< 2 Samweli 6 >
1 Basi kwa mara nyingine Daudi akawakusanya wateuli wa Israeli, elfu thelathini.
Then David chose 30,000 Israeli men and gathered them together.
2 Daudi akainuka na akaenda na watu wake wote waliokuwa pamoja naye kutoka Baala ulioko Yuda ili alilete sanduku la Mungu, liitwalo kwa jina la Yahwe wa majeshi, akaaye juu ya makerubi.
He led them to the place in Judah [formerly] called Baalah, [now called Kiriath-Jearim]. They went in order to bring from there [to Jerusalem] the sacred chest, which had the name of Yahweh, the leader of the armies of [the angels in] heaven, written on it, and which had the [statues of the] winged creatures on top of it. Between those statues was where Yahweh spoke messages about ruling his people [MTY].
3 Wakaliweka sanduku la Mungu juu ya mkokoteni mpya. Wakalitoa katika nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wanawe, wakauongoza mkokoteni.
The sacred chest was in the house of Abinadab, on top of a hill. They went there, and they put the chest on a new cart. Uzzah and Ahio, the two sons of Abinadab, were guiding [the oxen that were pulling the cart].
4 Wakautoa mkokoteni na sanduku la Mungu juu yake nyumbani mwa Abinadabu juu ya kilima. Ahio alikuwa ametangulia mbele ya sanduku.
Uzzah walked alongside the cart, and Ahio walked in front of it.
5 Kisha Daudi na nyumba yote ya Israeli wakaanza kucheza mbele ya Yahwe, wakishangilia kwa vyombo vya mziki, vinubi, vinanda, matari, kayamba na matowazi.
David and all the Israeli men were celebrating in God’s presence, singing with all their strength and [playing] lyres and harps, and beating tambourines, and clashing castanets and cymbals.
6 Hata walipofika katika shinikizo la Nasoni, wale ng'ombe wakakwama, Uza akanyosha mkono wake na kulikumbatia sanduku la Mungu, naye akalishikilia.
But when they came to the place where Nacon threshed grain, the oxen stumbled. So Uzzah put his hand on the sacred chest to (steady it/prevent it from falling [off the cart]).
7 Kisha asira ya Yahweh ikawaka dhidi ya Uza. Mungu akampiga kwa ajili ya dhambi yake. Uza akafa pale pale kando ya sandaku la Mungu.
Yahweh immediately became very angry with Uzzah, and he killed him right there alongside the sacred chest, because he had touched the chest, [and Yahweh had commanded that only the descendants of Levi who help the priests should touch the sacred chest].
8 Daudi akakasirika kwa kuwa Yahwe alimpiga Uza, naye akapaita mahali pale Peresi Uza. Eneo hilo linaitwa Peres Uza hata leo.
David was angry because Yahweh had punished Uzzah. So ever since that time, that place has been called ‘The Punishment of Uzzah’.
9 Daudi akamwogopa Yahweh siku hiyo. Akasema, “Sanduku la Yahwe lawezaje kuja kwangu?”
David was [also] afraid of [what else] Yahweh [would do to punish them], so he said, “(How can I take the sacred chest with me [to Jerusalem]?/I am afraid to take the sacred chest with me [to Jerusalem].)” [RHQ]
10 Hivyo Daudi hakuwatayari tena kulichukua sanduku la Yahwe katika mji wa Daudi. Badala yake, akaliweka kando katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti.
So he did not want to take the sacred chest to Jerusalem. Instead, they took it to another place; they took it to the house of Obed-Edom, from Gath [city].
11 Sanduku la Yahwe likakaa katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti kwa miezi mitatu. Kwa hiyo Yahwe akambariki yeye na nyumba yake yote.
They left the sacred chest in the house of Obed-Edom for three months, and [during that time] Yahweh blessed Obed-Edom and his family.
12 Kisha mfalme Daudi akaambiwa, “Yahwe ameibariki nyumba ya Obedi Edomu na kila kitu alichonacho kwa sababu ya sanduku la Mungu.” Hivyo Daudi akaenda na kulipandisha sanduku la Mungu kutoka katika nyumba ya Obedi Edomu hadi mji wa Daudi kwa furaha.
Later, people told David, “Yahweh has blessed Obed-Edom and his family because [he is taking care] of the sacred chest!” When David heard that, he [and some other men] went to Obed-Edom’s house, and very joyfully brought the sacred chest from there to Jerusalem.
13 Ikawa waliolibeba sanduku la Yahwe walipochukua hatua sita, akatoa sadaka ng'ombe na ndama aliyenona.
[This time, descendants of Levi] were carrying the sacred chest, but when they had walked only six steps, they stopped, and there David killed a bull and a fat calf, and offered them to Yahweh for a sacrifice.
14 Daudi akacheza mbele ya Yahwe kwa nguvu zake zote; alikuwa amevaa naivera ya kitani pekee.
David was wearing [only] a linen cloth wrapped around his waist, and was dancing very energetically to honor Yahweh.
15 Hivyo Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalipandisha sanduku la Yahwe kwa vifijo na sauti za tarumbeta.
David and the Israeli men took the sacred chest up [to Jerusalem], shouting [loudly] and blowing trumpets.
16 Hata ikawa sanduku la Yahwe lilipofika mjini mwa Daudi, Mikali, binti Sauli, alichungulia dirishani. Akamwona mfalme Daudi akiruka na kucheza mbele ya Yahwe. Akamdharau moyoni mwake.
While they were carrying the sacred chest into the city, [David’s wife] Michal, who was Saul’s daughter, looked out the window [of her house]. She saw King David leaping and dancing to honor Yahweh. So she was disgusted with him.
17 Wakaliingiza sanduku la Yahwe na kuliweka mahali pake, katikati ya hema ambayo Daudi alikuwa ameliwekea. Kisha Daudi akatoa sadaka ya kuteketezwa na matoleo ya amani mbele za Yahwe.
They brought the sacred chest into the tent that David had erected for it. Then David gave to Yahweh offerings to be completely burned [on an altar], and other offerings to maintain fellowship with Yahweh.
18 Ikawa Daudi alipomaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Yahwe wa majeshi.
When David had finished offering those sacrifices, he asked Yahweh, the Commander of the armies [of the angels], to bless the people.
19 Kisha akawagawia watu wote, umati wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kipande cha mkate, nyama na keki ya zabibu. Kisha watu wote wakaondoka; kila mmoja akarudi kwake.
He also distributed food to all the people. To each Israeli man and woman he gave a loaf of bread, some meat, and a raisin cake. Then all the people returned to their homes.
20 Kisha Daudi akarudi ili aibariki familia yake. Mikali, binti Sauli, akatoka ili akutane na Daudi naye akasema, “Jinsi gani mtukufu mfalme wa Israeli alivyokuwa leo, aliyejiacha uchi mbele ya macho ya vijakazi miongoni mwa watumishi wake, kama mmoja wa wapumbavu ambaye bila aibu hujifunua yeye mwenyewe!”
When David went home to [ask Yahweh to] bless his family, his wife Michal came out to meet him. She said to him, “Maybe you, the king of Israel, [think that you] [IRO] were honoring yourself today, but really, you acted like a fool, uncovering yourself while the female servants of your officials were watching!”
21 Daudi akamjibu Mikali, “Nilifanya hivyo mbele ya Yahwe, aliyenichagua juu ya baba yako na juu ya familia yake yote, aliyeniweka kuwa kiongozi juu ya watu wa Yahwe, juu ya Israeli. Mbele ya Yahwe nitafurahi!
David replied to Michal, “[I was doing that] to honor Yahweh, who chose me instead of your father and other members of his family, to be the king of the Israeli people, the people who belong to Yahweh. And I will [continue to] dance to honor Yahweh!
22 Nitakuwa nisiye na heshima hata zaidi ya hapa, na nitajishusha mbele za macho yangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliowasema, nitaheshimiwa.”
[Even though you think that what I did] was disgraceful, I will continue to do it even more. You may despise me [because of what I did], but the women whom you were talking about will honor me!”
23 Hivyo Mikali, binti Sauli, hakuwa na watato hata alipokufa.
[As a result, ] Saul’s daughter Michal never gave birth to any children.