< 3 Yohana 1 >

1 Mzee, kwa Gayo mpenzi, ninayempenda katika kweli.
The elder to the beloved Gaius, whom I love in the truth.
2 Mpendwa, nakuombea ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya njema, kama vile roho yako inavyofanikiwa.
Beloved, I pray that in all respects yoʋ may prosper and be in good health, even as yoʋr soul prospers.
3 Maana nilifurahi sana wakati nilipoambiwa na ndugu waliokuja na kutoa ushuhuda juu ya kweli yako, kama vile unavyoenenda katika kweli.
For I was overjoyed when the brothers came and testified about yoʋr faithfulness to the truth and how yoʋ walk in the truth.
4 Sina furaha kubwa zaidi ya hii, kusikia kwamba watoto wangu wanatembea katika kweli.
I have no greater joy than to hear that my children are walking in the truth.
5 Mpendwa, unaenenda kwa uaminifu unapowahudumia ndugu na wageni,
Beloved, yoʋ are acting faithfully in whatever yoʋ do for the brothers and for those who are strangers to you.
6 ambao wametoa ushuhuda wa upendo wako mbele ya kanisa. Unafanya vizuri kuwasafirisha katika safari zao kwa namna ambayo inampendeza Mungu.
They have testified of yoʋr love before the church, and yoʋ will do well to send them on their way in a manner worthy of God.
7 Kwa sababu kwa ajili ya Jina, walienda bila kuchukua kitu chochote kutoka kwa watu wa Mataifa.
For they went out for the sake of the Name, receiving nothing from the Gentiles.
8 Hivyo, tunatakiwa kuwakaribisha watu kama hawa, ili tuwe watenda kazi wenza kwa ajili ya kweli.
Therefore we ought to receive men like them, so that we may be fellow workers for the truth.
9 Nililiandikia kusanyiko jambo fulani, lakini Diotrofe, anayependa kuwa wa kwanza miongoni mwao, hakubaliani na sisi.
I wrote to the church, but Diotrephes, who loves to put himself first, does not acknowledge us.
10 Hivyo, kama nikija nitayakumbuka matendo yake anayoyafanya, jinsi anavyosema maneno mabaya kinyume nasi. Hajaridhika na matendo haya, yeye mwenyewe hawapokei ndugu. Hata huwakataza wengine ambao wanatamani kuwakaribisha hao ndugu na kuwafukuza watoke kwenye kusanyiko.
So if I come, I will call attention to what he is doing and the evil accusations of nonsense that he is making against us. And he is not satisfied with that! He not only refuses to receive the brothers, but also stops those who want to do so and throws them out of the church.
11 Mpenzi, usiige kilicho kibaya, bali iga kilicho chema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu; na yeye atendaye mabaya hajamwona Mungu.
Beloved, do not imitate what is evil, but what is good. Whoever does good is of God; whoever does evil has not seen God.
12 Demetrio ameshuhudiwa na wote na kweli yenyewe. sisi pia ni mashahidi, na unajua kuwa ushahuhuda wetu ni wa kweli.
Demetrius is well spoken of by everyone—and even by the truth itself. We also speak well of him, and you know that our testimony is true.
13 Ninayo mambo mengi ya kukuandikia, lakini sipendi kukuandikia kwa kalamu na wino.
I have much to write, but I do not want to write to yoʋ with pen and ink.
14 Bali ninatarajia kukuona hivi karibuni, na tutaongea nawe ana kwa ana. Amani iwe pamoja nawe. Marafiki wanakusalimu. Wasalimu marafiki kila mmoja kwa jina lake.
I hope to see yoʋ soon, and we will speak face to face. Peace be with yoʋ. The friends greet yoʋ. Greet the friends by name.

< 3 Yohana 1 >