the days of purification, until an offering may be made for each one of them.
27 Siku hizo saba zilipokaribia kumalizika, baadhi ya Wayahudi kutoka Asia wakamuona Paulo Hekaluni, na makutano wakakasirika, na wakamnyoshea mikono.
And when the seven days were about to have an end, the Jews from Asia, seeing him in the temple, stirred up the whole multitude, and laid hands on him, crying out,
28 Walikuwa wanapiga kelele, “Watu wa Israeli, tusaidieni. Huyu ni yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo ambayo ni kinyume na watu, sheria, na mahali hapa. Pia amewaleta Wayunani katika Hekalu na kupanajisi mahali hapa patakatifu.”
Israelitish men, help: this is the man, teaching all everywhere against the people, and the law, and this place, and he has even yet led Greeks into the temple, and polluted this holy place.
29 Kwa kuwa mwanzoni walikuwa wamemwona Trofimo Muefeso akiwa pamoja naye mjini, nao walidhani kwamba Paulo alimleta hekaluni.
For they saw Trophimus the Ephesian in the city with him, whom they supposed that Paul led into the temple.
30 Mji wote ulikuwa na taharuki, na watu wakakimbia pamoja na kumkamata Paulo. Wakamtoa nje ya Hekalu, na milango mara ikafungwa.
And the whole city was excited, and there was a commotion of the people: and taking Paul, they dragged him out of the temple; and immediately the doors were closed.
31 Walipokuwa wakijaribu kumuua, habari zilimfikia mkuu wa jeshi la walinzi kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
And seeking to kill him, the report went up to the chiliarch of the band, that all Jerusalem is in commotion;
32 Mara hiyo akawachukua askari na jemadari akaukimbilia umati. Wakati Watu walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
who immediately, taking soldiers and centurions, ran to them: and they, seeing the chiliarch and the soldiers, ceased beating Paul.
33 Kisha mkuu wa jeshi alimkaribia na akamshika Paulo, na akaamuru afungwe minyororo miwili. Akamuuliza yeye ni nani na amefanya nini.
Then the chiliarch, having come nigh, took Paul, and commanded that he should be bound with two chains; and was making inquiry who he might be, and what he had done.
34 Baadhi ya watu kwenye umati walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kingine. Kwa kuwa jemadari hakuweza kuwaambia chochote kwa sababu ya zile kelele, akaamuru Paulo aletwe ndani ya ngome.
And they continued to cry aloud in the multitude, some one thing, and some another: and he, being unable to know the certainty on account of the uproar, commanded that he should be led into the castle.
35 Basi alipofika kwenye ngazi, akachukuliwa na askari kwa sababu ya ghasia za umati.
Then when he was on the threshold, it happened that he was carried by the soldiers, on account of the violence of the mob;
36 Maana umati wa watu walimfuata na waliendelea kupiga kelele, “Mwondoeni huyu!”
for the multitude of the people were following, crying out, Take him away.
37 Paulo alipokuwa analetwa ndani ya ngome, alimwambia mkuu wa jeshi, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akasema, “Je unaongea Kiyunani?
And Paul, being about to be led into the castle, says to the chiliarch, Is it lawful for me to say something to thee? And he said, Do you speak Greek?
38 Je, wewe si yule Mmisri ambaye awali aliongoza uasi na alichukua magaidi elfu nne nyikani?”
Are you not that Egyptian who before these days rising up and leading away into the desert four hundred men of daggers?
39 Paulo akasema, “Mimi ni Myahudi, kutoka mji wa Tarso ya Kilikia. Mimi ni raia wa mji maarufu. Nawaomba, mniruhusu nizungumze na watu.”
But Paul said, I am indeed a Jewish man, a Tarsean, a citizen of Cilicia, no mean city: but, I pray you, permit me to speak to the people.
40 Wakati jemadari alipompa ruhusa, Paulo akasimama penye ngazi na akatoa ishara kwa watu kwa mkono wake. Wakati kulipokuwa na ukimya sana, akaongea nao kwa Kihebrania. Akasema,
And he permitting, Paul, standing on the threshold, beckoned with his hand to the people: and there being great silence, he spoke to them in the Hebrew tongue, saying:

< Matendo 21 >