< Matendo 1 >

1 Kitabu cha zamani nilikiandika, Theofilo, nikisema yote Yesu aliyoanza kufanya na kufundisha,
Le premier livre que j'ai écrit, Théophile, concerne tout ce que Jésus a commencé à faire et à enseigner,
2 mpaka siku ambayo Yeye alipokelewa juu. Hii ilikuwa baada ya kutoa amri kupitia Roho Mtakatifu kwa mitume aliokuwa amewachagua.
jusqu'au jour où il a été reçu, après avoir donné ses ordres par le Saint-Esprit aux apôtres qu'il avait choisis.
3 Baada ya mateso yake, Yeye alionekana kwao akiwa hai pia na vithibitisho vingi vikishuhudia. Kwa siku arobaini alijidhihirisha kwao, na alizungumza kuhusu ufalme wa Mungu.
C'est à eux aussi qu'il s'est montré vivant après avoir souffert, par de nombreuses preuves, en leur apparaissant pendant quarante jours et en leur parlant du royaume de Dieu.
4 Alipokuwa akikutana pamoja nao, aliwaamuru wasiondoke Yerusalemu, lakini wasubiri kwa ajili ya ahadi ya Baba, ambayo, alisema, “Mlisikia kutoka kwangu
Puis, s'étant réuni avec eux, il leur donna cet ordre: Ne partez pas de Jérusalem, mais attendez la promesse du Père, que vous avez entendue de ma part.
5 kwamba Yohana alibatiza kabisa kwa maji, lakini mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku hizi chache.”
En effet, Jean a baptisé dans l'eau, mais vous, dans peu de jours, vous serez baptisés dans l'Esprit Saint. »
6 Na walipokuwa wamekutanika pamoja walimuuliza, “Bwana, hivi huu ndio muda utakaowarudishia Israeli ufalme?”
C'est pourquoi, s'étant réunis, ils lui demandèrent: « Seigneur, est-ce maintenant que tu rétablis le royaume d'Israël? »
7 Yeye akawaambia, “Siyo sawa kwenu kujua wakati au majira ambayo Baba amekusudia kwa mamlaka yake mwenyewe.”
Il leur dit: « Ce n'est pas à vous de connaître les temps et les moments que le Père a fixés de son propre chef.
8 Lakini mtapokea nguvu, wakati Roho Mtakatifu atakapokuja juu yenu, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu kote katika Yerusalemu na Uyahudi yote na Samaria mpaka mwisho wa nchi.”
Mais vous recevrez une puissance, lorsque le Saint-Esprit sera descendu sur vous. Vous serez mes témoins à Jérusalem, dans toute la Judée et la Samarie, et jusqu'aux extrémités de la terre. »
9 Bwana Yesu alipokwisha yasema haya, wakiwa wanatazama juu, Yeye aliinuliwa juu, na wingu likamfunika wasimwone kwa macho yao.
Après avoir dit ces choses, comme ils regardaient, il fut enlevé, et une nuée le déroba à leurs yeux.
10 Wakati wanatazama mbinguni kwa makini akienda, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi meupe.
Comme ils regardaient fixement le ciel pendant qu'il s'en allait, voici, deux hommes en vêtements blancs se tenaient près d'eux.
11 Walisema, “Enyi watu wa Galilaya, kwa nini mnasimama hapa mkitazama mbinguni?” Huyu Yesu aliyepaa juu mbinguni atarudi kwa namna ile ile kama mlivyomuona akienda mbinguni.
Ils dirent aussi: Hommes de Galilée, pourquoi restez-vous là à regarder le ciel? Ce Jésus, qui a été enlevé d'entre vous dans le ciel, reviendra de la même manière que vous l'avez vu aller dans le ciel. »
12 Ndipo wakarudi Yerusalemu kutoka kwenye mlima wa mizeituni, ambao uko karibu na Yerusalemu, mwendo wa siku ya Sabato.
Puis ils retournèrent à Jérusalem, de la montagne appelée oliviers, qui est près de Jérusalem, à une distance d'un jour de sabbat.
13 Walipofika walikwenda ghorofani walikokuwa wakikaa. Nao ni Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Thomaso, Batholomayo, Mathayo, Yakobo Mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda Mwana wa Yakobo.
Après leur arrivée, ils montèrent dans la chambre haute où ils séjournaient, c'est-à-dire Pierre, Jean, Jacques, André, Philippe, Thomas, Barthélemy, Matthieu, Jacques, fils d'Alphée, Simon le Zélote, et Judas, fils de Jacques.
14 Wote waliungana kama mtu mmoja, kwa juhudi walikuwa wakiendelea katika maombi. Pamoja na hao walikuwepo wanawake, Mariamu Mama yake Yesu, na kaka zake.
Tous ceux-là, d'un commun accord, persévéraient dans la prière et la supplication, ainsi que les femmes, Marie, mère de Jésus, et ses frères.
15 Katika siku zile Petro alisimama katikati ya ndugu, kama watu 120, akasema,
En ces jours-là, Pierre se leva au milieu des disciples (dont le nombre était d'environ cent vingt), et dit:
16 Ndugu, ilikuwa lazima kwamba maandiko yatimizwe, ambapo zamani Roho Mtakatifu alisema kwa kinywa cha Daudi kuhusiana na Yuda, ambaye aliwaelekeza wale waliomkamata Yesu.
Frères, il fallait que s'accomplît cette Écriture, que le Saint-Esprit avait déjà annoncée par la bouche de David au sujet de Judas, qui servait de guide à ceux qui avaient pris Jésus.
17 Kwa kuwa yeye alikuwa mmoja wetu na alipokea fungu lake la faida katika hii huduma.”
Car il a été compté parmi nous, et il a reçu sa part dans ce ministère.
18 (Sasa mtu huyu alinunua eneo kwa kile alichokipokea kwa uovu wake na hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.
Or, cet homme s'est procuré un champ avec la récompense de sa méchanceté; et, tombant la tête la première, son corps s'est ouvert et tous ses intestins ont jailli.
19 Wote walioishi Yerusalemu walisikia kuhusu hili, hivyo eneo hilo wakaliita kwa lugha yao “Akeldama” hilo ni “shamba la damu.”)
Tous les habitants de Jérusalem apprirent que, dans leur langue, ce champ était appelé « Akeldama », c'est-à-dire « champ du sang ».
20 “Kwenye kitabu cha Zaburi imeandikwa, 'Ngoja eneo lake liwe hame na isiruhusiwe hata mmoja kuishi pale;' na, 'Ruhusu mtu mwingine achukue nafasi yake ya uongozi.'
Car il est écrit dans le livre des Psaumes, « Que sa demeure devienne déserte. Que personne n'y habite. et, « Laissez un autre prendre son poste.
21 Hiyo ni muhimu, kwa hiyo, mmoja wa wanaume ambao waliambatana nasi wakati Bwana Yesu alipotoka na kuingia kati yetu,
« Parmi les hommes qui nous ont accompagnés pendant tout le temps où le Seigneur Jésus est entré et sorti au milieu de nous,
22 kuanzia kwenye ubatizo wa Yohana mpaka siku ile alipotwaliwa juu, lazima awe shahidi wa ufufuo pamoja nasi.
depuis le baptême de Jean jusqu'au jour où il a été reçu d'entre nous, il faut que l'un d'eux devienne avec nous témoin de sa résurrection. »
23 “Wakaweka mbele wanaume wawili, Yusufu aitwaye Barnaba, ambaye pia aliitwa Yusto na Mathia.
Ils en présentèrent deux: Joseph appelé Barsabbas, qu'on appelait aussi Justus, et Matthias.
24 Wao waliomba wakisema, “Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, hivyo weka wazi yupi kati ya wawili hawa ambaye umemchagua
Ils prièrent et dirent: « Toi, Seigneur, qui connais le cœur de tous les hommes, montre lequel de ces deux-là tu as choisi
25 kuchukua nafasi katika huduma na utume, ambapo Yuda alitenda uovu na kwenda mahali pake.”
pour participer à ce ministère et à cet apostolat dont Judas s'est dépouillé, afin qu'il aille à sa place. »
26 Wakapiga kura kwa ajili yao, na kura ikamwangukia Mathia ambaye alihesabiwa pamoja na wale mitume kumi na moja.
On tira au sort pour eux, et le sort tomba sur Matthias; il fut compté parmi les onze apôtres.

< Matendo 1 >