< Matendo 1 >

1 Kitabu cha zamani nilikiandika, Theofilo, nikisema yote Yesu aliyoanza kufanya na kufundisha,
The former record I made, O Theophilus, of all things that Jesus began both to do and to teach,
2 mpaka siku ambayo Yeye alipokelewa juu. Hii ilikuwa baada ya kutoa amri kupitia Roho Mtakatifu kwa mitume aliokuwa amewachagua.
till the day on which he was taken up, after he had, through the Holy Spirit, given commandments to the apostles whom he had chosen.
3 Baada ya mateso yake, Yeye alionekana kwao akiwa hai pia na vithibitisho vingi vikishuhudia. Kwa siku arobaini alijidhihirisha kwao, na alizungumza kuhusu ufalme wa Mungu.
To whom, after he had suffered, he also showed himself alive, by many indubitable proofs; appearing to them for forty days, and speaking of the things that pertain to the kingdom of God.
4 Alipokuwa akikutana pamoja nao, aliwaamuru wasiondoke Yerusalemu, lakini wasubiri kwa ajili ya ahadi ya Baba, ambayo, alisema, “Mlisikia kutoka kwangu
And calling them together, he commanded them not to depart from Jerusalem, but to wait for the promise of my Father, which, said he, you have heard from me;
5 kwamba Yohana alibatiza kabisa kwa maji, lakini mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu katika siku hizi chache.”
for John indeed immersed in water, but you shall be immersed in the Holy Spirit, not many days hence.
6 Na walipokuwa wamekutanika pamoja walimuuliza, “Bwana, hivi huu ndio muda utakaowarudishia Israeli ufalme?”
Therefore, when they came together, they asked him, saying: Lord, wilt thou at this time restore the kingdom to Israel?
7 Yeye akawaambia, “Siyo sawa kwenu kujua wakati au majira ambayo Baba amekusudia kwa mamlaka yake mwenyewe.”
But he said to them: It is not for you to know times or seasons that the Father has reserved under his own control.
8 Lakini mtapokea nguvu, wakati Roho Mtakatifu atakapokuja juu yenu, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu kote katika Yerusalemu na Uyahudi yote na Samaria mpaka mwisho wa nchi.”
But you shall receive power, after the Holy Spirit has come upon you, and you shall be witnesses for me both in Jerusalem, and in all Judea, and in Samaria, and to the most distant part of the earth.
9 Bwana Yesu alipokwisha yasema haya, wakiwa wanatazama juu, Yeye aliinuliwa juu, na wingu likamfunika wasimwone kwa macho yao.
And when he had spoken these things, while they were looking on him, he was taken up, and a cloud received him out of their sight.
10 Wakati wanatazama mbinguni kwa makini akienda, ghafla, watu wawili walisimama katikati yao wamevaa mavazi meupe.
And while they were looking earnestly toward heaven, as he went up, behold, two men stood by them in white raiment,
11 Walisema, “Enyi watu wa Galilaya, kwa nini mnasimama hapa mkitazama mbinguni?” Huyu Yesu aliyepaa juu mbinguni atarudi kwa namna ile ile kama mlivyomuona akienda mbinguni.
who also said: Men of Galilee, why stand you gazing up into heaven? This Jesus, who has been taken up from you into heaven, shall come in the same manner in which you saw him go into heaven.
12 Ndipo wakarudi Yerusalemu kutoka kwenye mlima wa mizeituni, ambao uko karibu na Yerusalemu, mwendo wa siku ya Sabato.
Then they returned to Jerusalem from the mount called Olivet, which is near Jerusalem, a sabbath-day’s journey.
13 Walipofika walikwenda ghorofani walikokuwa wakikaa. Nao ni Petro, Yohana, Yakobo, Andrea, Filipo, Thomaso, Batholomayo, Mathayo, Yakobo Mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda Mwana wa Yakobo.
And when they had come in, they went up into an upper room, in which dwelt Peter and James, and John and Andrew, Philip and Thomas, Bartholomew and Matthew, James the son of Alphæus, and Simon Zelotes, and Judas the brother of James.
14 Wote waliungana kama mtu mmoja, kwa juhudi walikuwa wakiendelea katika maombi. Pamoja na hao walikuwepo wanawake, Mariamu Mama yake Yesu, na kaka zake.
All these, with one mind, continued in prayer and supplication, with the women, and Mary the mother of Jesus, and with his brothers.
15 Katika siku zile Petro alisimama katikati ya ndugu, kama watu 120, akasema,
And in those days Peter arose in the midst of the disciples, (the number of the names together was about a hundred and twenty, ) and said:
16 Ndugu, ilikuwa lazima kwamba maandiko yatimizwe, ambapo zamani Roho Mtakatifu alisema kwa kinywa cha Daudi kuhusiana na Yuda, ambaye aliwaelekeza wale waliomkamata Yesu.
Brethren, it was necessary for this scripture to be fulfilled, which the Holy Spirit had before spoken by the mouth of David, concerning Judas, who was a guide to those who took Jesus:
17 Kwa kuwa yeye alikuwa mmoja wetu na alipokea fungu lake la faida katika hii huduma.”
for he was numbered with us, and had been appointed to this ministry.
18 (Sasa mtu huyu alinunua eneo kwa kile alichokipokea kwa uovu wake na hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.
Therefore he purchased a field with the reward of his iniquity; and falling headlong, he burst asunder in the midst, and all his bowels gushed out.
19 Wote walioishi Yerusalemu walisikia kuhusu hili, hivyo eneo hilo wakaliita kwa lugha yao “Akeldama” hilo ni “shamba la damu.”)
And it was known to all that dwelt in Jerusalem, so that the field is called, in their own language, Akeldama, that is, The field of blood.
20 “Kwenye kitabu cha Zaburi imeandikwa, 'Ngoja eneo lake liwe hame na isiruhusiwe hata mmoja kuishi pale;' na, 'Ruhusu mtu mwingine achukue nafasi yake ya uongozi.'
For it is written in the book of Psalms, Let his habitation be desolate, and let no one dwell in it, and, His office let another take.
21 Hiyo ni muhimu, kwa hiyo, mmoja wa wanaume ambao waliambatana nasi wakati Bwana Yesu alipotoka na kuingia kati yetu,
Therefore, of these men who have associated with us during the whole time in which the Lord Jesus went in and out among us,
22 kuanzia kwenye ubatizo wa Yohana mpaka siku ile alipotwaliwa juu, lazima awe shahidi wa ufufuo pamoja nasi.
beginning from the immersion of John till the day on which he was taken up from us, must one be appointed as a witness with us of his resurrection.
23 “Wakaweka mbele wanaume wawili, Yusufu aitwaye Barnaba, ambaye pia aliitwa Yusto na Mathia.
And they set apart two, Joseph called Barsabas, who was surnamed Justus, and Matthias;
24 Wao waliomba wakisema, “Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, hivyo weka wazi yupi kati ya wawili hawa ambaye umemchagua
and praying, they said: Thou, Lord, who knowest the hearts of all, make known which of these two thou hast chosen,
25 kuchukua nafasi katika huduma na utume, ambapo Yuda alitenda uovu na kwenda mahali pake.”
that he may be appointed to this ministry and apostleship, from which Judas by transgression fell, that he might go to his own place.
26 Wakapiga kura kwa ajili yao, na kura ikamwangukia Mathia ambaye alihesabiwa pamoja na wale mitume kumi na moja.
And they gave in their lots, and the lot fell on Matthias: and he was numbered with the eleven apostles.

< Matendo 1 >