< 2 Timotheo 4 >

1 Ninakupa agizo hili lenye uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, atakaye wahukumu walio hai na wafu, na kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake:
Declaro solemnemente delante de Dios y de Cristo Jesús, Quien está destinado a juzgar a [los ]vivos y a [los ]muertos en su aparición y en su reino:
2 Hubiri Neno. Uwe tayari kwa wakati ufaao na usiofaa. Waambie watu dhambi zao, kemea, himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho.
Predica la Palabra, está listo a tiempo y fuera de tiempo, convierte el argumento contra el que lo presenta, reprende, exhorta con toda longanimidad y doctrina.
3 Kwa maana wakati utakuja ambao watu hawatachukuliana na mafundisho ya kweli. Badala yake, watajitafutia walimu wa kufundisha kulingana na tamaa zao. kwa njia hii masikio yao yatakuwa yametekenywa.
Habrá tiempo cuando no aceptarán la sana doctrina, sino, al tener una comezón de predicación, se acumularán para sí mismos maestros según sus propios deseos ardientes,
4 Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli, na kugeukia hadithi.
y ciertamente apartarán el oído de la verdad, y serán extraviados a las fábulas.
5 Lakini wewe uwe mwaminifu katika mambo yote, vumilia magumu, fanya kazi ya mwinjilisti; timiza huduma yako.
Pero tú sé sobrio en todo, soporta privaciones, haz obra de evangelista, cumple tu ministerio.
6 Kwa maana mimi tayari nimekwisha kumiminwa. Muda wa kuondoka kwangu umewadia.
Porque yo ya soy ofrecido en libación, y el tiempo de mi partida es inminente.
7 Nimeshindana katika haki, Mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda.
He peleado la buena batalla, acabé la carrera, guardé la fe.
8 Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu, ambayo Bwana, anayehukumu kwa haki, atanipa siku ile. Na siyo kwangu tu bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.
Por lo demás, la corona de justicia me está reservada, la cual el Señor, Juez justo, me dará en aquel día, y no solo a mí, sino también a todos los que tienen en alta estima su aparecimiento.
9 Jitahidi kuja kwagu haraka.
Haz todo esfuerzo para venir pronto a mí,
10 Kwa kuwa Dema ameniacha. Anaupenda ulimwengu wa sasa na amekwenda Thesalonike, Kreseni alikwenda Galatia, na Tito alikwenda Dalmatia. (aiōn g165)
porque Demas, al amar al mundo de ahora, me desamparó y fue a Tesalónica, Crescente, a Galacia y Tito, a Dalmacia. (aiōn g165)
11 Luka tu ndiye yuko pamoja nami. Umchukue Marko uje naye kwani yeye ni muhimu kwangu katika huduma.
Solo Lucas está conmigo. Toma a Marcos y tráelo contigo, porque me es útil para [el] ministerio,
12 Nimemtuma Tikiko Efeso.
pues a Tíquico envié a Éfeso.
13 Lile joho ambalo nililiacha Troa kwa Karpo, utakapokuja lilete, pamoja na vile vitabu hasa vile vya ngozi.
Al venirte, trae el capote que dejé con Carpo en Troas, y los rollos, especialmente los pergaminos.
14 Alekizanda mfua chuma alinitendea maovu mengi. Bwana atamlipa kulingana na matendo yake.
Alejandro el calderero me hizo muchos males. El Señor le pagará según sus obras.
15 Nawe pia jihadhari naye, kwani aliyapinga sana maneno yetu.
Guárdate tú también de él, porque con vehemencia contradijo nuestras enseñanzas.
16 Katika utetezi wangu wa kwanza, hakuna mtu yeyote aliyesimama pamoja nami, badala yake, kila mmoja aliniacha. Mungu asiwahesabie hatia.
En mi primera defensa ninguno se presentó. Todos me abandonaron. No les sea tomado en cuenta.
17 Lakini Bwana alisimama pamoja nami, akanitia nguvu ili kwamba kupitia kwangu, neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia. Niliokolewa katika kinywa cha Simba.
Pero el Señor estuvo presente y me fortaleció para que yo cumpliera la predicación, y que todos los gentiles oyeran. Fui librado de [la] boca del león.
18 Bwana ataniepusha na matendo yote maovu na kuniokoa kwa ajili ya ufalme wake wa mbinguni. Utukufu uwe kwake milele na milele. Amen (aiōn g165)
El Señor me librará de toda obra mala y me preservará para su reino celestial. A Él sea la gloria por los siglos de los siglos. Amén. (aiōn g165)
19 Msalimie Priska, Akila na nyumba ya Onesiforo.
Saluda a Prisca y a Aquila, y a la familia de Onesíforo.
20 Erasto alibaki huko Korintho, lakini Trifimo nilimuacha Mileto akiwa mgonjwa.
Erasto quedó en Corinto. A Trófimo lo dejé en Mileto porque estaba enfermo.
21 Fanya hima uje kabla ya kipindi cha baridi. Eubulo anakusalimu, pia Pude, Lino, Claudia na ndugu wote.
Haz todo esfuerzo por venir antes del invierno. Eubulo te saluda, también Pudente, Lino, Claudia y todos los hermanos.
22 Mungu awe pamoja na roho yako, Neema iwe nawe.
El Señor esté con tu espíritu. La gracia sea con ustedes.

< 2 Timotheo 4 >