< 2 Wathesalonike 3 >

1 Na sasa, ndugu, tuombeeni, kwamba neno la Bwana liweze kuenea na kutukuzwa, kama ilivyo pia kwenu.
Finally, brethren, pray for us, that the word of the Lord may run and be glorified, as with you,
2 Ombeni kwamba tuweze kuokolewa kutoka katika uovu na watu waasi, kwa kuwa si wote wana imani.
and that we may be delivered from unreasonable and wicked men; for it is not all that have faith.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, ambaye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutoka kwa yule mwovu.
But faithful is the Lord, who will establish you, and guard you from evil.
4 Tunaujasiri katika Bwana kwa ajili yenu, kwamba mnatenda na mtaendelea kutenda mambo ambayo tunawaagiza.
And we have confidence in the Lord concerning you, that ye both do and will do the things which we command you.
5 Bwana aweze kuongoza mioyo yenu katika upendo na katika uvumilivu wa Kristo.
And the Lord direct your hearts to the love of God, and to perseverance in the cause of Christ.
6 Sasa tunawaagiza, ndugu, katika jina la Bwana Yesu Kristo, kwamba mwepuke kila ndugu ambaye anaishi maisha ya uvivu na siyo kwa kutokana na desturi ambazo mlipokea kutoka kwetu.
Now we charge you, brethren, in the name of the Lord Jesus Christ, that ye withdraw yourselves from every brother that walketh disorderly, and not after the tradition which they received of us.
7 Kwa kuwa ninyi wenyewe mnajua ni sawa kwenu kutuiga sisi. Hatukuishi miongoni mwenu kama wale ambao hawakuwa na nidhamu.
For ye yourselves know how ye ought to imitate us; for we behaved not ourselves disorderly among you,
8 Na hatukula chakula cha mtu yeyote bila kukilipia. Badala yake, tulifanya kazi usiku na mchana kwa kazi ngumu na kwa shida, ili tusiweze kuwa mzigo kwa yeyote katika ninyi.
neither did we eat any man's bread for nought, but were working with labor and travail night and day, that we might not be burdensome to any of you.
9 Tulifanya hivi si kwa sababu hatuna mamlaka. Badala yake, tulifanya hivi ili tuwe mfano kwenu, ili kwamba mweze kutuiga sisi.
Not because we have not authority, but to make ourselves an example to you, that ye should imitate us.
10 Wakati tulipokuwa pamoja nanyi tuliwaagiza, “Ikiwa mmoja wenu hataki kufanya kazi, na asile.”
For also when we were with you, this we commanded you: If any one will not work, neither let him eat.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi wanaenenda kwa uvivu miongoni mwenu. Hawafanyi kazi lakini badala yake ni watu wasio na utaratibu.
For we hear of some who walk among you disorderly, working not at all, but are busybodies.
12 Sasa hao nao tunaagiza na kuwaasa katika Bwana Yesu Kristo, kwamba lazima wafanye kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe.
Now such we charge and exhort in the Lord Jesus Christ, that with quietness they work, and eat their own bread.
13 Lakini ninyi, ndugu, msizimie roho katika kufanya yaliyo sahihi.
But ye, brethren, be not weary in well-doing.
14 Ikiwa mtu yeyote hataki kutii neno letu katika waraka huu, mwe makini naye na msiwe na ushirika pamoja naye, ili kwamba aweze kuaibika.
And if any one obey not our word by this epistle, mark that man; and keep no company with him, that he may be shamed;
15 Msimchukulie kama adui, lakini mwonyeni kama ndugu.
yet count him not as an enemy, but admonish him as a brother.
16 Bwana wa amani mwenyewe awape amani wakati wowote katika njia zote. Bwana awe nanyi nyote.
Now the Lord of peace himself give you peace always in every way; the Lord be with you all.
17 Hii ni salam yangu, Paulo, kwa mkono wangu mwenyewe, ambayo ni alama katika kila waraka. Hivi ndivyo niandikavyo.
The salutation by the hand of me, Paul; which is the token in every letter; so I write.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iweze kuwa nanyi nyote.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you all.

< 2 Wathesalonike 3 >