< Matendo 16 >
1 Paulo pia alipokuja Derbe na Lystra; na tazama, pale palikuwepo na mwanafunzi aitwaye Timotheo, ni Kijana aliyezaliwa na mama wa Kiyahudi ambaye ni muumini na baba yake ni Mgiriki.
Paul [and Silas] to Derbe [city and visited the believers there]. Next [they went to] Lystra [city]. A believer whose name was Timothy lived there. His mother was a Jewish believer, but his father was a Greek.
2 Watu wa Listra na Ikonia walimshudia vizuri.
The believers in Lystra and Iconium said good things about Timothy,
3 Paulo alimtaka ili asafiri naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwako huko kwani wote walimjua kuwa baba yake ni Mgiriki.
and Paul wanted to take Timothy with him [when he went] to other places, so he circumcised Timothy. [He did that so that] the Jews who lived in those places [would accept Timothy], because they knew that his non-Jewish father [had not allowed him to be circumcised] {[anyone to circumcise his son]}.
4 Walipokuwa wakienda walipita kwenye miji na kutoa maagizo kwa makanisa ili kuyatii maagizo hayo yaliandikwa na mitume na wazee huko Yerusalemu.
[So Timothy went with Paul and Silas] and they traveled to many other towns. [In each town] they told [the] believers the rules that had been decided by the apostles and elders in Jerusalem {that the apostles and elders in Jerusalem had decided} that [non-Jewish] believers should obey.
5 Hivyo makanisa yakaimarishwa katika imani na walioamini wakaongezeka kwa idadi kila siku.
[God was helping] the believers in those towns to trust more strongly [in the Lord Jesus], and every day more people became believers.
6 Paulo na mwenzake wakaenda Firigia na Galatia, kwani Roho wa Mungu aliwakataza kuhubiri neno huko kwenye jimbo la Asia.
Paul and his companions wanted/planned to enter Asia [province] preach the message [about Jesus] there, but they were prevented by the Holy Spirit {the Holy Spirit prevented them} [from going there. So] they traveled through Phrygia and Galatia [provinces].
7 Walipokaribia Misia, walijaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu akawakataza.
They arrived at the border of Mysia [province] and they wanted to go [north] Bithynia [province]. But [again] the Spirit of Jesus showed them that they should not [go there].
8 Kwa hiyo wakapita Misia wakaja mpaka Mji wa Troa.
So they went through Mysia [province] and arrived at Troas, a [port city. I, Luke, joined them there].
9 Maono yalimtokea Paulo usiku, kulikuwa na mtu wa Makedonia amesimama, akimwita na kusema “Njoni mtusaidie huku Makedonia”.
That night [God gave] Paul a vision in which he saw a man [who was a native] of Macedonia [province]. He was standing [some distance away], and he was earnestly calling to Paul, “[Please] come over [here] to Macedonia and help us!”
10 Paulo alipoona maono, mara tukajiandaa kwenda Makedonia, akijua kwamba Mungu alituita kwenda kuwahubiria injili.
[The next morning] we [(exc)] immediately got ready to go to Macedonia, because we believed that God had called us to [go and] preach the good message to the people there.
11 Hivyo tukaondoka kutoka Troa, tukaenda moja kwa moja Samothrake, na siku iliyofuata tukafika mji wa Neapoli.
So we [(exc)] got on a ship in Troas and sailed across [the sea] Samothrace [Island. We spent the night there], and the next day [we sailed again across the sea and arrived] at Neapolis [port/town].
12 Kutoka hapo tukaenda Filipi ambao ni moja ya mji wa Makedonia, mji muhimu katika wilaya na utawala wa Kirumi na tukakaa siku kadhaa.
Then we [left Neapolis and] went [by land] to Philippi. It was a very important city in Macedonia [province, where many] Roman citizens lived. We stayed in Philippi several days.
13 Siku ya Sabato, tulikwenda nje ya lango kwa njia ya mto, sehemu ambayo tulidhania kutakuwa na mahali pa kufanyia maombi. Tulikaa chini na kuongea na akinamama waliokuja pamoja.
On the first (Sabbath/Jewish day of rest) [after we(exc) arrived], we went outside the city gate [down] to the river. We had heard [someone say] that [Jewish] people gathered to pray there. [When we arrived there, we saw] some women who had gathered [to pray]. So we sat down and began to tell them [the message about Jesus].
14 Mwanamke mmoja aitwaye Lidia, muuzaji wa zambarau, kutoka katika mji wa Tiatira, mwenye kumwabudu Mungu, alitusikiliza. Bwana alimfungua moyo wake na kuweka maanani maneno yaliyosemwa na Paulo.
A woman whose name was Lydia was one of those who were listening [to Paul. She was a non-Jewish woman], from Thyatira [city, who bought and] sold [expensive] purple cloth. She had accepted what the Jews believe about God. The Lord [God] caused her to pay attention to the message that Paul preached, and she believed it. [The members of her household also heard the good message and believed in Jesus] [MTY].
15 Baada ya kubatizwa, yeye na nyumba yake yote, alitusihi akisema “kama mmeniona kuwa mimi ni mwaminifu katika Bwana, basi nawasihi muingie na kukaa kwangu”. Akatusihi sana.
After [Paul and Silas] baptized Lydia and the others who lived in her house [MTY] {After Lydia and the others who lived in her house were baptized}, she invited us to [go and stay in] her home. She said, “You [(pl)] know that I [now] believe in the Lord [Jesus], so [please] come and stay in my house.” She persuaded us [to do that, so we(exc) stayed there].
16 Ikawa kwamba, tulipokuwa tunaenda mahali pa kuomba, msichana mmoja aliyekuwa na pepo la utambuzi akakutana nasi. Alimletea bwana wake faida nyingi kwa kubashiri.
Another day, while we [(exc)] were going to the place where people regularly gathered to pray, we met a young woman who was a slave. An evil spirit was enabling her to be a ventriloquist and to tell people what would happen [to them]. People paid a lot of money to [the men who were] her owners, in return for her telling them things that [she said] would happen [to them].
17 Mwanamke huyu alimfuata Paulo pamoja na sisi, akipiga kelele na kusema “Hawa wanaume ni watumishi wa Mungu aliye Mkuu, wanaowatangazia ninyi habari ya wokovu”.
This young woman followed Paul and the rest of us. She continually shouted, “These men serve the God who is the greatest [of all gods]! They are telling you how ([God] can save you [so that he will not punish you/to be] saved)”
18 Alifanya hivyo kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa amekasirishwa na tendo hilo, aligeuka nyuma na kumwambia pepo, “Nakuamuru kwa Jina la Yesu umtoke ndani yake.” Naye akatoka na kumwacha mara moja.
She continued to do that for many days. Finally Paul became irritated. So he turned [toward the young woman] and rebuked the evil spirit [that was in her. He said], “By the authority [MTY] of Jesus Christ, I command you [(sg)] to come out of this young woman!” Right away the evil spirit left her.
19 Mabwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limeondoka, waliwakamata Paulo na Sila na kuwaburuza sokoni mbele ya wenye mamlaka.
And then her owners realized that she could no longer earn money for them [because she could no longer predict what would happen to people, so they were angry]. They grabbed Paul and Silas and forcefully took them to the public square, to [the place where] the government authorities and [a lot of other people were gathered].
20 Walipowafikisha kwa mahakimu, walisema, “Hawa wanaume ni Wayahudi na wanasababisha ghasia kubwa katika mji wetu.
The owners [of the young woman] brought Paul and Silas to the city officials and told them, “These men are Jews, and they are greatly troubling [the people in] [MTY] our city.
21 Wanafundisha mambo ambayo siyo sheria sisi kuyapokea wala kuyafuata kama Warumi.”
They are teaching that we [(inc)] should follow customs that our laws do not allow us Romans to consider [to be correct] or to obey!”
22 Umati ukawainukia kinyume Paulo na Sila, mahakimu wakararua nguo zao na kuwavua na kuamuru wachapwe viboko
Many of the crowd joined [those who were accusing] Paul and Silas, and started beating them. Then the [Roman] authorities commanded [soldiers] to tear the shirts off Paul and Silas and to beat them [with rods/sticks].
23 Baada ya kuwachapa viboko vingi, waliwatupa gerezani na kumuamuru askari wa gereza kuwalinda vyema.
[So the soldiers] beat Paul and Silas vigorously [with rods]. After that, they [took them and] shoved them into the prison. They told the jailer that he should lock them up securely.
24 Baada ya kupokea amri hiyo, askari wa gereza aliwatupa katika chumba cha ndani ya gereza na kuwafunga miguu yao kwenye sehemu alipowahifadhi.
[Because the officials] had [commanded] him [to do that], the jailer shoved Paul and Silas into the cell that was farthest inside. [There, he made them sit down on the floor/ground and stretch out their legs]. Then he fastened their ankles in [grooves] between two large wooden beams, [so that Paul and Silas could not move their legs].
25 Wakati wa usiku wa manane, Paulo na Sila wakawa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwasikiliza,
About midnight, Paul and Silas were praying [aloud] and praising God by singing hymns. The [other] prisoners were listening attentively to them.
26 Ghafla kukatokea tetemeko kuu na misingi ya gereza ikatikiswa, milango ya gereza ikafunguka, na minyororo ya wafungwa wote ikalegezwa.
Suddenly there was a very strong earthquake. It shook the entire jail [SYN] and its foundation [SYN]. [The earthquake caused] all the doors [of the jail] to open suddenly, and [caused] all the chains that fastened the prisoners to fall off.
27 Mlinzi wa Gereza aliamka kutoka usingizini na akaona milango yote ya gereza imefunguliwa; hivyo akachukua upanga wake maana alitaka kujiua kwa sababu alifikiri wafungwa wote walikwishatoroka,
The jailer woke up and saw that the doors of the jail were open. He thought that the prisoners had escaped. So he pulled out his sword in order to kill himself, [because he knew that the officials would kill him if the prisoners escaped].
28 Lakini, Paulo akapiga kelele kwa sauti kuu, akisema “usijidhuru kwa sababu wote tuko mahali hapa”.
Paul [saw the jailer and] shouted to him, “Do not harm yourself! We [(exc) prisoners] are all here!”
29 Mlinzi wa gereza aliomba taa ziletwe na akaingia ndani ya gereza kwa haraka, akitetemeka na kuogopa, akawaangukia Paulo na Sila,
The jailer shouted [to someone] to bring torches/lanterns, [and after they brought them], he rushed into the jail and knelt down in front of Paul and Silas. [He was very afraid, so] much so that he was trembling/shaking.
30 na kuwatoa nje ya gereza na kusema, “Waheshimiwa, nifanye nini ili nipate kuokoka?”
Then he brought Paul and Silas out [of the jail] and asked: “Sirs, what do I need to do to be saved [from being punished for my sins]?”
31 Nao wakamwambia, “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.”
[They answered], “Trust in [what] the Lord Jesus [has done for you], and you will be saved {[God] will save you}, and the others who live in [MTY] your house will [also] be saved [if they believe in Jesus].”
32 Walinena neno la Bwana kwake, pamoja na watu wote wa nyumbani kwake,
Then the jailer took Paul and Silas into his house, washed their wounds, and gave them a meal. [He woke up all the people in his house, and] Paul and Silas told all of them the message about the Lord [Jesus. They all believed in him]. Immediately [after that, the jailer and all his family were baptized] {[Paul and Silas] baptized the jailer and all his family}. They were very happy, because now they all believed in God.
33 Mlinzi wa gereza aliwachukua usiku ule na kuwaosha sehemu walizoumia, yeye pamoja na watu wa nyumbani mwake wakabatizwa mara.
34 Akawaleta Paulo na Sila nyumbani kwake na kuwatengea chakula. Naye akawa na furaha kuu pamoja na watu wa nyumbani mwake kwa sababu walimwamini Mungu.
35 Ilipokuwa mchana, mahakimu walituma ujumbe kwa yule mlinzi wa gereza wakisema, “Waruhusu wale watu waende”,
The next morning, the [Roman] officials commanded [some] police officers [to go to the jail to say to the jailer], “[Our bosses] say, ‘Let those [two] prisoners go [now]!’”
36 Mlinzi wa gereza akamjulisha Paulo juu ya maneno hayo ya kuwa, “Mahakimu walituma ujumbe niruhusu mwondoke: hivyo tokeni nje na mwende kwa amani.”
[After the officers went and told that to] the jailer, he [went and] told Paul, “The [Roman] authorities have sent a message [(sg)] saying that I should release you [(sg)] and Silas [from prison]. So you [two] can leave [the jail] now. Now you can go peacefully!”
37 Lakini Paulo akawaambia, “Walitupiga hadharani, watu ambao ni Warumi bila kutuhukumu na waliamua kututupa gerezani; halafu sasa wanataka kututoa kwa siri? Hapana, haitawezekana, wao wenyewe waje kututoa mahali hapa”.
But Paul said to the police officers, “The authorities [commanded men to] beat us in front of a crowd before [those authorities] had learned if we [(exc)] had done anything wrong! Then they [ordered men to] shove us into jail! [But that was not legal, because] we [(exc)] are Roman citizens! And now they want [RHQ] to send us away secretly! We will not accept that! Those [Roman] officials must come themselves and [tell us that they are sorry], and take us out [of jail].”
38 Walinzi wakawajulisha mahakimu juu ya maneno hayo, mahakimu wakaogopa sana pale walipojua kuwa Paulo na Sila ni Warumi.
So the police officers [went and] told the city authorities [what Paul had said]. When those authorities heard that Paul and Silas were Roman citizens, they were afraid [that someone would report to more important officials what they had done, and as a result they would be punished] {[those officials would punish them]}.
39 Mahakimu wakaja na kuwasihi watoke, na walipowatoa nje ya gereza, waliwaomba Paulo na Sila watoke nje ya mji wao.
So the city authorities came to Paul and Silas and told them that they were sorry for what they had done to them. The authorities brought them out of the jail, and repeatedly asked them to leave the city [soon].
40 Kwa hiyo Paulo na Sila wakatoka nje ya gereza wakaja nyumbani kwa Lidia. Paulo na Sila walipowaona ndugu, waliwatia moyo na kisha kuondoka katika mji huo.
After Paul and Silas left the jail, they went to Lydia’s house. There they met with her and the [other] believers. They encouraged the believers [to continue trusting in the Lord Jesus], and then the two apostles left [Philippi].