< 2 Timotheo 2 >

1 Kwa hiyo, wewe mwanangu, utiwe nguvu katika neema iliyondani ya Kristo Yesu.
Do you, therefore, my son, be strong in the grace that is in Christ Jesus;
2 Na mambo uliyoyasikia kwangu miongoni mwa mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu waaminifu ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
and the things which you have heard from me through many witnesses, these do you commit to faithful men, who shall be able to teach others also.
3 Shiriki mateso pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu.
Do you, therefore, suffer evil, as a good soldier of Jesus Christ.
4 Hakuna askari atumikae wakati huo huo akijihusisha na shughuli za kawaida za maisha haya, ili kwamba ampendeze ofisa wake mkuu.
Every one that serves as a soldier keeps himself free from the business of this life, that he may please him that has chosen him to be a soldier.
5 Pia kama mtu akishindana kama mwanariadha, hatapewa taji asiposhindana kwa kufuata kanuni.
And if any one also contend in the public games, he is not crowned, unless he contend according to the laws.
6 Ni Muhimu kwamba mkulima mwenye bidii awe wa kwanza kupokea mgao wa mazao yake.
It is necessary that, the farmer should labor, before he partakes of the fruits.
7 Tafakari kuhusu nisemacho, kwa maana Bwana atakupa uelewa katika mambo yote.
Consider what I say, for I pray that the Lord may give you understanding in all things.
8 Mkumbuke Yesu Kristo, kutoka uzao wa Daudi, ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu. Hii ni kulingana na ujumbe wangu wa Injili,
Remember that Jesus Christ, of the posterity of David, was raised from the dead, according to my gospel;
9 ambao kwa sababu ya huo ninateswa hata kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi kwa minyororo.
in which I suffer evil, as an evil-doer, even to bonds: but the word of God is not bound.
10 Kwa hiyo, navumilia mambo yote kwa ajili ya wale ambao Mungu amekwishawachagua, ili kwamba nao pia waupate wokovu ulio katika Kristo Yesu pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
For this reason I endure all things for the sake of the elect, that they also may obtain the salvation that is in Christ Jesus, with eternal glory. (aiōnios g166)
11 Usemi huu ni wakuaminika: “Ikiwa tumekufa pamoja naye, tutaishi pamoja naye pia,
Assuredly true is the saying: If indeed we have died with him, we shall also live with him;
12 kama tukivumilia, tutatawala pamoja naye pia, kama tukimkana yeye, naye pia atatukana sisi.
if we are patient, we shall also reign with him; if we deny him, he will also deny us;
13 kama hatutakuwa waaminifu, yeye atabaki kuwa mwaminifu, maana hawezi kujikana mwenyewe.”
if we are unfaithful, he remains faithful: he can not deny himself.
14 Endelea kuwakumbusha juu ya mambo haya. Waonye mbele za Mungu waache kubishana kuhusu maneno. Kwa sababu hakuna manufaa katika jambo hili. Kutokana na hili kuna uharibifu kwa wale wanaosikiliza.
Put them in mind of these things, charging them before the Lord that they dispute not about words to no profit, which disputes end in the overthrow of the hearers.
15 Fanya bidii kujionesha kuwa umekubalika kwa Mungu kama mtenda kazi asiye na sababu ya kulaumiwa. Litumie neno la kweli kwa usahihi.
Strive to present yourself to God as approved, a workman that has no cause to be ashamed, rightly setting forth the word of truth.
16 Jiepushe na majadiliano ya kidunia, ambayo huongoza kwa zaidi na zaidi ya uasi.
But shun profane and vain babblings; for they will make further advance to ungodliness,
17 Majadiliano yao yatasambaa kama donda ndugu. Miongoni mwao ni Himenayo na Fileto.
and their word will eat as a gangrene: of whom are Hymenæus and Philetus,
18 Hawa ni watu walioukosa ukweli. Wanasema ya kuwa ufufuo tayari umishatokea. Wanapindua imani ya baadhi ya watu.
who, as it respects the truth, have erred, saying that the resurrection has already taken place; and they overthrow the faith of some.
19 Hata hivyo, msingi imara wa Mungu unasimama, wenye uandishi huu, “Bwana anawajua walio wake, na kila alitajaye jina la Bwana ni lazima ajitenge na udhalimu.”
But the foundation of God stands firm, having this inscription: The Lord knows those who are his; and, Let every one that names the name of Christ depart from iniquity.
20 Kwenye nyumba ya kitajiri, siyo kwamba vimo vyombo vya dhahabu na shaba tu. Pia kuna vyombo vya miti na udongo. Baadhi ya hivi ni kwa ajili ya matumizi ya heshima na baadhi yake ni kwa matumizi yasiyo ya heshima.
In a great house, however, there are not only vessels of gold and of silver, but also of wood and of earth, and some for honor, and some for dishonor.
21 Ikiwa mtu atajitakasa mwenyewe kutoka kwenye matumizi yasiyo ya heshima, yeye ni chombo chenye kuheshimika. Ametengwa maalumu, mwenye manufaa kwa Bwana, na ameandaliwa kwa kila kazi njema.
If, therefore, any one will cleanse himself from these strifes about words, he will be a vessel for honor, sanctified, highly useful to the master, prepared for every good work.
22 Zikimbie tamaa za ujanani. Ukifuata haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
Shun youthful desires, and follow righteousness, faithfulness, love, peace, with those who call on the Lord out of a pure heart.
23 Lakini ukatae upumbavu na maswali ya kipuuzi. Kwani unajua ya kuwa huzaa ugomvi.
But avoid foolish and unprofitable questions, because you know that they produce contentions:
24 Mtumishi wa Bwana hapaswi kugombana, badala yake inampasa kuwa mpole kwa watu wote, awezaye kufundisha, na mvumilivu.
and the servant of the Lord must not be contentious, but gentle toward all men, able to teach, patient under evils,
25 Ni lazima awaelimishe kwa upole wale wampingao. Yamkini Mungu aweze kuwapatia toba kwa kuifahamu kweli.
in meekness instructing those who oppose themselves, if, possibly, God may give them repentance in order to the acknowledgment of the truth,
26 Waweze kupata ufahamu tena na kuepuka mtego wa Shetani, baada ya kuwa wametekwa na yeye kwa ajili ya mapenzi yake.
and that they may awake to sobriety out of the snare of the devil, after having been taken captive by him according to his will.

< 2 Timotheo 2 >