< 2 Timotheo 4 >
1 Ninakupa agizo hili lenye uzito mbele za Mungu na Kristo Yesu, atakaye wahukumu walio hai na wafu, na kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake:
I adjure you in the presence of God and of Christ Jesus who is about to judge the living and the dead - by his appearing and his kingdom, I adjure you -
2 Hubiri Neno. Uwe tayari kwa wakati ufaao na usiofaa. Waambie watu dhambi zao, kemea, himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho.
proclaim the message, be urgent in season and out of season; convince, rebuke, encourage, with never-failing patience and teaching.
3 Kwa maana wakati utakuja ambao watu hawatachukuliana na mafundisho ya kweli. Badala yake, watajitafutia walimu wa kufundisha kulingana na tamaa zao. kwa njia hii masikio yao yatakuwa yametekenywa.
For a time will come when they will not listen to wholesome teaching, but wanting to have their ears tickled, they will heap up for themselves teachers upon teachers to satisfy their own fancies.
4 Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli, na kugeukia hadithi.
They will turn away their ears from the truth, and turn aside to myths.
5 Lakini wewe uwe mwaminifu katika mambo yote, vumilia magumu, fanya kazi ya mwinjilisti; timiza huduma yako.
But as for you, be always self-controlled, face hardships, do the work of a missionary, discharge all the duties of your ministry.
6 Kwa maana mimi tayari nimekwisha kumiminwa. Muda wa kuondoka kwangu umewadia.
I for my part am a libation already being poured in sacrifice; and the time of my unmooring is at hand.
7 Nimeshindana katika haki, Mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda.
I have fought in the glorious contest; I have run the race; I have kept the faith.
8 Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu, ambayo Bwana, anayehukumu kwa haki, atanipa siku ile. Na siyo kwangu tu bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.
Henceforth there is laid up for me the garland of righteousness which the Lord, the righteous Judge, will award to me on that Day, and not to me only, but also to all those who have loved his appearing.
9 Jitahidi kuja kwagu haraka.
Do your best to come to me speedily,
10 Kwa kuwa Dema ameniacha. Anaupenda ulimwengu wa sasa na amekwenda Thesalonike, Kreseni alikwenda Galatia, na Tito alikwenda Dalmatia. (aiōn )
for Demas has deserted me for love of this present world, and is gone to Thessalonica; Crescens is gone to Galatia; Titus to Dalmatia. (aiōn )
11 Luka tu ndiye yuko pamoja nami. Umchukue Marko uje naye kwani yeye ni muhimu kwangu katika huduma.
Luke only is with me. Pick up Mark, and bring him with you, for he is useful to me in my ministry.
12 Nimemtuma Tikiko Efeso.
Tychicus I have sent to Ephesus.
13 Lile joho ambalo nililiacha Troa kwa Karpo, utakapokuja lilete, pamoja na vile vitabu hasa vile vya ngozi.
When you come, bring the cloak I left in Troas with Carpus; also my books, but especially my parchments.
14 Alekizanda mfua chuma alinitendea maovu mengi. Bwana atamlipa kulingana na matendo yake.
Alexander, the coppersmith, manifested bitter hostility toward me. The Lord will requite him according to his works.
15 Nawe pia jihadhari naye, kwani aliyapinga sana maneno yetu.
Be also on your guard against him, for he has violently opposed my arguments.
16 Katika utetezi wangu wa kwanza, hakuna mtu yeyote aliyesimama pamoja nami, badala yake, kila mmoja aliniacha. Mungu asiwahesabie hatia.
At the time of my first defense no one stood by me; on the contrary they all deserted me - may it not be laid to their charge!
17 Lakini Bwana alisimama pamoja nami, akanitia nguvu ili kwamba kupitia kwangu, neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia. Niliokolewa katika kinywa cha Simba.
Nevertheless the Lord Jesus stood by me, and strengthened my heart, that through me full proclamation of the gospel might be made, and the Gentiles might hear it; and I was rescued from the lion’s jaws.
18 Bwana ataniepusha na matendo yote maovu na kuniokoa kwa ajili ya ufalme wake wa mbinguni. Utukufu uwe kwake milele na milele. Amen (aiōn )
And the Lord will rescue me from every evil assault, and will preserve me for his heavenly kingdom. To him be the glory forever and ever! Amen! (aiōn )
19 Msalimie Priska, Akila na nyumba ya Onesiforo.
Give my greetings to Prisca and Aquila, and the household of Onesiphorus.
20 Erasto alibaki huko Korintho, lakini Trifimo nilimuacha Mileto akiwa mgonjwa.
Erastus remained at Corinth; Trophimus I left behind me ill at Miletus.
21 Fanya hima uje kabla ya kipindi cha baridi. Eubulo anakusalimu, pia Pude, Lino, Claudia na ndugu wote.
Do try to come before winter. Eubulus greets you, and so do Pudens and Linus and Claudia and all the brotherhood.
22 Mungu awe pamoja na roho yako, Neema iwe nawe.
The Lord Jesus be with your spirit. Grace be with you all.