< 3 Yohana 1 >

1 Mzee, kwa Gayo mpenzi, ninayempenda katika kweli.
L'Ancien à Gaïus le bien-aimé, leque j'aime en vérité.
2 Mpendwa, nakuombea ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema, kama vile roho yako inavyofanikiwa.
Bien-aimé, je souhaite que tu prospères en toutes choses, et que tu sois en santé, comme ton âme est en prospérité.
3 Maana nilifurahi sana wakati nilipoambiwa na ndugu waliokuja na kutoa ushuhuda juu ya kweli yako, kama vile unavyoenenda katika kweli.
Car je me suis fort réjoui quand les frères sont venus, et ont rendu témoignage de ta sincérité, et comment tu marches dans la vérité.
4 Sina furaha kubwa zaidi ya hii, kusikia kwamba watoto wangu wanatembea katika kweli.
Je n'ai point de plus grande joie que celle-ci, [qui est] d'entendre que mes enfants marchent dans la vérité.
5 Mpendwa, unaenenda kwa uaminifu unapowahudumia ndugu na wageni,
Bien-aimé, tu agis fidèlement en tout ce que tu fais envers les frères, et envers les étrangers;
6 ambao wametoa ushuhuda wa upendo wako mbele ya kanisa. Unafanya vizuri kuwasafirisha katika safari zao kwa namna ambayo inampendeza Mungu.
Qui en la présence de l'Eglise ont rendu témoignage de ta charité, et tu feras bien de les accompagner dignement, comme il est séant selon Dieu.
7 Kwa sababu kwa ajili ya Jina, walienda bila kuchukua kitu chochote kutoka kwa watu wa Mataifa.
Car ils sont partis pour son Nom, ne prenant rien des Gentils.
8 Hivyo, tunatakiwa kuwakaribisha watu kama hawa, ili tuwe watenda kazi wenza kwa ajili ya kweli.
Nous devons donc recevoir ceux qui leur ressemblent, afin que nous aidions à la vérité.
9 Nililiandikia kusanyiko jambo fulani, lakini Diotrofe, anayependa kuwa wa kwanza miongoni mwao, hakubaliani na sisi.
J'ai écrit à l'Eglise; mais Diotrèphes, qui aime d'être le premier entre eux, ne nous reçoit point.
10 Hivyo, kama nikija nitayakumbuka matendo yake anayoyafanya, jinsi anavyosema maneno mabaya kinyume nasi. Hajaridhika na matendo haya, yeye mwenyewe hawapokei ndugu. Hata huwakataza wengine ambao wanatamani kuwakaribisha hao ndugu na kuwafukuza watoke kwenye kusanyiko.
C'est pourquoi, si je viens, je représenterai les actions qu'il commet, s'évaporant en mauvais discours contre nous, et n'étant pas content de cela, non seulement il ne reçoit pas les frères, mais il empêche même ceux qui les veulent recevoir, et les chasse de l'Eglise.
11 Mpenzi, usiige kilicho kibaya, bali iga kilicho chema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu; na yeye atendaye mabaya hajamwona Mungu.
Bien-aimé, n'imite point le mal, mais le bien; celui qui fait bien, est de Dieu; mais celui qui fait mal, n'a point vu Dieu.
12 Demetrio ameshuhudiwa na wote na kweli yenyewe. sisi pia ni mashahidi, na unajua kuwa ushahuhuda wetu ni wa kweli.
Tous rendent témoignage à Démétrius, et la vérité même le [lui rend], et nous aussi lui rendons témoignage, et vous savez que notre témoignage est véritable.
13 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa kalamu na wino.
J'avais plusieurs choses à écrire, mais je ne veux point t'écrire avec de l'encre et avec la plume;
14 Bali ninatarajia kukuona hivi karibuni, na tutaongea nawe ana kwa ana. Amani iwe pamoja nawe. Marafiki wanakusalimu. Wasalimu marafiki kila mmoja kwa jina lake.
Mais j'espère de te voir bientôt, et nous parlerons bouche à bouche. Que la paix soit avec toi! les amis te saluent; salue les amis nom par nom.

< 3 Yohana 1 >