< 2 Samweli 6 >

1 Basi kwa mara nyingine Daudi akawakusanya wateuli wa Israeli, elfu thelathini.
Againe Dauid gathered together all the chosen men of Israel, euen thirtie thousand,
2 Daudi akainuka na akaenda na watu wake wote waliokuwa pamoja naye kutoka Baala ulioko Yuda ili alilete sanduku la Mungu, liitwalo kwa jina la Yahwe wa majeshi, akaaye juu ya makerubi.
And Dauid arose and went with all the people that were with him from Baale of Iudah to bring vp from thence the Arke of God, whose name is called by the Name of the Lord, of hostes, that dwelleth vpon it betweene the Cherubims.
3 Wakaliweka sanduku la Mungu juu ya mkokoteni mpya. Wakalitoa katika nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wanawe, wakauongoza mkokoteni.
And they put the Arke of God vpon a newe cart, and brought it out of the house of Abinadab that was in Gibeah. And Vzzah and Ahio the sonnes of Abinadab did driue the newe carte.
4 Wakautoa mkokoteni na sanduku la Mungu juu yake nyumbani mwa Abinadabu juu ya kilima. Ahio alikuwa ametangulia mbele ya sanduku.
And when they brought the Arke of God out of the house of Abinadab, that was at Gibeah, Ahio went before the Arke,
5 Kisha Daudi na nyumba yote ya Israeli wakaanza kucheza mbele ya Yahwe, wakishangilia kwa vyombo vya mziki, vinubi, vinanda, matari, kayamba na matowazi.
And Dauid and al the house of Israel played before the Lord on all instruments made of firre, and on harpes, and on Psalteries, and on timbrels, and on cornets, and on cymbals.
6 Hata walipofika katika shinikizo la Nasoni, wale ng'ombe wakakwama, Uza akanyosha mkono wake na kulikumbatia sanduku la Mungu, naye akalishikilia.
And when they came to Nachons threshing floore, Vzzah put his hande to the Arke of God, and helde it: for the oxen did shake it.
7 Kisha asira ya Yahweh ikawaka dhidi ya Uza. Mungu akampiga kwa ajili ya dhambi yake. Uza akafa pale pale kando ya sandaku la Mungu.
And the Lord was verie wroth with Vzzah, and God smote him in the same place for his fault, and there he dyed by the Arke of God.
8 Daudi akakasirika kwa kuwa Yahwe alimpiga Uza, naye akapaita mahali pale Peresi Uza. Eneo hilo linaitwa Peres Uza hata leo.
And Dauid was displeased, because the Lord had smitten Vzzah: and he called the name of the place Perez Vzzah vntill this day.
9 Daudi akamwogopa Yahweh siku hiyo. Akasema, “Sanduku la Yahwe lawezaje kuja kwangu?”
Therefore Dauid that day feared the Lord, and sayd, How shall the Arke of the Lord come to mee?
10 Hivyo Daudi hakuwatayari tena kulichukua sanduku la Yahwe katika mji wa Daudi. Badala yake, akaliweka kando katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti.
So Dauid would not bring the Arke of the Lord vnto him into the citie of Dauid, but Dauid caried it into ye house of Obed-edom a Gittite.
11 Sanduku la Yahwe likakaa katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti kwa miezi mitatu. Kwa hiyo Yahwe akambariki yeye na nyumba yake yote.
And the Arke of the Lord continued in the house of Obed-edom the Gittite, three moneths, and the Lord blessed Obed-edom, and all his houshold.
12 Kisha mfalme Daudi akaambiwa, “Yahwe ameibariki nyumba ya Obedi Edomu na kila kitu alichonacho kwa sababu ya sanduku la Mungu.” Hivyo Daudi akaenda na kulipandisha sanduku la Mungu kutoka katika nyumba ya Obedi Edomu hadi mji wa Daudi kwa furaha.
And one told King Dauid, saying, The Lord hath blessed the house of Obed-edom, and all that hee hath, because of the Arke of God: therefore Dauid went and brought the Arke of God from the house of Obed-edom, into the citie of Dauid with gladnesse.
13 Ikawa waliolibeba sanduku la Yahwe walipochukua hatua sita, akatoa sadaka ng'ombe na ndama aliyenona.
And when they that bare the Arke of the Lord had gone sixe paces, he offred an oxe, and a fatte beast.
14 Daudi akacheza mbele ya Yahwe kwa nguvu zake zote; alikuwa amevaa naivera ya kitani pekee.
And Dauid danced before the Lord with al his might, and was girded with a linnen Ephod.
15 Hivyo Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalipandisha sanduku la Yahwe kwa vifijo na sauti za tarumbeta.
So Dauid and all the house of Israel, brought the Arke of the Lord with shouting, and sound of trumpet.
16 Hata ikawa sanduku la Yahwe lilipofika mjini mwa Daudi, Mikali, binti Sauli, alichungulia dirishani. Akamwona mfalme Daudi akiruka na kucheza mbele ya Yahwe. Akamdharau moyoni mwake.
And as the Arke of the Lord came into the citie of Dauid, Michal Sauls daughter looked through a windowe, and sawe King Dauid leape, and dance before the Lord, and shee despised him in her heart.
17 Wakaliingiza sanduku la Yahwe na kuliweka mahali pake, katikati ya hema ambayo Daudi alikuwa ameliwekea. Kisha Daudi akatoa sadaka ya kuteketezwa na matoleo ya amani mbele za Yahwe.
And when they had brought in the Arke of the Lord, they set it in his place, in the mids of the tabernacle that Dauid had pitched for it: then Dauid offred burnt offrings, and peace offrings before the Lord.
18 Ikawa Daudi alipomaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Yahwe wa majeshi.
And assoone as Dauid had made an ende of offring burnt offrings and peace offrings, hee blessed the people in the Name of the Lord of hostes,
19 Kisha akawagawia watu wote, umati wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kipande cha mkate, nyama na keki ya zabibu. Kisha watu wote wakaondoka; kila mmoja akarudi kwake.
And gaue among all the people, euen among the whole multitude of Israel, aswel to the women as men, to euerie one a cake of bread, and a piece of flesh, and a bottell of wine: so all the people departed euerie one to his house.
20 Kisha Daudi akarudi ili aibariki familia yake. Mikali, binti Sauli, akatoka ili akutane na Daudi naye akasema, “Jinsi gani mtukufu mfalme wa Israeli alivyokuwa leo, aliyejiacha uchi mbele ya macho ya vijakazi miongoni mwa watumishi wake, kama mmoja wa wapumbavu ambaye bila aibu hujifunua yeye mwenyewe!”
The Dauid returned to blesse his house, and Michal the daughter of Saul came out to meete Dauid, and sayde, O howe glorious was the King of Israel this day, which was vncouered to day in the eyes of the maidens of his seruantes, as a foole vncouereth himselfe.
21 Daudi akamjibu Mikali, “Nilifanya hivyo mbele ya Yahwe, aliyenichagua juu ya baba yako na juu ya familia yake yote, aliyeniweka kuwa kiongozi juu ya watu wa Yahwe, juu ya Israeli. Mbele ya Yahwe nitafurahi!
Then Dauid sayd vnto Michal, It was before the Lord, which chose me rather then thy father, and all his house, and commanded me to bee ruler ouer the people of the Lord, euen ouer Israel: and therefore will I play before the Lord,
22 Nitakuwa nisiye na heshima hata zaidi ya hapa, na nitajishusha mbele za macho yangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliowasema, nitaheshimiwa.”
And will yet be more vile then thus, and will be low in mine owne sight, and of the verie same maidseruants, which thou hast spoken of, shall I be had in honour.
23 Hivyo Mikali, binti Sauli, hakuwa na watato hata alipokufa.
Therfore Michal the daughter of Saul had no childe vnto the day of her death.

< 2 Samweli 6 >