< 2 Timotheo 1 >

1 Paulo mtume wa Yesu Kristo kwa mapenzi ya Mungu, sawasawa na ahadi ya uzima ulio ndani ya Kristo Yesu,
Paul, an apostle of Yahushua the Messiah by the will of YHWH, according to the promise of life which is in Yahushua the Messiah,
2 kwa Timotheo mwana mpendwa: Neema, rehema na amani toka kwa Mungu Baba na Kristo Yesu Bwana wetu.
To Timothy, my dearly beloved son: Favour, mercy, and peace, from YHWH the Father and Yahushua the Messiah our Master.
3 Ninamshukuru Mungu, ambaye ninamtumikia kwa nia njema kama walivyofanya baba zangu, ninapokumbuka daima katika maombi yangu. Usiku na
I thank YHWH, whom I serve from my forefathers with pure conscience, that without ceasing I have remembrance of thee in my prayers night and day;
4 mchana ninatamani kukuona, ili kwamba nijawe na furaha. Ninayakumbuka machozi yako.
Greatly desiring to see thee, being mindful of thy tears, that I may be filled with joy;
5 Nimekuwa nikikumbushwa kuhusu imani yako halisi, ambayo hapo kwanza ilikaa kwa bibi yako Loisi na mama yako Yunisi. Na nina hakika ya kwamba imani hiyo inakaa ndani yako pia.
When I call to remembrance the unfeigned faith that is in thee, which dwelt first in thy grandmother Lois, and thy mother Eunice; and I am persuaded that in thee also.
6 Hii ndiyo sababu nakukumbusha kuchochea karama ya Mungu iliyomo ndani yako kwa njia ya kuwekewa mikono yangu.
Wherefore I put thee in remembrance that thou stir up the gift of YHWH, which is in thee by the putting on of my hands.
7 Kwa kuwa Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na upendo na nidhamu.
For YHWH hath not given us the spirit of fear; but of power, and of love, and of a sound mind.
8 Kwa hiyo usiuonee haya ushuhuda kuhusu Bwana wetu, wala wangu mimi Paulo mfungwa wake. Bali ushiriki mateso kwa ajili ya injili sawasawa na uweza wa Mungu.
Be not thou therefore ashamed of the testimony of our Master, nor of me his prisoner: but be thou partaker of the afflictions of the evangel according to the power of YHWH;
9 Ni Mungu aliyetuokoa na kutuita kwa wito mtakatifu. Hakufanya hivi kulingana na kazi zetu bali kulingana na neema na mpango wake mwenyewe. Alitupatia mambo haya katika Kristo Yesu kabla ya nyakati kuanza. (aiōnios g166)
Who hath saved us, and called us with an holy calling, not according to our works, but according to his own purpose and Favour, which was given us in Yahushua the Messiah before the world began, (aiōnios g166)
10 Lakini sasa wokovu wa Mungu umekwishafunuliwa kwa kuja kwa mwokozi wetu Kristo Yesu. Ni Kristo aliyeikomesha mauti na kuleta uzima usiokoma kwa nuru ya injili.
But is now made manifest by the appearing of our Saviour Yahushua the Messiah, who hath abolished death, and hath brought life and immortality to light through the glad tidings:
11 Kwa sababu hiyo nilichaguliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu.
Whereunto I am appointed a preacher, and an apostle, and a teacher of the Gentiles.
12 Kwa sababu hii nateseka pia, lakini sioni haya kwa kuwa namjua yeye niliyekwisha kumuamini. Nina hakika kuwa yeye anaweza kukitunza kile nilichokikabidhi kwake hata siku ile.
For the which cause I also suffer these things: nevertheless I am not ashamed: for I know whom I have believed, and am persuaded that he is able to keep that which I have committed unto him against that day.
13 Ukumbuke mfano wa ujumbe wa uaminifu uliousikia toka kwangu, pamoja na imani na upendo ulio ndani ya Kristo Yesu.
Hold fast the form of sound words, which thou hast heard of me, in faith and love which is in Yahushua the Messiah.
14 Yatunze Mambo mazuri aliyokukabidhi Mungu kupitia Roho Mtakatifu aishiye ndani yetu.
That good thing which was committed unto thee keep by the Holy Spirit which dwelleth in us.
15 Unajua ya kuwa, wote waishio katika Asia waliniacha. Kwenye kundi hili wamo Figelo na Hemogene.
This thou knowest, that all they which are in Asia be turned away from me; of whom are Phygellus and Hermogenes.
16 Bwana airehemu nyumba ya Onesiforo kwa kuwa mara nyingi aliniburudisha na hakuionea aibu minyororo yangu.
YHWH give mercy unto the house of Onesiphorus; for he oft refreshed me, and was not ashamed of my chain:
17 Badala yake, alipokuwa Roma alinitafuta kwa bidii na akanipata.
But, when he was in Rome, he sought me out very diligently, and found me.
18 Mungu amjalie kupata rehema kutoka kwake siku ile. Kama alivyonisaidia nilipokuwa Efeso, wewe wajua vyema.
YHWH grant unto him that he may find mercy in that day: and in how many things he ministered unto me at Ephesus, thou knowest very well.

< 2 Timotheo 1 >