< Matendo 20 >
1 Baada ya ghasia kumalizika, Paulo aliwaita wanafunzi na kuwatia moyo. Kisha kuwaaga na akaondoka kwenda Makedonia.
After the tumult had ceased, Paul called the disciples to him, and bade them farewell, and departed, in order to go into Macedonia.
2 Naye akiishakupita mikoa hiyo na alikuwa akiwatia moyo waamuni, akaingia Uyunani.
And when he had gone through those regions, and had exhorted them with many words, he came into Greece.
3 Baada ya yeye kuwa pale kwa muda wa miezi mitatu, njama ziliundwa dhidi yake na Wayahudi alipokuwa akikaribia kusafiri kwa njia ya bahari kuelekea Shamu, hivyo aliazimu kurudi kupitia Makedonia.
And having remained there three months, he determined to return through Macedonia, because a plot had been laid for him by the Jews, as he was about to sail to Syria.
4 Walioandamana naye hadi Asia walikuwa Sopatro, mwana wa Pirho kutoka Berea; Aristariko na Sekundo, wote kutoka waamini wa Wathesalonike; Gayo wa Derbe; Timotheo; Tikiko na Trofimo kutoka Asia.
And Sopater of Berea, and Aristarchus and Secundus of Thessalonica, and Gaius of Derbe, and Timothy and Tychicus and Trophimus, who were Asiatics, accompanied him to Asia.
5 Lakini watu hawa wamekwisha tangulia na walikuwa wanatungojea kule Troa.
These went before, and waited for us at Troas.
6 kwa njia ya Bahari kutoka Filipi baada ya siku za mikate isiyotiwa chachu, na katika siku tano tukawafikia huko Troa. Tulikaa huko kwa siku saba.
But we sailed from Philippi, after the days of unleavened bread, and came to them at Troas in five days, where we remained seven days.
7 Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekusanyika pamoja ili kuumega mkate, Paulo alizungumza na Waamini. Alikuwa akipanga kuondoka kesho yake, hivyo akaendelea kuongea hadi usiku wa manane.
And on the first day of the week, when the disciples came together to break bread, Paul discoursed to them, intending to depart on the morrow; and he continued his speech till midnight.
8 Kulikuwa na taa nyingi katika chumba cha juu ambapo tulikuwa tumekusanyika pamoja.
And there were many lamps in the upper room, in which they had met together.
9 Katika dirisha alikuwa amekaa kijana mmoja jina lake Utiko, ambaye alielemewa na usingizi mzito. Hata Paulo alipokuwa akihutubu kwa muda mrefu, kijana huyu, akiwa amelala, akaanguka chini kutoka ghorofa ya tatu na aliokotwa akiwa amekufa.
And a certain young man, named Eutychus, was sitting in the window, overpowered with deep sleep: and, as Paul was discoursing a long time, being oppressed with sleep, he fell from the third story, and was taken up dead.
10 Lakini Paulo alishuka chini, alijinyoosha yeye mwenyewe juu yake, akamkumbatia. Kisha akasema, “Msikate tamaa, kwa kuwa yu hai.”
But Paul went down, and fell upon him, and embracing him, said: Be not troubled, for his life is in him.
11 Kisha akapanda tena ghorofani na akaumega mkate, akala. Baada ya kuzungumza nao kwa muda mrefu hadi alfajiri, akaondoka.
And he went up again, and broke bread, and ate; and having conversed a long time, till daylight, he thus departed.
12 Wakamleta yule kijana akiwa hai wakafarijika sana.
And they brought the young man alive, and were not a little comforted.
13 Sisi wenyewe tulitangulia mbele ya Paul kwa meli na tukaelekea Aso, ambapo sisi tulipanga kumchukua Paul huko. Hiki ndicho yeye mwenyewe alitaka kufanya, kwa sababu alipanga kwenda kupitia nchi kavu.
And we went on before to the ship, and put to sea for Assos, intending to take Paul on board at that place; for he had so directed, intending to go himself on foot.
14 Alipotufikia huko Aso, tukampakia kwenye Meli tukaenda Mitilene.
And when he met us at Assos, we took him on board, and came to Mitylene;
15 Kisha sisi tukatweka kutoka huko na siku ya pili tulifika upande wa pili wa kisiwa cha Kio. Siku iliyofuata, tukawasili kisiwa cha Samo, na kesho yake tukafika mji wa Mileto.
and sailing from that place, we came, on the following day, opposite to Chios; and, on the next day, we arrived at Samos: and after stopping at Trogyllium, we came, on the next day, to Miletus.
16 Kwa sababu Paulo alikuwa ameamua kusafiri kupitia Efeso, ili kwamba asitumie muda wowote katika Asia; kwa maana alikuwa na haraka ya kuwahi Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Pentekoste, kama ingeliwezekana yeye kufanya hivyo.
For Paul had determined to sail past Ephesus, that he might not spend time in Asia; for he hastened, that, if it were possible for him, he might be in Jerusalem on the day of Pentecost.
17 Kutoka Mileto akatuma watu hadi Efeso na akawaita wazee wa Kanisa.
From Miletus he sent to Ephesus, and called the elders of the church.
18 Walipofika kwake, akawaambia, ninyi wenyewe mwajua tangu siku ya kwanza nilipokanyaga hapa Asia, jinsi nilivyokuwa kwenu muda wote.
And when they had come to him, he said to them: You know, from the first day on which I came into Asia, how I have been with you during the whole time,
19 Nimemtumikia Bwana kwa unyenyekevu wote na kwa machozi, na mateso yaliyonipata mimi kwa hila za Wayahudi.
serving the Lord with all lowliness of mind, and with tears, and with trials, which came upon me through the plots of the Jews;
20 Mwajua jinsi ambavyo sikujizuia kutangaza kwenu kitu chochote ambacho kilikuwa muhimu, na jinsi mimi nilivyowafundisha wazi wazi na pia kwenda nyumba kwa nyumba.
and that I have kept back nothing that was profitable, but have preached to you, and taught you both publicly, and from house to house,
21 Mnajua jinsi mimi nilivyoendelea kuwaonya Wayahudi na Wayunani juu ya toba kwa Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.
bearing full testimony both to Jews and to Greeks, of the repentance that leads to God, and of the faith that leads to our Lord Jesus Christ.
22 Na sasa, angalieni, mimi, nikiwa ninamtii Roho Mtakatifu kuelekea Yerusalemu, nisiyajue mambo ambayo yatanitokea mimi huko,
And now, behold, I am going, bound in spirit, to Jerusalem, not knowing what shall befall me there,
23 ila kwa kuwa Roho Mtakatifu hunishuhudia mimi katika kila mji na anasema kwamba minyororo na mateso ndivyo vinavyoningojea.
except that in every city the Holy Spirit testifies to me, saying, That bonds and afflictions await me.
24 Lakini mimi si kufikiria kwamba maisha yangu ni kwa njia yoyote ya thamani kwangu, ili niweze kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu, kuishuhudia injili ya neema ya Mungu.
But I esteem this a matter of no importance, nor do I hold my life dear to myself, so that I may finish my course with joy, and the ministry that I have received from the Lord Jesus, to bear full testimony to the gospel of the grace of God.
25 Na sasa, tazama, najua kwamba wote, miongoni mwa wale nilioenda kuwahubiri Ufalme, hamtaniona uso tena.
And now, behold, I know that you all, among whom I have gone preaching the kingdom of God, will see my face no more.
26 Kwa hiyo nawashuhudia leo hii, kwamba sina hatia kwa damu ya mtu yeyote.
For this reason I solemnly affirm to you this day, that I am clean from the blood of all men.
27 Kwa maana sikujizuia kuwatangazia mapenzi yote ya Mungu.
For I have not shunned to declare to you the whole counsel of God.
28 Kwa hiyo iweni waangalifu juu yenu ninyi wenyewe, na juu ya kundi lolote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi. Iweni waangalifu kulichunga kusanyiko la Bwana, ambalo alilinunua kwa damu yake mwenyewe.
Therefore, take heed to yourselves, and to all the flock over which the Holy Spirit has made you overseers, that you be shepherds to the church of God, which he has purchased with his own blood.
29 Najua kwamba baada ya kuondoka kwangu, mbwa mwitu wakali wataingia kwenu, na wasilihurumie kundi.
For I know this, that, after my departure, rapacious wolves will enter in among you, who will not spare the flock;
30 Najua kwamba hata miongoni mwenu wenyewe baadhi ya watu watakuja na kusema mambo mapotovu, ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao.
and men will arise from among yourselves, speaking perverse things, that they may draw off disciples after them.
31 Kwa hiyo muwe macho. Kumbukeni kwamba kwa miaka mitatu sikuweza kuacha kuwafundisha kila mmoja wenu kwa machozi usiku na mchana.
Therefore watch, remembering that for three years, by day and by night, I ceased not to warn every one of you with tears.
32 Na sasa mimi nawakabidhi kwa Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliowekwa wakfu kwa Mungu.
And now, brethren, I commend you to God, and to the word of his grace; to Him who is able to build you up, and to give you an inheritance among all the sanctified.
33 Sikutamani fedha, dhahabu, au mavazi.
I have coveted no man’s silver, or gold, or apparel.
34 Mnajua ninyi wenyewe kwamba mikono hii imenipatia mahitaji yangu mwenyewe na mahitaji ya wale waliokuwa pamoja nami.
You yourselves know that these hands have ministered to my necessities, and to those who were with me.
35 Katika mambo yote niliwapa mfano wa jinsi inavyopasa kuwasaidia wanyonge kwa kufanya kazi, na jinsi mnavyopaswa kukumbuka maneno ya Bwana Yesu, maneno ambayo yeye mwenyewe alisema: “Ni heri kutoa kuliko kupokea.”
In all things I have taught you by example, that by thus laboring, you ought to support the weak, and to remember the words of the Lord Jesus; for he himself said, It is more blessed to give, than to receive.
36 Baada ya kusema namna hii, alipiga magoti akaomba pamoja nao.
And when he had thus spoken, he kneeled down and prayed with them all.
37 Wote wakalia sana na kumwangukia Paulo shingoni na kumbusu.
And they all wept much, and fell on Paul’s neck, and kissed him,
38 Walihuzunika zaidi ya yote kwa sababu ya kile ambacho alikuwa amesema, kwamba kamwe hawatauona uso wake tena. Kisha wakamsindikiza merikebuni.
grieving most of all for the word he had spoken, that they would see his face no more. And they conducted him to the ship.