< 2 Wathesalonike 2 >
1 Sasa kuhusu kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanywa pamoja ili tuwe naye: tunawaomba ninyi ndugu zetu,
And we ask you, brothers, in regard to the coming of our Lord Jesus Christ, and of our gathering together to Him,
2 kwamba msisumbuliwe wala kutabishwa kwa urahisi, kwa roho, au kwa ujumbe au kwa barua inayoonkana kuwa imetoka kwetu, ikisema ya kuwa siku ya Bwana tayari imekuja.
that you are not quickly shaken in mind, nor be troubled, neither through spirit, neither through word, neither through letters as through us, as that the Day of the LORD has arrived;
3 Mtu na asiwadanganye kwa namna yoyote. Kwa kuwa haitakuja mpaka lile anguko litokee kwanza na mtu wa uasi afunuliwe, yule mwana wa uharibifu.
do not let anyone deceive you in any way, because if the departure may not come first, the man of lawlessness may [not] be revealed—the son of destruction,
4 Huyu ndiye apingaye naye hujiinua mwenyewe akimpinga Mungu na chochote kinachoabudiwa. Na matokeo yake, hukaa kwenye hekalu la Mungu na kujionyesha yeye kuwa kama Mungu.
who is opposing and is raising himself up above all called god or worshiped, so as for him to have sat down in the temple of God, proclaiming that he is God.
5 Je, hamkumbuki kuwa nilipokuwa nanyi niliwaambia juu ya mambo haya?
Do you not remember that, yet being with you, I said these things to you?
6 Sasa mnajua kile kinachomzuia, ili kwamba aweze kufunuliwa kwa wakati sahihi utakapowadia.
And now, you have known what is restraining, for his being revealed in his own time,
7 Kwa kuwa siri ya yule mtu mwenye kuasi inafanya kazi mpaka sasa, ila tu kuna anaye mzuia sasa mpaka atakapotolewa njiani.
for the secret of lawlessness already works, only the [One] now restraining [will do so] until He may come out of [the] midst,
8 Ndipo yule mwenye kuasi atakapofunuliwa, amabaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake. Bwana atamfanya kuwa si chochote kwa ufunuo wa ujio wake.
and then the lawless one will be revealed, whom the LORD will consume with the Spirit of His mouth, and will nullify at the appearance of His coming,
9 Ujio wa yule mwenye kuasi utakuwa kwa sababu ya kazi ya shetani kwa nguvu zote, ishara na maajabu ya uongo,
whose coming is according to the working of Satan, in all power, and signs, and lying wonders,
10 na uongo wote wenye udhalimu. Mambo haya yatakuwepo kwa wale wanaopotea, kwa sababu hawakuupokea upendo wa kweli kwa ajili ya kuokolewa kwao.
and in all deceitfulness of the unrighteousness in those perishing, because they did not receive the love of the truth for their being saved,
11 Kwa sababu hiyo Mungu anawatumia kazi yenye uovu ili waamini uongo.
and because of this God will send to them a working of delusion, for their believing the lie,
12 Matokeo yake ni kwamba wote watahukumiwa, wale ambao hawakuamini ukweli bali wao hujifurahisha katika udhalimu.
that they may be judged—all who did not believe the truth, but were well pleased in the unrighteousness.
13 Lakini inatupasa tumshukuru Mungu kila mara kwa ajili yenu ndugu mpendwao na Bwana. Kwa sababu Bwana aliwachagua ninyi kama malimbuko ya wokovu kwa utakaso wa Roho na imani katika ile kweli.
And we ought to give thanks to God always for you, brothers, beloved by the LORD, that God chose you from the beginning to salvation, in sanctification of the Spirit, and belief of the truth,
14 Hiki ndicho alichowaitieni ninyi, kwamba kupitia injili muweza kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
to which He called you through our good news, to the acquiring of the glory of our Lord Jesus Christ;
15 Kwa hiyo, ndugu, simameni imara. Ueleweni ule utamaduni mliofundishwa, kwa neno au kwa barua yetu.
so, then, brothers, stand fast, and hold the traditions that you were taught, whether through word, whether through our letter;
16 Sasa, Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe, na Mungu Baba yetu aliyetupenda na kutupa faraja ya milele na ujasiri mwema kwa ajili ya maisha yajayo kupitia neema, (aiōnios )
and may our Lord Jesus Christ Himself, and our God and Father, who loved us, and gave continuous comfort, and good hope in grace, (aiōnios )
17 awafariji na kuifanya imara mioyo yenu katika kila neno na kazi njema.
comfort your hearts, and establish you in every good word and work.