< 2 Timotheo 1 >

1 Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, sawasawa na ahadi ya uzima ulio ndani ya Kristo Yesu,
Paul, an apostle of Jesus Christ by the will of God according to the promise of life that is in Christ Jesus,
2 kwa Timotheo mwana mpendwa: Neema, rehema na amani toka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my beloved child: Grace, mercy, and peace from God the Father and Christ Jesus our Lord.
3 Ninamshukuru Mungu, ambaye ninamtumikia kwa nia njema kama walivyofanya baba zangu, ninapokumbuka daima katika maombi yangu. Usiku na
I thank God, whom I serve with a clear conscience as my forefathers did, as night and day I constantly remember yoʋ in my prayers.
4 mchana ninatamani kukuona, ili kwamba nijawe na furaha. Ninayakumbuka machozi yako.
Recalling yoʋr tears, I long to see yoʋ so that I may be filled with joy.
5 Nimekuwa nikikumbushwa kuhusu imani yako halisi, ambayo hapo kwanza ilikaa kwa bibi yako Loisi na mama yako Yunisi. Na nina hakika ya kwamba imani hiyo inakaa ndani yako pia.
I am reminded of the sincere faith that is in yoʋ, which dwelt first in yoʋr grandmother Lois and in yoʋr mother Eunice, and now, I am sure, dwells in yoʋ also.
6 Hii ndiyo sababu nakukumbusha kuchochea karama ya Mungu iliyomo ndani yako kwa njia ya kuwekewa mikono yangu.
Therefore I remind yoʋ to rekindle the gift of God that is in yoʋ through the laying on of my hands.
7 Kwa kuwa Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na upendo na nidhamu.
For God did not give us a spirit of timidity, but a spirit of power, love, and sound judgment.
8 Kwa hiyo usiuonee haya ushuhuda kuhusu Bwana wetu, wala wangu mimi Paulo mfungwa wake. Bali ushiriki mateso kwa ajili ya injili sawasawa na uweza wa Mungu.
Therefore do not be ashamed of the testimony of our Lord or of me his prisoner. Rather, join with me in suffering for the gospel as you rely on the power of God.
9 Ni Mungu aliyetuokoa na kutuita kwa wito mtakatifu. Hakufanya hivi kulingana na kazi zetu bali kulingana na neema na mpango wake mwenyewe. Alitupatia mambo haya katika Kristo Yesu kabla ya nyakati kuanza. (aiōnios g166)
He saved us and called us with a holy calling, not according to our works, but according to his own purpose and grace. This grace was given to us in Christ Jesus before time began, (aiōnios g166)
10 Lakini sasa wokovu wa Mungu umekwishafunuliwa kwa kuja kwa mwokozi wetu Kristo Yesu. Ni Kristo aliyeikomesha mauti na kuleta uzima usiokoma kwa nuru ya injili.
but has now been revealed through the appearing of our Savior Jesus Christ, who abolished death and brought life and immortality to light through the gospel.
11 Kwa sababu hiyo nilichaguliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu.
For this gospel I was appointed to be a preacher, an apostle, and a teacher of the Gentiles.
12 Kwa sababu hii nateseka pia, lakini sioni haya kwa kuwa namjua yeye niliyekwisha kumuamini. Nina hakika kuwa yeye anaweza kukitunza kile nilichokikabidhi kwake hata siku ile.
That is why I am suffering these things. But I am not ashamed, for I know whom I have believed, and I am persuaded that he is able to guard what has been entrusted to me until that day.
13 Ukumbuke mfano wa ujumbe wa uaminifu uliousikia toka kwangu, pamoja na imani na upendo ulio ndani ya Kristo Yesu.
Hold to the pattern of sound teaching that yoʋ have heard from me, in the faith and love that are in Christ Jesus.
14 Yatunze Mambo mazuri aliyokukabidhi Mungu kupitia Roho Mtakatifu aishiye ndani yetu.
By the Holy Spirit who dwells within us, guard the good deposit that has been entrusted to yoʋ.
15 Unajua ya kuwa, wote waishio katika Asia waliniacha. Kwenye kundi hili wamo Figelo na Hemogene.
Yoʋ know that everyone in Asia has turned away from me, including Phygelus and Hermogenes.
16 Bwana airehemu nyumba ya Onesiforo kwa kuwa mara nyingi aliniburudisha na hakuionea aibu minyororo yangu.
May the Lord give mercy to the household of Onesiphorus, because he often refreshed me and was not ashamed of my chains.
17 Badala yake, alipokuwa Roma alinitafuta kwa bidii na akanipata.
On the contrary, when he arrived in Rome, he sought me out very diligently and found me.
18 Mungu amjalie kupata rehema kutoka kwake siku ile. Kama alivyonisaidia nilipokuwa Efeso, wewe wajua vyema.
May the Lord grant him to find mercy from the Lord on that day! Yoʋ know very well all the ways he helped me in Ephesus.

< 2 Timotheo 1 >