< 2 Samweli 9 >
1 Daudi akasema, “Je kuna yeyote aliyesalia wa familia ya Sauli ambaye naweza kumwonyesha kwa fadhiri kwa ajili ya Yonathani?
And David said, Is there still anyone of Saul's family living, so that I may be a friend to him, because of Jonathan?
2 Alikuwepo mtumishi katika familia ya Sauli jina lake Siba, akaitwa kwa Daudi. Mfalme akamuuliza, “Je wewe ndiye Siba?” Akajibu, “Mimi ni mtumishi wako, ndiye.”
Now there was of Saul's people a servant named Ziba, and they sent him to David; and the king said to him, Are you Ziba? And he said, I am.
3 Hivyo mfalme akasema, “Je hakuna aliyesalia wa familia ya Sauli ambaye naweza kumuonesha wema wa Mungu?” Siba akamjibu mfalme, “Yonathani ana mwana, ambaye ni mlemavu wa miguu.
And the king said, Is there anyone of Saul's family still living, to whom I may be a friend in God's name? And Ziba said, There is a son of Jonathan, whose feet are damaged.
4 Mfalme akamwambia, “Yupo wapi?” Siba akamjibu mfalme, “Tazama, yupo katika nyumba ya Makiri mwana wa Amieli huko Lo Debari.
And the king said to him, Where is he? And Ziba said to the king, He is in the house of Machir, the son of Ammiel, in Lo-debar.
5 Ndipo mfalme Daudi akatuma watu na kumtoa katika nyumba ya Makiri mwana wa Amieli huko Lo Debari.
Then King David sent, and had him taken from Lo-debar, from the house of Machir, the son of Ammiel.
6 Hivyo Mefiboshethi mwana wa Yonathani mwana wa Sauli, akaja kwa Daudi naye akainama uso wake hadi katika sakafu kwa kumheshimu Daudi. Daudi akasema, “Mefiboshethi.” Naye akajibu, “Angalia, mimi ni mtumishi wako!
And Mephibosheth, the son of Jonathan, came to David, and falling down on his face, gave him honour. And David said, Mephibosheth. And answering he said, Your servant is here.
7 Daudi akamwambia, “Usiogope, maana hakika nitakufadhiri kwa ajili ya Yonathani baba yako, nami nitakurudishia ardhi yote ya Sauli babu yako, nawe utakula katika meza yangu daima.”
And David said to him, Have no fear: for truly I will be good to you, because of your father Jonathan, and I will give back to you all the land which was Saul's; and you will have a place at my table at all times.
8 Mefiboshethi akainama na kusema, “Mtumishi wako ni nani, hata ukamwangalia kwa fadhiri mbwa mfu kama nilivyo?”
And he went down on his face before the king, and said, What is your servant, for you to take note of a dead dog such as I am?
9 Kisha mfalme akamwita Siba, mtumishi wa Sauli, na kumwambia, “Yote yaliyo ya Sauli na familia yake nimempa mjukuu wa bwana wako.
Then the king sent for Ziba, Saul's servant, and said to him, All the property of Saul and of his family I have given to your master's son.
10 Wewe, wanao, na watumishi wako mtalima mashamba kwa ajili yake nanyi mtavuna mazao ili kwamba mjukuu wa bwana wako apate chakula. Kwa maana Mefiboshethi, mjukuu wa bwana wako, atakula katika meza yangu daima.” Basi Siba alikuwa na wana kumi na watano na watumishi ishirini.
And you and your sons and your servants are to take care of the land for him, and get in the fruit of it, so that your master's son may have food: but Mephibosheth, your master's son, will have a place at my table at all times. Now Ziba had fifteen sons and twenty servants.
11 Kisha Siba akamwambia mfalme, “Mtumishi wako atafanya yote ambayo bwana wangu mfalme amemwamuru mtumishi wake.” Mfalme akaongeza kusema, kwa Mefiboshethi yeye atakula katika meza yangu, kama mmojawapo ya wana wa mfalme.”
Then Ziba said to the king, Every order which you have given to your servant will be done. As for Mephibosheth, he had a place at David's table, like one of the king's sons.
12 Mefiboshethi alikuwa na mwana mdogo jina lake Mika. Na wote waliokuwa wanaishi katika nyumba ya Siba walikuwa watumishi wa Mefiboshethi.
And Mephibosheth had a young son named Mica. And all the people living in the house of Ziba were servants to Mephibosheth.
13 Hivyo Mefiboshethi akaishi Yerusalemu, naye akala chakula cha daima katika meza ya mfalme, japokuwa alikuwa mlemavu wa miguu yote.
So Mephibosheth went on living in Jerusalem; for he took all his meals at the king's table; and he had not the use of his feet.