< Matendo 18 >
1 Baada ya mambo hayo, Paulo aliondoka Athene kwenda Korintho.
Après cela, Paul partit d'Athènes et vint à Corinthe.
2 Huko akampata Myahudi aitwaye Akwila mtu wa kabila la Ponto, yeye na mke wake aitwaye Prisila walikuja kutoka huko Italia, kwa sababu Klaudia aliamuru Wayahudi wote waondoke Roma; Paulo akaja kwao;
Il y trouva un Juif nommé Aquilas, originaire du Pont, et récemment arrivé d'Italie avec sa femme Priscille, chassé de Rome comme tous les Juifs par un édit de Claude. Il se réunit à eux
3 Paulo akaishi na kufanya kazi nao kwani yeye anafanya kazi inayofanana na yao. Wao walikuwa ni watengeneza mahema.
et comme ils étaient du même métier que lui, il demeura chez eux pour y travailler. Ils étaient, de leur état, fabricants de tentes.
4 Paulo akajadiliana nao katika sinagogi kila siku ya Sabato. Aliwashawishi Wayahudi pamoja na Wagiriki.
Chaque sabbat il parlait à la synagogue, et il gagnait des Juifs et des Grecs.
5 Lakini Sila na Timotheo walipokuja kutoka Makedonia, Paulo alisukumwa na Roho kuwashuhudia Wayahudi kuwa Yesu ndiye Kristo.
Quand Silas et Timothée arrivèrent de Macédoine, Paul se consacrait uniquement à la prédication, affirmant aux Juifs que Jésus était le Christ.
6 Wakati Wayahudi walipompinga na kumdhihaki, hivyo Paulo akakung'uta vazi lake mbele yao, na kuwaambia, “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe; Mimi sina hatia. Kutoka sasa na kuendelea, nawaendea Mataifa”.
Mais ceux-ci s'opposaient à lui et l'insultaient; alors, secouant sur eux la poussière de ses vêtements, il leur dit: «Que votre sang retombe sur votre tête! J'en suis innocent et désormais je m'adresserai aux païens.»
7 Hivyo akaondoka kutoka pale akaenda kwenye nyumba ya Tito Yusto, Mtu anayemwabudu Mungu. Nyumba yake iko karibu na sinagogi.
Il sortit de la salle et se rendit chez un certain Titius Justus, homme «craignant Dieu», dont la maison était contiguë à la synagogue.
8 Krispo, kiongozi wa sinagogi pamoja na watu wa nyumbani mwake wakamwamini Bwana. Watu wengi wa Korintho waliomsikia Paulo akiongea waliamini na kubatizwa.
Crispus, le chef de la synagogue, crut au Seigneur avec toute sa maison, et plusieurs des Corinthiens qui entendaient Paul devenaient croyants et se faisaient baptiser.
9 Bwana akamwambia Paulo usiku kwa njia ya maono, “Usiogope, lakini ongea na usinyamaze.
Une nuit, le Seigneur dit à Paul dans une vision: «Sois sans crainte, parle au contraire, ne cesse de parler, car je suis avec toi;
10 Kwani Mimi niko pamoja nawe, na hakuna atakayejaribu kukudhuru, maana nina watu wengi katika mji huu”.
personne ne mettra la main sur toi pour te faire du mal, parce que j'ai un grand peuple dans cette ville.»
11 Paulo akakaa huko kwa muda wa mwaka mmoja na miezi sita akifundisha neno la Mungu miongoni mwao.
Paul alors s'établit à Corinthe pendant un an et demi, et il y prêcha la parole de Dieu.
12 Lakini Galio alipofanywa mtawala wa Akaya, Wayahudi walisimama pamoja kinyume na Paulo na kumpeleka mbele ya kiti cha hukumu,
Pendant le proconsulat de Gallion en Achaïe, les Juifs, tous d'accord, se soulevèrent contre Paul et l'amenèrent devant le tribunal:
13 wakisema, “Mtu huyu huwashawishi watu wamwabudu Mungu kinyume cha sheria”.
«Cet homme, dirent-ils, excite les gens à rendre à Dieu un culte contraire à la Loi.»
14 Wakati Paulo alipokuwa akitaka kusema, Galio akawaambia Wayahudi, “Ninyi Wayahudi, kama ingelikuwa ni kosa au uhalifu, ingekuwa halali kuwashughulikia.
Paul ouvrait la bouche pour répondre, quand Gallion, s'adressant aux Juifs: «S'il s'agissait de quelque crime ou de quelque méfait, leur dit-il, j'accueillerais vos plaintes comme il convient, ô Juifs!
15 Lakini kwa sababu ni maswali, yanayohusu maneno na majina, na sheria zenu, basi hukumuni ninyi wenyewe. Mimi sitamani kuwa hakimu kwa habari ya mambo hayo.”
mais s'il s'agit de vos discussions sur une doctrine, sur des noms propres, sur votre Loi particulière, regardez-y vous-mêmes; je ne veux pas juger ces questions-là.»
16 Galio akawaamuru waondoke mbele ya kiti cha hukumu,
Et il les renvoya du tribunal.
17 Hivyo, wakamkamata Sosthene, kiongozi wa sinagogi, wakampiga mbele ya kiti cha hukumu. Lakini Galio hakujali walichokifanya.
Tout le monde alors tomba sur Sosthènes, le chef de la synagogue, et l'on se mit à le battre devant le tribunal. Gallion ne s'en soucia nullement.
18 Paulo, baada ya kukaa pale kwa muda mrefu, aliwaacha ndugu na kwenda kwa meli Siria pamoja na Prisila na Akwila. Kabla ya kuondoka bandarini, alinyoa nywele zake kwani alikuwa ameapa kuwa Mnadhiri.
Paul resta encore longtemps à Corinthe; puis il prit congé des frères et s'embarqua pour la Syrie avec Priscille et Aquilas, après s'être fait raser la tête à Kenchrées; car il avait fait un voeu.
19 Walipofika Efeso, Paulo alimwacha Prisila na Akwila pale, lakini yeye mwenyewe akaingia kwenye sinagogi na kujadiliana na Wayahudi.
On débarqua à Éphèse; Paul y laissa ses compagnons et se rendit à la synagogue, où il s'entretint avec les Juifs.
20 Walipomwambia Paulo akae nao kwa muda mrefu, yeye alikataa.
Mais quand ils lui demandèrent de prolonger son séjour, il n'y consentit pas
21 Lakini akaondoka kwao, akawaambia, “Nitarudi tena kwenu, ikiwa ni mapenzi ya Mungu”. Baada ya hapo, akaondoka kwa meli kutoka Efeso.
et leur dit en prenant congé d'eux: «Je reviendrai une autre fois chez vous, s'il plaît à Dieu.» Il partit d'Éphèse,
22 Paulo alipotua Kaisaria, alipanda kwenda kusalimia Kanisa la Yerusalemu, kisha akashuka chini kwa kanisa la Antiokia.
débarqua à Césarée et, après être monté à Jérusalem pour saluer l'Église, il descendit à Antioche.
23 Baada ya kukaa kwa muda pale, Paulo aliondoka kupitia maeneo ya Galatia na Frigia na kuwatia moyo wanafunzi wote.
Il en repartit après un court séjour et traversa successivement le pays des Galates et la Phrygie pour fortifier tous les disciples.
24 Myahudi mmoja aitwaye Apolo, aliyezaliwa huko Alexandria, alikuja Efeso. Alikuwa na ufasaha katika kuongea na hodari katika Maandiko.
Cependant un certain Juif, du nom d'Apollos, né à Alexandrie, un homme éloquent, arriva à Éphèse;
25 Apollo alikuwa ameelekezwa katika mafundisho ya Bwana. Kwa jinsi alivyokuwa na bidii katika roho, aliongea na kufundisha kwa usahihi mambo yanayomuhusu Yesu, ila alijua tu ubatizo wa Yohana.
il connaissait à fond les Écritures. On l'avait instruit dans la doctrine du Seigneur; c'était une âme ardente qui prêchait et enseignait avec soin ce qui concerne Jésus, bien qu'il ne connût que le baptême de Jean.
26 Apolo akaanza kuzungumza kwa ujasiri katika hekalu. Lakini Prisila na Akwila walipomsikia, walifanya urafiki naye na wakamwelezea juu ya njia za Mungu kwa usahihi.
Quand il commença à parler librement dans la synagogue, Priscilla et Aquilas qui l'entendirent l'emmenèrent avec eux et lui exposèrent plus exactement la doctrine de Dieu.
27 Alipotamani kuondoka kwenda Akaya, ndugu walimtia moyo na kuwaandikia barua wanafunzi walioko Akaya ili wapate kumpokea. Alipowasili, kwa neema aliwasaidia sana wale waliomini.
Lorsqu'il se proposa de passer en Achaïe, les frères l'y encouragèrent et écrivirent aux disciples de lui faire bon accueil. Une fois arrivé, il se rendit, par la grâce de Dieu, très utile aux croyants;
28 Kwa nguvu zake na maarifa, Apolo aliwazidi Wayahudi hadharani akionesha kupitia maandiko ya kuwa Yesu ndiye Kristo.
car il réfutait vigoureusement les Juifs en public, leur démontrant par les Écritures que Jésus est le Christ.