< 2 Timotheo 1 >

1 Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, sawasawa na ahadi ya uzima ulio ndani ya Kristo Yesu,
From Paul who, by the will of God, is an apostle of Christ Jesus, charged to proclaim the life that comes from union with Christ Jesus,
2 kwa Timotheo mwana mpendwa: Neema, rehema na amani toka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my dear child: may God, the Father, and Christ Jesus, our Lord, bless you, and be merciful to you, and give you peace.
3 Ninamshukuru Mungu, ambaye ninamtumikia kwa nia njema kama walivyofanya baba zangu, ninapokumbuka daima katika maombi yangu. Usiku na
I am thankful to God, whom I serve, as my ancestors did, with a clear conscience, when I remember you, as I never fail to do, in my prayers – night and day alike,
4 mchana ninatamani kukuona, ili kwamba nijawe na furaha. Ninayakumbuka machozi yako.
as I think of your tears, longing to see you, that my happiness may be completed,
5 Nimekuwa nikikumbushwa kuhusu imani yako halisi, ambayo hapo kwanza ilikaa kwa bibi yako Loisi na mama yako Yunisi. Na nina hakika ya kwamba imani hiyo inakaa ndani yako pia.
now that I have been reminded of the sincere faith that you have shown. That faith was seen first in your grandmother Lois and your mother Eunice, and is now, I am convinced, in you also.
6 Hii ndiyo sababu nakukumbusha kuchochea karama ya Mungu iliyomo ndani yako kwa njia ya kuwekewa mikono yangu.
And that is my reason for reminding you to stir into flame that gift of God, which is yours through your ordination at my hands.
7 Kwa kuwa Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na upendo na nidhamu.
For the Spirit which God gave us was not a spirit of cowardice, but a spirit of power, love, and self-control.
8 Kwa hiyo usiuonee haya ushuhuda kuhusu Bwana wetu, wala wangu mimi Paulo mfungwa wake. Bali ushiriki mateso kwa ajili ya injili sawasawa na uweza wa Mungu.
Do not, therefore, be ashamed of the testimony which we have to bear to our Lord, or of me imprisoned for his sake; but join with me in suffering for the good news, as far as God enables you.
9 Ni Mungu aliyetuokoa na kutuita kwa wito mtakatifu. Hakufanya hivi kulingana na kazi zetu bali kulingana na neema na mpango wake mwenyewe. Alitupatia mambo haya katika Kristo Yesu kabla ya nyakati kuanza. (aiōnios g166)
It was God who saved us, and from him we received our solemn call – not as a reward for anything that we had done, but in fulfilment of his own loving purpose. For that love was extended to us, through Christ Jesus, before time began, (aiōnios g166)
10 Lakini sasa wokovu wa Mungu umekwishafunuliwa kwa kuja kwa mwokozi wetu Kristo Yesu. Ni Kristo aliyeikomesha mauti na kuleta uzima usiokoma kwa nuru ya injili.
and has now been made apparent through the appearing of our Saviour, Christ Jesus; who has made an end of death, and has brought life and immortality to light by that good news,
11 Kwa sababu hiyo nilichaguliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu.
of which I was myself appointed a herald, apostle, and teacher.
12 Kwa sababu hii nateseka pia, lakini sioni haya kwa kuwa namjua yeye niliyekwisha kumuamini. Nina hakika kuwa yeye anaweza kukitunza kile nilichokikabidhi kwake hata siku ile.
That is why I am undergoing these sufferings; yet I feel no shame, for I know in whom I have put my faith, and am convinced that he is able to guard what I have entrusted to him until that day.
13 Ukumbuke mfano wa ujumbe wa uaminifu uliousikia toka kwangu, pamoja na imani na upendo ulio ndani ya Kristo Yesu.
Keep before you, as an example of sound teaching, all that you learnt from me as you listened with that faith and love which come from union with Christ Jesus.
14 Yatunze Mambo mazuri aliyokukabidhi Mungu kupitia Roho Mtakatifu aishiye ndani yetu.
Guard by the help of the Holy Spirit, who is within us, the glorious trust that has been committed to you.
15 Unajua ya kuwa, wote waishio katika Asia waliniacha. Kwenye kundi hili wamo Figelo na Hemogene.
You know, of course, that all our friends in Roman Asia turned their backs on me, including Phygellus and Hermogenes.
16 Bwana airehemu nyumba ya Onesiforo kwa kuwa mara nyingi aliniburudisha na hakuionea aibu minyororo yangu.
May the Lord show mercy to the household of Onesiphorus; for he often cheered me and was not ashamed of my chains.
17 Badala yake, alipokuwa Roma alinitafuta kwa bidii na akanipata.
On the contrary, when he arrived in Rome, he sought eagerly for me until he found me.
18 Mungu amjalie kupata rehema kutoka kwake siku ile. Kama alivyonisaidia nilipokuwa Efeso, wewe wajua vyema.
The Lord grant that he may find mercy at the hands of the Lord on that day. The many services that he rendered at Ephesus you have the best means of knowing.

< 2 Timotheo 1 >