< 2 Samweli 1 >

1 Baada ya kifo cha Sauli, Daud alirudi kutoka kuwashambulia Waamaleki na akakaa Siklagi kwa siku mbili.
And so it was, after the death of Saul, when David had returned from the smiting of the Amalekites, and David had abode in Ziklag two days,
2 Siku ya tatu, mtu mmoja alikuja kutoka kambi ya Sauli nguo zake zikiwa zimeraruliwa na akiwa na vumbi juu ya kichwa chake. Alipofika kwa Daudi alinamisha uso wake chini akajifanya yeye mwenyewe kuwa si kitu.
yea so it was, on the third day, that lo! a man came out of the camp, from Saul, with his clothes rent, and earth upon his head, —and so it was, when he came in unto David, that he fell to the earth, and did homage.
3 Daudi akamuliza, “Unatoka wapi?” Yeye akajibu, “Nimeponyoka kutoka kambi ya Israeli.”
And David said unto him, From whence comest thou? And he said unto him, Out of the camp of Israel, am I escaped.
4 Daudi akamwambia, “Tafadhari nieleze jinsi mambo yalivyokuwa.” Akajibu, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wameanguka, na wengi wao wameuawa. Sauli na Yonathani mwanawe pia wameuawa.”
And David said unto him—How turned out the matter? tell me, I pray thee. And he said—The people have fled from the battle, yea moreover, many, of the people have fallen, and died, Yea moreover, Saul, and Jonathan his son, are dead.
5 Daudi akamwuliza kijana, “unajuaje kuwa Sauli na Yonathani mwanawe wameuawa?”
Then said David unto the young man who was telling him, —How knowest thou that Saul and Jonathan his son are dead?
6 Yule kijana akajibu, “Kwa bahati nilikuwa juu ya Mlima Gilboa, na pale alikuwepo Sauli ameegemea mkuki wake, na magari ya farasi na waongozaji walikuwa karibu kumkamata.
And the young man who was telling him said, It, so happened, that I was on Mount Gilboa, when lo! Saul, leaning upon his spear, and lo! the chariots and horsemen, hotly pursued him;
7 Sauli alipogeuka aliniona na akaniita. Nikajibu, 'Mimi hapa.'
so he turned behind him, and saw me, —and cried out unto me, and I said, Behold me!
8 Akaniuliza, 'Wewe ni nani?' Nikamjibu, 'Mimi ni Mwamaleki,'
And he said unto me, Who art thou? And I said unto him, An Amalekite, am I.
9 Akaniambia, Tafadhari simama juu yangu uniuwe, kwa kuwa shida kubwa imenipata, lakini uhai ungalimo ndani yangu.'
And he said unto me, I pray thee, take thy stand by me, and put me to death, for the cramp hath seized me, —even for as long as my life shall be in me.
10 Hivyo nilisimama juu yake nikamuuwa, kwa maana nilijua kwamba asingeweza kuishi baada ya kuwa ameanguka. Ndipo nikachukuwa taji iliyokuwa juu ya kichwa chake na kikuku kilichokuwa mkononi mwake, na nimevileta hapa kwako, bwana wangu.”
So I took my stand by him, and put him to death, for I perceived that he could not survive his fall, —so I took the crown that was on his head, and the bracelet that was on his arm, and have brought them in unto my lord, here.
11 Kisha Daudi akararua mavazi yake, na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafanya vilevile.
Then David took hold of his clothes, and rent them, —yea moreover, [so did] all the men who were with him.
12 Walilia, wakaomboleza na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli, Yonathani mwanawe, watu wa Yahwe, na kwa ajili ya nyumba ya Israeli kwa maana wameanguka kwa upanga.
And they lamented aloud, and wept, and fasted until the evening, —for Saul, and for Jonathan his son, and for the people of Yahweh, and for the house of Israel, because they had fallen by the sword.
13 Daudi akamwambia yule kijana, “Unatokea wapi?” Akajibu, mimi ni kijana wa mgeni Mwamaleki.”
And David said unto the young man who was telling him, Whence art thou? And he said, Son of a sojourner—an Amalekite, am I.
14 Daudi akamwambia, “Kwa nini haukuogopa kumwua mfalme, mtiwa mafuta wa Yahwe kwa mkono wako?”
And David said unto him, —How wast thou not afraid to thrust forth thy hand, to destroy the Anointed of Yahweh?
15 Daudi akamwita mmojawapo wa vijana na akamwambia, “Nenda ukamuue.” Hivyo kijana huyo akaenda na kumpiga hata ata chini, Mwamaleki akafa.
So David called one of the young men, and said, —Go near—fall upon him. And he smote him, that he died.
16 Ndipo Daudi akamwambia Mwamaleke aliyekufa, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako kwa kuwa kinywa chako kimeshuhudia dhidi yako kusema, Nimemuua mfalme mtiwa mafuta wa Yahwe.
And David said unto him, Thy blood, be upon thine own head, —for, thine own mouth, hath testified against thee, saying, I myself, put to death the Anointed of Yahweh.
17 Ndipo Daudi akaimba wimbo wa maombolezo juu ya Sauli na Yonathani mwanawe.
Then chanted David this dirge, —over Saul and over Jonathan his son;
18 Akawaamuru watu kuufundisha wimbo wa Bow kwa wana wa Yuda, ambao umeandikwa katika Kitabu cha Yashari.
and he thought to teach the sons of Judah [the song of] the Bow, —lo! it is written in the Book of the Upright: —
19 “Utukufu wako, Israel, umeondolewa, umeondolewa juu ya mahali pako pa juu! Jinsi mwenye nguvu alivyoanguka!
The beauty of Israel! on thy high plumes—slain! How have fallen—the mighty!
20 Msiiseme katika Gathi, msiitangaze katika mitaa ya Ashikeloni, ili binti za wafilisti wasifurahi, ili binti za wasiotailiwa wasisherehekee.
Do not tell it in Gath, Do not publish it in the streets of Ashkelon, —lest the daughters of the Philistines rejoice, lest the daughters of the Uncircumcised triumph.
21 Milima ya Gilboa, kusiwe na umande au mvua juu yenu. wala mashamba yasitoe nafaka kwa ajili ya sadaka, kwa maana hapo ngao ya mwenye nguvu imeharibiwa. Ngao ya Sauli haiwezi tena kutiwa mafuta.
Ye mountains in Gilboa! Be there neither dew nor rain upon you, nor fields of offerings, —for, there, were cast away, the shields of the mighty, The shield of Saul, unanointed with oil.
22 Kutoka katika damu ya waliouawa, kutoka katika miili ya wenye nguvu, upinde wa Yonathani haukurudi nyuma, na upanga wa Sauli haukurudi patupu.
From the blood of the slain, from the fat of the mighty, the bow of Jonathan ne’er drew back, —and, the sword of Saul, ne’er returned, empty.
23 Sauli na Yonathani walikuwa wakipendwa na walikuwa wenye neema maishani, hata wakati wa mauti yao walikuwa pamoja. Walikuwa na kasi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
Saul and Jonathan, delightfully loving in their lives, even, in their death, were not divided, —Beyond eagles, were they swift, beyond lions, were they strong!
24 Enyi binti wa Israeli lieni juu ya Sauli, aliyewavika mavazi ya thamani pamoja na vito vya thamani, na aliyetia mapambo ya dhahabu katika mavazi yenu.
Ye daughters of Israel! For Saul, weep ye, —who clothed you in crimson, [decked] with lovely things, who hung ornaments of gold on your apparel!
25 Jinsi wenye nguvu walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa juu ya mahali pako pa juu.
How have fallen the mighty, in the midst of the battle! Jonathan, on thy high places, slain!
26 Nimesikitishwa sana kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu. Ulikuwa mpendwa wangu sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, ukipita upendo wa wanawake.
I am distressed for thee, my brother, Jonathan! Delightful to me, exceedingly, —Wonderful, was thy love to me, passing the love of women.
27 Jinsi wenye nguvu walivyoanguka na silaha za vita zimeteketea!”
How have fallen the mighty, and perished the weapons of war!

< 2 Samweli 1 >