< Matendo 13 >
1 Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
Now there were in the church in Antioch prophets and teachers; Barnabas and Symeon, surnamed "the Black," Lucius of Cyrene, Manaen, the foster-brother of Herod the Tetrarch, and Saul.
2 Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
And as they were worshiping the Lord, and fasting, the Holy Spirit said to them, "Separate me Barnabas and Saul for the work to which I have called them."
3 Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
So after fasting and praying, they laid their hands on them, and let them go.
4 Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
So they, sent forth by the Holy Spirit, went down to Seleucia, and from thence they sailed to Cyprus.
5 Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
And while they were in Salamis, they proclaimed the word of God in the synagogues of the Jews.
6 Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
They had John Mark as an assistant; and after going through the whole island as far as Paphos, they found a certain Jewish sorcerer and false prophet, named Bar-Jesus,
7 Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
who belonged to the suite of the proconsul, Sergius Paulus, an intelligent man. He summoned Barnabas and Saul, and sought to hear the word of God.
8 Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
But Elymas, "the sorcerer," for that is the translation of his name, opposed them, and tried to divert the proconsul from the faith.
9 Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
So Saul, who is also called Paul, filled with the Holy Spirit, gazed steadily at him, and said.
10 na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
"O full of all craft and cunning, you son of the devil! You enemy of all goodness! Will you never stop perverting the right ways of the Lord?
11 Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
"The Lord’s hand is now upon you, and you shall be blind, not seeing the sun for a season." Instantly there fell on him a mist and a darkness, and groping about, he sought some one to lead him by the hand.
12 Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
Then the proconsul, seeing what had happened, believed. He was astounded at the teaching of the Lord.
13 Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
From Paphos Paul and his party set sail for Perga in Pamphylia; but John Mark left them and went back to Jerusalem.
14 Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
Then they themselves, passing through from Perga, came to Antioch in Pisidia. Here they went into the synagogue on the Sabbath Day and sat down.
15 Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
And, after the reading of the Law and the Prophets, the wardens of the synagogue sent word to them. "Brothers," they said, "if you have any word of encouragement to the people, say it."
16 Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
So Paul stood up, and motioning with his hand, said. "Men of Israel, and you who fear God, listen.
17 Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
"The God of this people of Israel chose our forefathers and made this people great, while they sojourned in the land of Egypt. And with an uplifted arm he led them out of it.
18 Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
"For about forty years he bore with them in the desert,
19 Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
"and when he had destroyed seven nations in the land of Canaan, he gave them their land as an inheritance for about four hundred and fifty years.
20 Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
"And afterwards he gave them Judges, until Samuel, the prophet.
21 Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
"Then they asked for a king, and he gave them Saul, the son of Kish, a Benjamite for forty years.
22 Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
After deposing him, he raised up David to be their king, to whom he also bore witness, when he said, "I have found David, the son of Jesse, a man after my own heart, and who will obey all my will.
23 Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
"Of this man’s descendants God has brought unto Israel, according to his promise, a Savior, Jesus;
24 Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
"before whose coming John had already preached a baptism of repentance to all the people of Israel.
25 Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
"And John, when he was finishing his race, repeatedly asked the people. "‘Who do you suppose that I am? I am not He. But behold there comes One after me, whose sandal I am not worthy to unfasten.’
26 Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
"Brothers, sons of Abraham’s race, and all among you who reverence God, to us has the word of this salvation been sent.
27 Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
"For those who dwell in Jerusalem, and their rulers, because they knew him not, nor the utterances of the prophets which are read every Sabbath, fulfilled them by condemning him.
28 Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
"Though they found no cause of death in him, yet they asked Pilate to put him to death.
29 Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
"And when they had fulfilled everything which had been written concerning him, they took him down from the tree and laid him in a tomb.
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
"But God raised him from the dead.
31 Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
"For many days he was seen by those that came up with him from Galilee to Jerusalem, and are now his witnesses to the people.
32 Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
"And we bring you glad tidings of the promise made to our forefathers,
33 Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
"how that God fulfilled it for us their children in raising up Jesus; as it is also written in the second Psalm, "Thou art my son, today have I become thy Father.
34 Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
"And as to his having raised him from among the dead, now no more to return to corruption, he has said this, "I will give thee the holy and sure blessings of David.
35 Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
"Because in another psalm he says, "Thou wilt not give thy Holy One to see corruption.
36 Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
"For David, after he had served his own generation according to the will of God, fell on sleep, and was gathered to his forefathers, and did see corruption;
37 Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
but he whom God raised up saw no corruption.
38 Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
"Be it known unto you therefore, brothers, that remission of sins is proclaimed to you through this man;
39 Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
"and that by him every one that believes is justified from all things from which you could never be justified by the law of Moses.
40 Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
"Beware, then, lest that spoken of in the prophets come upon you.
41 'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
"Behold, ye despisers, and wonder, and perish, For in your days I will do a deed, A deed which you will never believe, Though one should declare it unto you."
42 Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
As Paul and Barnabas left the synagogue, the people earnestly begged that these words might be repeated to them on the following Sabbath.
43 Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
When the congregation broke up, many of the Jews, and of the devout proselytes, followed Paul and Barnabas, who talked to them, and urged them to continue in the grace of God.
44 Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
On the next Sabbath almost the entire city was gathered together to know the word of God.
45 Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
When they saw the crowds, the Jews were filled with jealousy, and began to contradict Paul’s statements, and to abuse him.
46 Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios )
So Paul and Barnabas spoke out boldly. "It was necessary," they said, "first to proclaim the word of God to you. But since you push it away from you, and judge yourselves unworthy of eternal life, lo, we turn to the Gentiles. (aiōnios )
47 Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
"For such is God’s command to us, saying, "I have set thee for a light to the Gentiles, That thou shouldest be for salvation to the uttermost part of the earth."
48 Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios )
When the Gentiles heard this, they were glad, and glorified the word of the Lord, and all who had been ordained to eternal life, believed. (aiōnios )
49 Neno la Bwana lilienea nchi yote.
So the Lord’s message went far and wide, through the whole district.
50 Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
But the Jews urged on the devout women of high rank, and the leading citizens, and stirred up a persecution against Paul and Barnabas, and drove them out of the district,
51 Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
But they shook off the dust of their feet against them, and came to Iconium.
52 Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.
As for the disciples, they were continually filled with joy, and with the Holy Spirit.