< 3 Yohana 1 >

1 Mzee, kwa Gayo mpenzi, ninayempenda katika kweli.
The eldere man to Gayus, most dere brother, whom Y loue in treuthe.
2 Mpendwa, nakuombea ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema, kama vile roho yako inavyofanikiwa.
Most dere brothir, of alle thingis Y make preyer, that thou entre, and fare welefuly, as thi soule doith welefuli.
3 Maana nilifurahi sana wakati nilipoambiwa na ndugu waliokuja na kutoa ushuhuda juu ya kweli yako, kama vile unavyoenenda katika kweli.
Y ioyede greetli, for britheren camen, and baren witnessing to thi treuthe, `as thou walkist in treuthe.
4 Sina furaha kubwa zaidi ya hii, kusikia kwamba watoto wangu wanatembea katika kweli.
Y haue not more grace of these thingis, than that Y here that my sones walke in treuthe.
5 Mpendwa, unaenenda kwa uaminifu unapowahudumia ndugu na wageni,
Most dere brother, thou doist feithfuli, what euer thou worchist in britheren, and that in to pilgrymys,
6 ambao wametoa ushuhuda wa upendo wako mbele ya kanisa. Unafanya vizuri kuwasafirisha katika safari zao kwa namna ambayo inampendeza Mungu.
which yeldiden witnessing to thi charite, in the siyt of the chirche; which thou leddist forth, and doist wel worthili to God.
7 Kwa sababu kwa ajili ya Jina, walienda bila kuchukua kitu chochote kutoka kwa watu wa Mataifa.
For thei wenten forth for his name, and token no thing of hethene men.
8 Hivyo, tunatakiwa kuwakaribisha watu kama hawa, ili tuwe watenda kazi wenza kwa ajili ya kweli.
Therfor we owen to resseyue siche, that we be euen worcheris of treuthe.
9 Nililiandikia kusanyiko jambo fulani, lakini Diotrofe, anayependa kuwa wa kwanza miongoni mwao, hakubaliani na sisi.
I hadde write perauenture to the chirche, but this Diotrepes, that loueth to bere primacie in hem, resseyueth not vs.
10 Hivyo, kama nikija nitayakumbuka matendo yake anayoyafanya, jinsi anavyosema maneno mabaya kinyume nasi. Hajaridhika na matendo haya, yeye mwenyewe hawapokei ndugu. Hata huwakataza wengine ambao wanatamani kuwakaribisha hao ndugu na kuwafukuza watoke kwenye kusanyiko.
For this thing, if Y schal come, Y schal moneste hise werkis, whiche he doith, chidinge ayens vs with yuel wordis. And as if these thingis suffisen not to hym, nether he resseyueth britheren, and forbedith hem that resseyuen, and puttith out of the chirche.
11 Mpenzi, usiige kilicho kibaya, bali iga kilicho chema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu; na yeye atendaye mabaya hajamwona Mungu.
Moost dere brothir, nyle thou sue yuel thing, but that that is good thing. He that doith wel, is of God; he that doith yuel, seeth not God.
12 Demetrio ameshuhudiwa na wote na kweli yenyewe. sisi pia ni mashahidi, na unajua kuwa ushahuhuda wetu ni wa kweli.
Witnessing is yoldun to Demetrie of alle men, and of treuthe it silf; but also we beren witnessing, and thou knowist, that oure witnessing is trewe.
13 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa kalamu na wino.
Y hadde many thingis to wryte to thee, but Y wolde not write to thee bi enke and penne.
14 Bali ninatarajia kukuona hivi karibuni, na tutaongea nawe ana kwa ana. Amani iwe pamoja nawe. Marafiki wanakusalimu. Wasalimu marafiki kila mmoja kwa jina lake.
For Y hope soone to se thee, and we schulen speke mouth to mouth. Pees be to thee. Frendis greten thee wel. Greete thou wel frendis bi name.

< 3 Yohana 1 >