< Matendo 12 >
1 Wakati huo mfalme Herode akanyosha mkono wake kwa baadhi ya wale wanaotoka kwenye kusanyiko ili kuwatesa.
Now, at about that time, Herod the king put forth his hands to ill- treat certain members of the church;
2 Akamwuua Yakobo nduguye Yohana kwa upanga.
and beheaded James, the brother of John, with the sword.
3 Baada ya kuona kuwa inawapendeza Wayahudi, akamkamata na Petro tena. Hii ilikuwa wakati wa mikate isiyochachwa.
And when he saw that it pleased the Jews, he proceeded to seize Peter also. (This was during the days of unleavened bread.)
4 Alipomkamata, akamweka gerezani na akaweka vikosi vinne vya askari ili kumlinda, alikuwa akitarajia kumpeleka kwa watu baada ya Pasaka.
He had him arrested and thrown in prison, and put under guard of sixteen soldiers. He intended, after the Passover, to bring him forth to the people.
5 Petro akawekwa gerezani, lakini maombi yakafanywa kwa bidii na kusanyiko kwa ajili yake kwa Mungu.
So Peter was kept in prison, but earnest prayer to God was made by the church for him.
6 Siku kabla Herode hajaenda kumtoa, Usiku huo Petro alikuwa amelala katikati ya maaskari wawili, akiwa amefungwa na minyororo miwili, na walinzi mbele ya mlango walikuwa wakilinda gereza.
Now when Herod was about to bring him forth, on that very night, while Peter was sleeping between two soldiers, bound with chains, and sentries before the door were guarding the prison,
7 Tazama, malaika wa Bwana ghafla akamtokea na nuru ikang'aa ndani. Akampiga Petro ubavuni na kumwamsha akisema, “Amka haraka.”ndipo minyororo aliyokuwa amefungwa ikafunguka kutoka mikononi mwake.
suddenly an angel of the Lord stood by him, and a light shone in the cell. Striking Peter on the side, he woke him saying, "Rise up quickly." At once the chains dropped from his hands.
8 Malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na vaa viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Malaika akamwambia, “Vaa vazi lako na unifuate.”
"Gird yourself," said the angel, "and put on your sandals." He did so. Then he said unto him, "Throw your cloak about you, and follow me."
9 Hivyo Petro akamfuata Malaika na akatoka nje. Hakuamini kilichofanywa na malaika kama ni cha kweli. Alidhani anaona maono.
So Peter went out, following him, but did not realize that what the angel was doing was real, but supposed that he was seeing a vision.
10 Baada ya kupita lindo la kwanza na la pili, wakafika kwenye geti la chuma la kuingilia kwenda mjini, likafunguka lenyewe kwa ajili yao. Wakatoka nje wakashuka kwenye mtaa, mara Malaika akamwacha.
And when they had passed the first guard and the second, they came to the iron gate that led to the city. This opened to them of its own accord; and they went out passed on through one street; and suddenly the angel left him.
11 Petro alipojitambua, akasema, “Sasa nimeamini kuwa Bwana alimtuma Malaika wake ili kunitoa katika mikono ya Herode, na kwa matarajio ya watu wote wa uyahudi.”
Peter, coming to himself, said, "Now I know for a certainty that the Lord has sent his angel and released me from the hand of Herod, and from all that the Jewish people were anticipating."
12 Baada ya kujua haya, akaja kwenye nyumba ya Mariamu mama yake Yohana ambaye ni Marko; Wakristo wengi walikusanyika wakiomba.
So, after he had thought things over, he went to the house of Mary, the mother of John, surnamed Mark, where a large number of people were assembled, praying.
13 Alipobisha kwenye mlango wa kizuizi, mtumishi mmoja msichana anayeitwa Roda akaja kufungua.
When he knocked at the door of the gate, a maid servant named Rhoda came to answer.
14 Alipotambua ni sauti ya Petro, kwa furaha akashindwa kuufungua mlango; badala yake, akakimbia ndani ya chumba; na kuwajulisha kuwa Petro amesimama mbele ya Mlango.
And when she recognized Peter’s voice, for very joy she did not open the door, but ran in and told them that Peter was standing in front of the gate.
15 Hivyo, Wakasema kwake, “Wewe ni mwendawazimu” lakini alikazia kuwa ni kweli ni yeye. Wakasema “Huyo ni malaika wake.”
"You are mad," they said. But she confidently insisted that it was so. "It is his angel," they said.
16 Lakini Petro aliendelea kubisha, na walipofungua mlango, wakamwona na wakashangaa sana. Petro akawanyamazisha kwa mkono kimya kimya na akawaambia jinsi Bwana alivyomtoa kutoka Gerezani. akasema,
Meanwhile Peter continued to knock, until at last they opened the door, and were amazed to see that it was really he.
17 “Wajulishe haya mambo Yakobo na ndugu zake.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.
He motioned to them to keep quiet, and told them how the Lord had brought him out of prison. "Tell all this to James," he said, "and to the brothers," and away he went to another place.
18 Kulipokuwa mchana, kukawa na huzuni kubwa kati ya askari, kuhusiana na kilichotokea kwa Petro.
When morning came there was no small stir among the soldiers as to what could possibly have become of Peter.
19 Baada ya Herode kumtafuta na hakumwona akawauliza walinzi na akaamuru wauawe. Akaenda kutoka uyahudi mpaka Kaisaria na kukaa huko.
Then Herod had search made for him, and could not find him. After sharply questioning the guards, he ordered them off to execution. He then went down from Judea to Caesarea, where he stayed for some time.
20 Herode alikuwa na hasira juu ya watu wa Tiro na Sidoni. Wakaenda kwa pamoja kwake. Wakawa na urafiki na Blasto msaidizi wa mfalme, ili awasaidie. Kisha wakaomba amani, kwa sababu nchi yao ilipokea chakula kutoka katika nchi ya mfalme.
Now Herod was violently displeased with the people of Tyre and Sidon. So they came to him, with one accord, and after conciliating Blastus, the royal chamberlain, they begged for peace because their country depended upon the king’s country for its food supply.
21 Siku iliyokusudiwa Herode alivaa mavazi ya kifalme na kukaa kwenye kiti chake cha kifalme, na akawahutubia.
So on the appointed day, Herod put on his royal robes, and after taking his seat upon the throne, began to harangue them.
22 Watu wakapiga kelele, “Hii ni sauti ya mungu wala si sauti ya mwanadamu!”
"The voice of a god, and not of a man," the people kept shouting.
23 Mara ghafla malaika akampiga, kwa sababu alikuwa hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango na akafa
Instantly an angel of the Lord smote him, because he had not given God the glory, and being eaten up by worms, he died.
24 Lakini neno la Mungu likakua na kusambaa.
But the word of God grew and multiplied;
25 Baada ya Barnaba na Sauli kukamilisha huduma yao wakatoka pale wakarejea Yerusalemu, wakamchukua na Yohana ambaye jina la kuzaliwa ni Marko.
and after discharging their mission, Barnabas and Saul returned from Jerusalem, bringing with them John, surnamed Mark.