< 2 Samweli 6 >
1 Basi kwa mara nyingine Daudi akawakusanya wateuli wa Israeli, elfu thelathini.
Then David again gathered together all the elect men of Israel, thirty thousand.
2 Daudi akainuka na akaenda na watu wake wote waliokuwa pamoja naye kutoka Baala ulioko Yuda ili alilete sanduku la Mungu, liitwalo kwa jina la Yahwe wa majeshi, akaaye juu ya makerubi.
And David arose and went away, with the entire people who were with him from the men of Judah, so that they might lead back the ark of God, over which is invoked the name of the Lord of hosts, who sits upon the cherubim above it.
3 Wakaliweka sanduku la Mungu juu ya mkokoteni mpya. Wakalitoa katika nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wanawe, wakauongoza mkokoteni.
And they placed the ark of God on a new cart. And they took it from the house of Abinadab, who was in Gibeon. And Uzzah and Ahio, the sons of Abinadab, drove the new cart.
4 Wakautoa mkokoteni na sanduku la Mungu juu yake nyumbani mwa Abinadabu juu ya kilima. Ahio alikuwa ametangulia mbele ya sanduku.
And when they had taken it from the house of Abinadab, who was in Gibeon, Ahio preceded the ark as the keeper of the ark of God.
5 Kisha Daudi na nyumba yote ya Israeli wakaanza kucheza mbele ya Yahwe, wakishangilia kwa vyombo vya mziki, vinubi, vinanda, matari, kayamba na matowazi.
But David and all of Israel played before the Lord on every kind of musical instrument made of wood, and on harps, and lyres, and timbrels, and bells, and cymbals.
6 Hata walipofika katika shinikizo la Nasoni, wale ng'ombe wakakwama, Uza akanyosha mkono wake na kulikumbatia sanduku la Mungu, naye akalishikilia.
And after they had arrived at the threshing floor of Nacon, Uzzah extended his hand to the ark of God, and he touched it, because the oxen were kicking and had caused it to tip.
7 Kisha asira ya Yahweh ikawaka dhidi ya Uza. Mungu akampiga kwa ajili ya dhambi yake. Uza akafa pale pale kando ya sandaku la Mungu.
And the indignation of the Lord was enraged against Uzzah. And he struck him for his temerity. And there he died, beside the ark of God.
8 Daudi akakasirika kwa kuwa Yahwe alimpiga Uza, naye akapaita mahali pale Peresi Uza. Eneo hilo linaitwa Peres Uza hata leo.
Then David was saddened because the Lord had struck Uzzah. And the name of that place was called: the Striking of Uzzah, even to this day.
9 Daudi akamwogopa Yahweh siku hiyo. Akasema, “Sanduku la Yahwe lawezaje kuja kwangu?”
And David was very fearful of the Lord on that day, saying, “How shall the ark of the Lord be brought to me?”
10 Hivyo Daudi hakuwatayari tena kulichukua sanduku la Yahwe katika mji wa Daudi. Badala yake, akaliweka kando katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti.
And he was not willing to send the ark of the Lord to himself in the city of David. Instead, he sent it into the house of Obededom, the Gittite.
11 Sanduku la Yahwe likakaa katika nyumba ya Obedi Edomu Mgiti kwa miezi mitatu. Kwa hiyo Yahwe akambariki yeye na nyumba yake yote.
And the ark of the Lord dwelt in the house of Obededom the Gittite, for three months. And the Lord blessed Obededom, and all his household.
12 Kisha mfalme Daudi akaambiwa, “Yahwe ameibariki nyumba ya Obedi Edomu na kila kitu alichonacho kwa sababu ya sanduku la Mungu.” Hivyo Daudi akaenda na kulipandisha sanduku la Mungu kutoka katika nyumba ya Obedi Edomu hadi mji wa Daudi kwa furaha.
And it was reported to king David that the Lord had blessed Obededom, and all that was his, because of the ark of God. Therefore, David went and brought the ark of God, from the house of Obededom, into the city of David with joy. And there were with David seven choirs, and calves for victims.
13 Ikawa waliolibeba sanduku la Yahwe walipochukua hatua sita, akatoa sadaka ng'ombe na ndama aliyenona.
And when those who were carrying the ark of the Lord had traveled six steps, he immolated an ox and a ram.
14 Daudi akacheza mbele ya Yahwe kwa nguvu zake zote; alikuwa amevaa naivera ya kitani pekee.
And David danced with all his ability before the Lord. And David was girded with the linen ephod.
15 Hivyo Daudi na nyumba yote ya Israeli wakalipandisha sanduku la Yahwe kwa vifijo na sauti za tarumbeta.
And David, and all the house of Israel, were leading the ark of the testament of the Lord, with jubilation and the sound of the trumpet.
16 Hata ikawa sanduku la Yahwe lilipofika mjini mwa Daudi, Mikali, binti Sauli, alichungulia dirishani. Akamwona mfalme Daudi akiruka na kucheza mbele ya Yahwe. Akamdharau moyoni mwake.
And when the ark of the Lord had entered into the city of David, Michal, the daughter of Saul, looking out through a window, saw king David leaping and dancing before the Lord. And she despised him in her heart.
17 Wakaliingiza sanduku la Yahwe na kuliweka mahali pake, katikati ya hema ambayo Daudi alikuwa ameliwekea. Kisha Daudi akatoa sadaka ya kuteketezwa na matoleo ya amani mbele za Yahwe.
And they led in the ark of the Lord. And they set it in its place in the middle of the tabernacle, which David had pitched for it. And David offered holocausts and peace offerings in the sight of the Lord.
18 Ikawa Daudi alipomaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Yahwe wa majeshi.
And when he had completed offering holocausts and peace offerings, he blessed the people in the name of the Lord of hosts.
19 Kisha akawagawia watu wote, umati wote wa Israeli, wanaume kwa wanawake, kipande cha mkate, nyama na keki ya zabibu. Kisha watu wote wakaondoka; kila mmoja akarudi kwake.
And he distributed to the entire multitude of Israel, as much to men as to women, to each one: one loaf of bread, and one piece of roasted beef, and fine wheat flour fried with oil. And all the people went away, each one to his own house.
20 Kisha Daudi akarudi ili aibariki familia yake. Mikali, binti Sauli, akatoka ili akutane na Daudi naye akasema, “Jinsi gani mtukufu mfalme wa Israeli alivyokuwa leo, aliyejiacha uchi mbele ya macho ya vijakazi miongoni mwa watumishi wake, kama mmoja wa wapumbavu ambaye bila aibu hujifunua yeye mwenyewe!”
And David returned, so that he might bless his own house. And Michal, the daughter of Saul, going out to meet David, said: “How glorious was the king of Israel today, uncovering himself before the handmaids of his servants, and being unclothed, as if one of the performers were unclothed.”
21 Daudi akamjibu Mikali, “Nilifanya hivyo mbele ya Yahwe, aliyenichagua juu ya baba yako na juu ya familia yake yote, aliyeniweka kuwa kiongozi juu ya watu wa Yahwe, juu ya Israeli. Mbele ya Yahwe nitafurahi!
And David said to Michal: “Before the Lord, who chose me rather than your father, and rather than his entire house, and who commanded me, that I should be the leader over the people of the Lord in Israel,
22 Nitakuwa nisiye na heshima hata zaidi ya hapa, na nitajishusha mbele za macho yangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliowasema, nitaheshimiwa.”
I will both play and demean myself, more so than I have done. And I will be little in my own eyes. And with the handmaids, about whom you are speaking, I will appear more glorious.”
23 Hivyo Mikali, binti Sauli, hakuwa na watato hata alipokufa.
And so, there was no child born to Michal, the daughter of Saul, even to the day of her death.