< Matendo 15 >
1 Watu fulani walishuka kutoka Uyahudi na kuwafundisha ndugu, wakisema, “msipotahiriwa kama desturi ya Musa, hamwezi kuokolewa.”
And certain men who came down from Judea, taught the brethren, [and said], Except ye be circumcised after the manner of Moses, ye cannot be saved.
2 Wakati Paulo na Barnaba walipokuwa na mapambano na mjadala pamoja nao, ndugu waliamua kwamba Paulo, Barnaba, na wengine kadhaa waende Yerusalem kwa mitume na wazee kwa ajili ya swali hili.
When therefore Paul and Barnabas had no small dissension and disputation with them, they determined that Paul and Barnabas, and certain others of them, should go to Jerusalem to the apostles and elders about this question.
3 Kwa hiyo, kwa kutumwa kwao na kanisa, walipitia Foinike na Samaria wakitangaza kugeuzwa nia kwa wamataifa. Walileta furaha kuu kwa ndugu wote,
And being brought on their way by the church, they passed through Phenice, and Samaria, declaring the conversion of the Gentiles: and they caused great joy to all the brethren.
4 Walipokuja Yerusalem, walikaribishwa na Kanisa na mitume na wazee, na waliwasilisha taarifa ya mambo yote ambayo Mungu amefanya pamoja nao.
And when they had come to Jerusalem, they were received by the church, and by the apostles and elders, and they declared all things that God had done with them.
5 Lakini watu fulani walioamini, waliokuwa katika kundi la Mafarisayo, walisimama nakusema, “ni muhimu kuwatahiri na kuwaamuru waishike sheria ya Musa.”
But there rose certain of the sect of the Pharisees, who believed, saying, That it was needful to circumcise them, and to command [them] to keep the law of Moses.
6 Hivyo mitume na wazee walisimama pamoja kulifikiria hili swala.
And the apostles and elders came together to consider of this matter.
7 Baada ya majadiliano marefu, Petro alisimama na kusema kwao, “Ndugu mwatambua kwamba kitambo kizuri kilichopita Mungu alifanya chaguo kati yenu, kwamba kwa mdomo wangu Mataifa wasikie neno la injili, na kuamini.
And when there had been much disputing, Peter rose and said to them, Men, brethren, ye know that a good while ago, God made choice among us, that the Gentiles, by my mouth should hear the word of the gospel, and believe.
8 Mungu, anayefahamu mioyo, anashuhudia kwao, anawapa Roho mtakatifu, kama alivyofanya kwetu;
And God, who knoweth the hearts, bore them witness, giving to them the Holy Spirit, even as [he did] to us:
9 na hakutengeneza utofauti kati yetu na wao, akiifanya mioyo yao safi kwa imani.
And put no difference between us and them, purifying their hearts by faith.
10 Kwa hiyo, kwa nini mnamjaribu Mungu kwamba muweke nira juu ya shingo za wanafunzi ambayo hata baba zetu wala sisi hatukuweza kustahimili?
Now therefore why tempt ye God, to put a yoke upon the neck of the disciples, which neither our fathers nor we were able to bear?
11 Lakini twaamini kwamba tutaokolewa kwa neema ya Bwana Yesu, kama walivyokuwa.”
But we believe, that through the grace of the Lord Jesus Christ, we shall be saved even as they.
12 Kusanyiko lote lilinyamaza walipokua wakimsikiliza Barnaba na Paulo walipokuwa wakitoa taarifa ya ishara na maajabu ambayo Mungu alifanya pamoja nao kati ya watu wa mataifa.
Then all the multitude kept silence, and gave audience to Barnabas and Paul, declaring what miracles and wonders God had wrought by them among the Gentiles.
13 Walipoacha kuongea, Yakobo alijibu akisema, “Ndugu nisikilizeni.
And after they held their peace, James answered, saying, Men, brethren, hearken to me.
14 Simoni ameelezea jinsi kwanza Mungu kwa neema aliwasaidia Mataifa ili kwamba ajipatie kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.
Simeon hath declared how God at the first visited the Gentiles to take from among them a people for his name.
15 Maneno ya manabii yanakubaliana na hili kama lilivyoandikwa.
And to this agree the words of the prophets; as it is written,
16 'Baada ya mambo haya nitarudi na kuijenga tena hema ya Daudi, iliyoanguka chini; nitainua na kuhuisha uhararibifu wake,
After this I will return, and will build again the tabernacle of David which is fallen down; and I will build again the ruins of it; and I will set it up:
17 ili kwamba watu waliobaki wamtafute Bwana, pamoja na watu wa Mataifa walioitwa kwa jina langu.'
That the residue of men may seek after the Lord, and all the Gentiles, upon whom my name is called, saith the Lord, who doeth all these things.
18 Hivi ndivyo asemavyo Bwana aliyefanya mambo haya yajulikanayo tangu enzi za zamani. (aiōn )
Known to God are all his works from the beginning of the world. (aiōn )
19 Hivyo basi, ushauri wangu ni, kwamba tusiwapatie shida watu wa Mataifa wamgeukiao Mungu;
Wherefore my sentence is, that we trouble not them, who from among the Gentiles are turned to God:
20 lakini tuandike kwao kwamba wajiepushe mbali na uharibifu wa sanamu, tamaa za uasherati, na vilivyonyongwa, na damu.
But that we write to them that they abstain from pollutions of idols, and [from] lewdness, and [from] things strangled, and [from] blood.
21 Kutoka vizazi vya wazee kuna watu katika kila mji wahubirio na kumsoma Musa katika masinagogi kila Sabato.”
For Moses of old time hath in every city them that preach him, being read in the synagogues every sabbath.
22 Kwa hiyo ikaonekana kuwa imewapendeza mitume na wazee, pamoja na kanisa lote, kumchagua Yuda aliyeitwa Barsaba, na Silas, waliokuwa viongozi wa kanisa, na kuwatuma Antiokia pamoja na Paulo na Barnaba.
Then it pleased the apostles and elders, with the whole church, to send chosen men of their own company to Antioch, with Paul and Barnabas; [namely], Judas surnamed Barsabas, and Silas, chief men among the brethren:
23 Waliandika hivi, “Mitume, wazee na ndugu, kwa ndugu wa Mataifa walioko Antiokia, Shamu na Kilikia, salamu.
And they wrote [letters] by them after this manner; The apostles, and elders, and brethren, [send] greeting to the brethren who are of the Gentiles in Antioch, and Syria, and Cilicia.
24 Tulisika kwamba watu fulani ambao hatukuwapatia amri hiyo, walitoka kwetu na wamewataabisha kwa mafundisho yaletayo shida nafsini mwenu.
Forasmuch as we have heard, that certain who went out from us, have troubled you with words, subverting your souls, saying, [Ye must] be circumcised, and keep the law; to whom we gave no [such] commandment:
25 Kwa hiyo imeonekana vyema kwetu sote kuchagua watu na kuwatuma kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo,
It seemed good to us, being assembled with one accord, to send chosen men to you, with our beloved Barnabas and Paul:
26 watu walio hatarisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana Yesu Kristo.
Men that have hazarded their lives for the name of our Lord Jesus Christ.
27 Kwa hiyo tumemtuma Yuda na Sila, watawaambia mambo yayo hayo.
We have sent therefore Judas and Silas, who will also tell [you] the same things by mouth.
28 Kwa kuwa ilionekana vyema kwa Roho Mtakatifu na kwetu, kutoweka juu yenu mzigo mkubwa kuliko mambo haya yaliyo ya lazima:
For it seemed good to the Holy Spirit, and to us, to lay upon you no greater burden than these necessary things;
29 kwamba mgeuke kutoka kwenye vitu vitolewavyo kwa sanamu, damu, vitu vya kunyongwa, na uasherati. Kama mtajiweka mbali na hivi, itakuwa vyema kwenu. Kwa herini.”
That ye abstain from things offered to idols, and from blood, and from things strangled, and from lewdness: from which if ye keep yourselves, ye will do well. Fare ye well.
30 Hivyo basi, walivyotawanyishwa, waliteremkia Antiokia; baada ya kukusanya kusanyiko pamoja, waliwasilisha barua.
So when they were dismissed, they came to Antioch: and when they had convened the multitude, they delivered the epistle.
31 Walipokua wameisoma, walifurahi kwa sababu ya kutiwa moyo.
[Which] when they had read, they rejoiced for the consolation.
32 Yuda na Sila, na manabii, waliwatia moyo ndugu kwa maneno mengi na kuwatia nguvu.
And Judas and Silas, being prophets also themselves, exhorted the brethren with many words, and confirmed [them].
33 Baada ya kukaa muda fulani huko, walitawanyishwa kwa amani kutoka kwa ndugu kwa wale waliowatuma.
And after they had tarried [there] a time, they were dismissed in peace from the brethren to the apostles.
34 [ Lakini ilionekana vyema Sila kubaki huko ]
Notwithstanding, it pleased Silas to abide there still.
35 Lakini Paulo na wengine walikaa Antiokia pamoja na wengine wengi, ambapo walifundisha na kuhubiri neno la Bwana.
Paul also and Barnabas continued in Antioch, teaching and preaching the word of the Lord, with many others also.
36 Baada ya siku kadhaa Paulo alisema kwa Barnaba, “Na turudi sasa na kuwatembelea ndugu katika kila mji tulipohubiri neno la Bwana, na kuwaona walivyo.
And some days after, Paul said to Barnabas, Let us go again and visit our brethren, in every city where we have preached the word of the Lord, [and see] how they do.
37 Barnaba alihitaji pia kumchukua pamoja nao Yohana aliyeitwa Marko.
And Barnabas determined to take with them John, whose surname was Mark.
38 Lakini Paulo alifikiria haikuwa vizuri kumchukua Marko, aliyewaacha huko Pamfilia na hakuendelea nao katika kazi.
But Paul thought not good to take him with them, who departed from them from Pamphylia, and went not with them to the work.
39 Kisha hapo kukatokea mabishano makubwa kwa hiyo walitengana, na Barnaba alimchukua Marko na kusafiri kwa meli mpaka Kipro,
And the contention was so sharp between them, that they departed, separating one from the other: and so Barnabas took Mark, and sailed to Cyprus.
40 Lakini Paulo alimchagua Sila na kuondoka, baada ya kukabidhiwa na ndugu katika neema ya Bwana.
And Paul chose Silas, and departed, being commended by the brethren to the grace of God.
41 Na alienda kupitia Shamu na Kilikia, akiimarisha makanisa.
And he went through Syria and Cilicia, confirming the churches.