< Matendo 2 >
1 Ilipofika siku ya Pentekoste, wote walikuwa pamoja sehemu moja.
When the day of Pentecost came, they were all meeting together in one place.
2 Ghafla ikatokea muungurumo kutoka mbinguni kama upepo mkali. ukaijaza nyumba yote walimokuwa wameketi.
Suddenly a noise came from heaven like a roaring wind that filled the whole house where they were staying.
3 Hapo zikawatokea ndimi, kama ndimi za moto zimegawanyika, zikawa juu yao kila mmoja wao.
They saw what looked like separate tongue-shaped flames that settled on each of them.
4 Wao wote wakajazwa na Roho Mtakatifu na wakaanza kusema kwa lugha zingine, kama vile Roho alivyowajalia kusema.
All of them were filled with the Holy Spirit and began to speak in different languages as the Spirit gave them the ability to do so.
5 Sasa walikuwapo wayahudi waliokuwa wanaishi Yerusalemu, wacha Mungu, kutoka kila taifa chini ya mbingu.
At that time there were devout Jews from every nation on earth living in Jerusalem.
6 Ngurumo hizi ziliposikiwa, kundi la watu likaja pamoja na wakiwa na wasiwasi kwa sababu kila mtu aliwasikia wakiongea kwa lugha yake mwenyewe.
When they heard this noise, a large crowd of them gathered. They were puzzled because everyone heard their own language being spoken.
7 waliduwaa na kushangazwa, wao walisema, “Kweli, hawa wote wanaoongea siyo Wagalilaya?
They were totally amazed, saying, “Look, these people who are speaking—aren't they all Galileans?
8 Kwa nini sisi tunawasikia, kila mmoja katika lugha tulizozaliwa nazo?
So how is it that we can all hear them speaking in our own mother tongue?
9 Waparthia na Wamedi na Waelamu, na hao waishio Mesopotamia, Uyahudi, na Kapadokia, na katika Ponto na Asia,
Parthians, Medes and Elamites; people from Mesopotamia, Judaea and Cappadocia, Pontus and Asia,
10 katika Frigia, Pamfilia, katika Misri, na sehemu ya Libya hata Kirene, na wageni kutoka Rumi,
Phrygia and Pamphylia; from Egypt and the area of Libya around Cyrene; visitors from Rome, both Jews and converts,
11 Wayahudi na waongofu, Wakrete na Waarabu, tunawasikia wakizungumza katika lugha zetu kuhusu kazi za uweza wa Mungu.”
Cretans and Arabians—we hear them speaking in our own languages about all the great things God has done.”
12 Wote walikuwa wameduwaa na kutatanishwa; walisemezana wao kwa wao, “Hii ina maana gani?”
They were all amazed and confused. “What does this mean?” they asked each other.
13 Lakini wengine walidhihaki wakisema, “Hawa wamejazwa kwa mvinyo mpya.”
But others jeered and said, “They've been drinking too much wine!”
14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti, akawaambia, “Watu wa Yudea na wote mnaoishi hapa Yerusalemu, hili lijulikane kwenu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
Then Peter stood up with the eleven disciples and spoke in a loud voice: “Fellow Jews and everyone living here in Jerusalem: pay attention to me and I'll explain all this to you!
15 Watu hawa hawajalewa kama mnavyodhani, sababu saa hizi ni asubuhi saa tatu.
These men aren't drunk as you presume. It's only nine in the morning!
16 Lakini hili lilikuwa limesemwa kupitia kwa nabii Yoeli:
What's happening is what was predicted by the prophet Joel:
17 Itakuwa katika siku za mwisho; Mungu asema, nitamwaga Roho wangu kwa watu wote. Wana wenu na binti zenu watatoa unabii, vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
God says, ‘In the last days I will pour out my Spirit on everyone. Your sons and daughters will prophesy. Your young men will see visions. Your old men will dream dreams.
18 Vilevile juu ya watumishi wangu na watumishi wangu wa kike katika siku hizo, nitamwaga Roho wangu, nao watatabiri.
I will pour out my Spirit on my servants, both male and female, and they will prophesy.
19 Nitaonesha maajabu juu angani na ishara chini duniani, damu, moto, na mafusho ya moshi.
I will also give you miraculous signs in the heavens above and on the earth below—blood, fire, and swirling smoke!
20 Na jua litabadilishwa kuwa giza na mwezi kuwa damu, kabla haijaja siku kuu na ya ajabu ya Bwana.
The sun will become dark, and the moon will become red like blood before the great and glorious day of the Lord.
21 itakuwa ya kwamba kila mmoja ambaye huliitia jina la Bwana ataokoka.'
But whoever calls on the name of the Lord will be saved.’
22 Watu wa Israeli, sikieni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mwanadamu aliyethibitishwa na Mungu kwenu kwa matendo ya uweza na maajabu, na ishara ambazo Mungu kupitia Yeye katikati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua-
People of Israel, listen to this: Jesus of Nazareth was a man confirmed by God to you by the powerful miracles and signs that God performed through him, right here among you—as you well know.
23 Kwa sababu ya mpango uliokusudiwa tangu mwanzo, na maarifa ya Mungu, alitolewa, na ninyi, kwa mikono ya watu wahalifu, mlimsulibisha na kumuua,
God, knowing beforehand what would happen, followed his plan and resolved to hand him over to you. By means of the hands of wicked men, you killed him by nailing him to a cross.
24 ambaye Mungu alimwinua, akauondoa uchungu wa mauti kwake, kwasababu haikuwezekana kwake kumilikiwa na huo.
But God raised him back to life, freeing him from the burden of death, because death did not have the power to keep him a prisoner.
25 Hivyo Daudi anasema kuhusu yeye, 'Nilimwona Bwana daima mbele ya uso wangu, yeye yuko mkono wangu wa kulia hivyo basi sitasogezwa.
David says of him, ‘I saw the Lord always in front of me. I will not be shaken, for he is right beside me.
26 Kwa hiyo moyo wangu ulikuwa na furaha na ulimi wangu ulifurahishwa. Pia mwili wangu utaishi katika ujasiri.
That's why I'm so happy! That's why my words are full of joy! That's why my body lives in hope!
27 Hutaiacha nafsi yangu iende kuzimu, wala hutaruhusu Mtakatifu wako kuona uozo. (Hadēs )
For you will not abandon me in the grave, nor will you allow your Holy One to experience decay. (Hadēs )
28 Wewe umedhihirisha kwangu njia za uzima; utanifanya nijae furaha mbele ya uso wako.'
You have revealed to me the ways of life. You will fill me with joy with your presence.’
29 Ndugu, ninaweza kuzungumza kwenu kwa ujasiri kuhusu baba yetu Daudi: yeye alikufa na akazikwa, na kaburi lake liko pamoja nasi hata hivi leo.
My brothers and sisters, let me tell you plainly that our ancestor David died and was buried, and his tomb is here with us to this day.
30 Hivyo, alikuwa nabii na alijua kuwa Mungu alishaapa kwa kiapo kwake, kwamba ataweka mmoja katika uzao wake kwenye kiti cha enzi.
But he was a prophet, and knew that God had promised on oath to place one of his descendants on his throne.
31 Aliliona hili mapema, na akasema kuhusu ufufuo wa Kristo, 'wala alikuwa hakuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuoza.' (Hadēs )
David saw what would happen and spoke about the resurrection of Christ—for Christ was not abandoned to the grave nor did he experience decay. (Hadēs )
32 Huyu Yesu - Mungu alimfufua, ambaye sisi wote ni mashahidi.
God has raised this Jesus from the dead, and we're all witnesses of that.
33 Kwa hiyo, akiwa ameinuliwa katika mkono wa kuume wa Mungu, na akiwa amepokea ahadi ya Roho Mtakatifu kutoka kwa Baba, yeye amemimina hii ahadi, ambaye ninyi mnaona na kusikia.
Now he's been exalted to God's right hand, and has received from the Father the Holy Spirit whom he promised, and has poured out what you're seeing and hearing.
34 Kwani Daudi hakupaa kwenda mbinguni, lakini anasema, 'BWANA alisema kwa Bwana wangu,
For David didn't ascend into heaven, but he did say: the Lord told my Lord, ‘Sit down here at my right hand
35 “keti mkono wangu wa kulia, mpaka nitakapowafanya adui zako kigoda kwa ajili ya miguu yako.
until I have made your enemies a stool to put your feet on.’
36 Kwa hiyo nyumba yote ya Israeli na ijue kwa hakika kwamba Mungu amemfanya Yeye kuwa Bwana na Kristo, huyu Yesu ambaye mlimsulibisha.”
Now let everyone in Israel be totally convinced of this: God has made this Jesus, who you killed on a cross, both Lord and Messiah!”
37 Sasa waliposikia hivyo, wakachomwa katika mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, “Ndugu, tufanyeje?”
When the people heard this they were conscience-stricken. They asked Peter and the other apostles, “Brothers, what should we do?”
38 Na Petro akawaambia, “Tubuni na Mbatizwe, kila mmoja wenu, katika jina la Yesu Kristo kwa ajili ya msamaha wa dhambi zenu, na mtapokea zawadi ya Roho Mtakatifu.
“Repent!” Peter told them. “All of you must be baptized in the name of Jesus Christ for the forgiveness of your sins, and you will receive the gift of the Holy Spirit.
39 Kwani kwenu ni ahadi na kwa watoto wenu na kwa wale wote walioko mbali, watu wengi kwa kadri Bwana Mungu wetu atakavyowaita.”
This promise is given to you, to your children, and to all who are far away—everyone the Lord our God calls.”
40 Kwa maneno mengi alishuhudia na kuwasihi; alisema, “Jiokoeni mtoke katika kizazi hiki kiovu.”
Peter went on speaking, giving them much more evidence. He warned them, “Save yourselves from this perverted generation.”
41 Ndipo wakayapokea maneno yake na wakabatizwa, hapo wakaongezeka katika siku hiyo kama nafsi elfu tatu.
Those who accepted what he'd said were baptized, adding about three thousand people to the group of believers that day.
42 Wakaendelea katika mafundisho ya mitume na ushirikiano, katika kuumega mkate na katika maombi.
They committed themselves to what the apostles had taught them, and to the fellowship of the believers, “breaking bread” and praying together.
43 Hofu ikaja juu ya kila nafsi, na maajabu mengi na ishara zikafanyika kupitia mitume.
Everyone was in awe, and many miracles and signs were done through the apostles.
44 Wote walioamini walikuwa pamoja na kuwa na vitu vyao kwa pamoja,
All the believers were together and shared everything they had.
45 na waliuza vitu na milki zao na kugawanya kwa wote kulingana na hitaji la kila mmoja.
They sold their property and belongings, sharing the proceeds with everyone as they needed.
46 Hivyo siku baada ya siku waliendelea wakiwa na lengo moja katika hekalu, na walimega mkate kwenye kaya, na walishiriki chakula kwa furaha na unyenyekevu wa moyo;
Day after day they continued to meet together in the Temple, and ate together in their homes. They enjoyed their meals humbly and happily. They praised God, and everyone thought favorably of them.
47 walimsifu Mungu na wakiwa na kibali na watu wote. Bwana aliwaongeza siku kwa siku ambao walikuwa wakiokolewa.
Every day the Lord added to their number those who were being saved.