< Matendo 20 >

1 Baada ya ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi na kuwatia moyo. Kisha kuwaaga na akaondoka kwenda Makedonia.
When the uproar had ceased, Paul sent for the disciples; and, after speaking words of encouragement to them, he took his leave, and started for Macedonia.
2 Naye akiishakupita mikoa hiyo na alikuwa akiwatia moyo waamuni, akaingia Uyunani.
Passing through those districts he encouraged the disciples in frequent addresses, and then came into Greece, and spent three months there.
3 Baada ya yeye kuwa pale kwa muda wa miezi mitatu, njama ziliundwa dhidi yake na Wayahudi alipokuwa akikaribia kusafiri kwa njia ya bahari kuelekea Shamu, hivyo aliazimu kurudi kupitia Makedonia.
The Jews having planned to waylay him whenever he might be on the point of taking ship for Syria, he decided to travel back by way of Macedonia.
4 Walioandamana naye hadi Asia walikuwa Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea; Aristariko na Sekundo, wote kutoka waamini wa Wathesalonike; Gayo wa Derbe; Timotheo; Tikiko na Trofimo kutoka Asia.
He was accompanied as far as the province of Asia by Sopater the Beroean, the son of Pyrrhus; by the Thessalonians, Aristarchus and Secundus; by Gaius of Derbe, and Timothy; and by the Asians, Tychicus and Trophimus.
5 Lakini watu hawa wamekwisha tangulia na walikuwa wanatungojea kule Troa.
These brethren had gone on and were waiting for us in the Troad.
6 kwa njia ya Bahari kutoka Filipi baada ya siku za mikate isiyotiwa chachu, na katika siku tano tukawafikia huko Troa. Tulikaa huko kwa siku saba.
But we ourselves sailed from Philippi after the days of Unleavened Bread, and five days later joined them in the Troad, where we remained for a week.
7 Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekusanyika pamoja ili kuumega mkate, Paulo alizungumza na Waamini. Alikuwa akipanga kuondoka kesho yake, hivyo akaendelea kuongea hadi usiku wa manane.
On the first day of the week, when we had met to break bread, Paul, who was going away the next morning, was preaching to them, and prolonged his discourse till midnight.
8 Kulikuwa na taa nyingi katika chumba cha juu ambapo tulikuwa tumekusanyika pamoja.
Now there were a good many lamps in the room upstairs where we all were,
9 Katika dirisha alikuwa amekaa kijana mmoja jina lake Utiko, ambaye alielemewa na usingizi mzito. Hata Paulo alipokuwa akihutubu kwa muda mrefu, kijana huyu, akiwa amelala, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu na aliokotwa akiwa amekufa.
and a youth of the name of Eutychus was sitting at the window. This lad, gradually sinking into deep sleep while Paul preached at unusual length, overcome at last by sleep, fell from the second floor and was taken up dead.
10 Lakini Paulo alishuka chini, alijinyoosha yeye mwenyewe juu yake, akamkumbatia. Kisha akasema, “Msikate tamaa, kwa kuwa yu hai.”
Paul, however, went down, threw himself upon him, and folding him in his arms said, "Do not be alarmed; his life is still in him."
11 Kisha akapanda tena ghorofani na akaumega mkate, akala. Baada ya kuzungumza nao kwa muda mrefu hadi alfajiri, akaondoka.
Then he went upstairs again, broke bread, and took some food; and after a long conversation which was continued till daybreak, at last he parted from them.
12 Wakamleta yule kijana akiwa hai wakafarijika sana.
They had taken the lad home alive, and were greatly comforted.
13 Sisi wenyewe tulitangulia mbele ya Paul kwa meli na tukaelekea Aso, ambapo sisi tulipanga kumchukua Paul huko. Hiki ndicho yeye mwenyewe alitaka kufanya, kwa sababu alipanga kwenda kupitia nchi kavu.
The rest of us had already gone on board a ship, and now we set sail for Assos, intending to take Paul on board there; for so he had arranged, he himself intending to go by land.
14 Alipotufikia huko Aso, tukampakia kwenye Meli tukaenda Mitilene.
Accordingly, when he met us at Assos, we took him on board and came to Mitylene.
15 Kisha sisi tukatweka kutoka huko na siku ya pili tulifika upande wa pili wa kisiwa cha Kio. Siku iliyofuata, tukawasili kisiwa cha Samo, na kesho yake tukafika mji wa Mileto.
Sailing from there, we arrived the next day off Chios. On the next we touched at Samos; and on the day following reached Miletus.
16 Kwa sababu Paulo alikuwa ameamua kusafiri kupitia Efeso, ili kwamba asitumie muda wowote katika Asia; kwa maana alikuwa na haraka ya kuwahi Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pentekoste, kama ingeliwezekana yeye kufanya hivyo.
For Paul's plan was to sail past Ephesus, so as not to spend much time in the province of Asia; since he was very desirous of being in Jerusalem, if possible, on the day of the Harvest Festival.
17 Kutoka Mileto akatuma watu hadi Efeso na akawaita wazee wa Kanisa.
From Miletus he sent to Ephesus for the Elders of the Church to come to him.
18 Walipofika kwake, akawaambia, ninyi wenyewe mwajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu muda wote.
Upon their arrival he said to them, "You Elders well know, from the first day of my setting foot in the province of Asia, the kind of life I lived among you the whole time,
19 Nimemtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi, na mateso yaliyonipata mimi kwa hila za Wayahudi.
serving the Lord in all humility, and with tears, and amid trials which came upon me through the plotting of the Jews--
20 Mwajua jinsi ambavyo sikujizuia kutangaza kwenu kitu chochote ambacho kilikuwa muhimu, na jinsi mimi nilivyowafundisha wazi wazi na pia kwenda nyumba kwa nyumba.
and that I never shrank from declaring to you anything that was profitable, or from teaching you in public and in your homes,
21 Mnajua jinsi mimi nilivyoendelea kuwaonya Wayahudi na Wayunani juu ya toba kwa Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.
and urging upon both Jews and Greeks the necessity of turning to God and of believing in Jesus our Lord.
22 Na sasa, angalieni, mimi, nikiwa ninamtii Roho Mtakatifu kuelekea Yerusalemu, nisiyajue mambo ambayo yatanitokea mimi huko,
"And now, impelled by a sense of duty, I am on my way to Jerusalem, not knowing what will happen to me there,
23 ila kwa kuwa Roho Mtakatifu hunishuhudia mimi katika kila mji na anasema kwamba minyororo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
except that the Holy Spirit, at town after town, testifies to me that imprisonment and suffering are awaiting me.
24 Lakini mimi si kufikiria kwamba maisha yangu ni kwa njia yoyote ya thamani kwangu, ili niweze kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kuishuhudia injili ya neema ya Mungu.
But even the sacrifice of my life I count as nothing, if only I may perfect my earthly course, and be faithful to the duty which the Lord Jesus has entrusted to me of proclaiming, as of supreme importance, the Good News of God's grace.
25 Na sasa, tazama, najua kwamba wote, miongoni mwa wale nilioenda kuwahubiri Ufalme, hamtaniona uso tena.
"And now, I know that none of you among whom I have gone in and out proclaiming the coming of the Kingdom will any longer see my face.
26 Kwa hiyo nawashuhudia leo hii, kwamba sina hatia kwa damu ya mtu yeyote.
Therefore I protest to you to-day that I am not responsible for the ruin of any one of you.
27 Kwa maana sikujizuia kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
For I have not shrunk from declaring to you God's whole truth.
28 Kwa hiyo iweni waangalifu juu yenu ninyi wenyewe, na juu ya kundi lolote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi. Iweni waangalifu kulichunga kusanyiko la Bwana, ambalo alilinunua kwa damu yake mwenyewe.
"Take heed to yourselves and to all the flock among which the Holy Spirit has placed you to take the oversight for Him and act as shepherds to the Church of God, which He has bought with His own blood.
29 Najua kwamba baada ya kuondoka kwangu, mbwa mwitu wakali wataingia kwenu, na wasilihurumie kundi.
I know that, when I am gone, cruel wolves will come among you and will not spare the flock;
30 Najua kwamba hata miongoni mwenu wenyewe baadhi ya watu watakuja na kusema mambo mapotovu, ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao.
and that from among your own selves men will rise up who will seek with their perverse talk to draw away the disciples after them.
31 Kwa hiyo muwe macho. Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuweza kuacha kuwafundisha kila mmoja wenu kwa machozi usiku na mchana.
Therefore be on the alert; and remember that, night and day, for three years, I never ceased admonishing every one, even with tears.
32 Na sasa mimi nawakabidhi kwa Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliowekwa wakfu kwa Mungu.
"And now I commend you to God and to the word of His grace. He is able to build you up and to give you your inheritance among His people.
33 Sikutamani fedha, dhahabu, au mavazi.
No one's silver or gold or clothing have I coveted.
34 Mnajua ninyi wenyewe kwamba mikono hii imenipatia mahitaji yangu mwenyewe na mahitaji ya wale waliokuwa pamoja nami.
You yourselves know that these hands of mine have provided for my own necessities and for the people with me.
35 Katika mambo yote niliwapa mfano wa jinsi inavyopasa kuwasaidia wanyonge kwa kufanya kazi, na jinsi mnavyopaswa kukumbuka maneno ya Bwana Yesu, maneno ambayo yeye mwenyewe alisema: “Ni heri kutoa kuliko kupokea.”
In all things I have set you an example, showing you that, by working as I do, you ought to help the weak, and to bear in mind the words of the Lord Jesus, how He Himself said, "'It is more blessed to give than to receive.'"
36 Baada ya kusema namna hii, alipiga magoti akaomba pamoja nao.
Having spoken thus, Paul knelt down and prayed with them all;
37 Wote wakalia sana na kumwangukia Paulo shingoni na kumbusu.
and with loud lamentation they all threw their arms round his neck, and kissed him lovingly,
38 Walihuzunika zaidi ya yote kwa sababu ya kile ambacho alikuwa amesema, kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Kisha wakamsindikiza merikebuni.
grieved above all things at his having told them that after that day they were no longer to see his face. And they went with him to the ship.

< Matendo 20 >