< 2 Samweli 4 >
1 Ikawa Ishboshethi, mwana wa Sauli, aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, mikono yake ikadhoofika, na Israeli yote ikataabika.
Ko je Savlov sin slišal, da je bil Abnêr mrtev v Hebrónu, so bile njegove roke slabotne in vsi Izraelci so bili zaskrbljeni.
2 Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa wakuu wa vikosi vya askari. Mmoja wao alikuwa Baana na mwingine alikuwa Rekabu, wana wa Rimoni Mbeerothi wa wana wa Benjamini(kwa maana Berothi ilihesabiwa kuwa sehemu ya Benjamini,
Savlov sin je imel dva moža, ki sta bila poveljnika čet. Ime enega je bilo Baaná in ime drugega Reháb, sinova Rimóna, Beeróčana, izmed Benjaminovih otrok (kajti tudi Beerót je bil štet k Benjaminu
3 na Waberothi walikimbilia Gitaimu na wamekuwa wakiishi pale hadi sasa).
in Beeróčani so pobegnili v Gitájim in bili tam začasni prebivalci do tega dne.)
4 Basi Yonathani, mwana wa Sauli, alikuwa na mwana mlemavu wa miguu. Alikuwa na umri wa miaka mitano habari kuhusu Sauli na Yonathani ilipofika Yezreeli. Yaya wake akamchukua ili akimbie. Lakini wakati anakimbia, mwana wa Yonathani alianguka na akawa kirema. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.
Savlov sin Jonatan je imel sina, ki je bil hrom od svojih stopal. Pet let je bil star, ko so prišle iz Jezreéla novice o Savlu in Jonatanu in njegova dojilja ga je vzela in pobegnila. Pripetilo pa se je, medtem ko je hitela, da pobegne, da je padel in postal hrom. Njegovo ime je bilo Mefibóšet.
5 Hivyo wana wa Rimoni mbeerothi, Rekabu na Baana, wakasafiri mchana wakati wa jua kali mpaka nyumbani mwa Ishbothethi, yeye alikuwa amepumzika mchana.
Sinova Beeróčana Rimóna, Reháb in Baaná sta odšla in prišla okoli dnevne vročine v hišo Iš Bošeta, ki je opoldan ležal na postelji.
6 Mwanamke aliyekuwa akililinda lango alisinzia wakati akipepeta ngano, Rekabu na Baana waliingia ndani polepole na wakampita.
Prišla sta tja, v sredo hiše, kakor bi hotela vzeti pšenico. Udarila sta ga pod peto rebro in Reháb in njegov brat Baaná sta pobegnila.
7 Hivyo walipoingia ndani ya nyumba, walimpiga na kumuua wakati amelala chumbani mwake. Kisha wakakata kichwa chake na wakaondoka nacho, wakasafiri njiani usiku kucha mpaka Araba.
Kajti ko sta prišla v hišo, je ležal na svoji postelji, v svoji spalnici in udarila sta ga in ga usmrtila in obglavila in vzela njegovo glavo in vso noč bežala čez ravnino.
8 Wakaleta kichwa cha Ishboshethi kwa Daudi huko Hebroni, nao wakamwambia mfalme, “Tazama, hiki ni kichwa cha Ishboshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyekuwa akiutafuta uhai wako. Leo Yahwe amemlipia kisasi bwana wetu mfalme dhidi ya Sauli na uzao wake.”
Glavo Iš Bošeta sta prinesla k Davidu v Hebrón in rekla kralju: »Glej, glava Savlovega sina Iš Bošeta, tvojega sovražnika, ki je iskal tvoje življenje in Gospod je ta dan maščeval mojega gospoda kralja nad Savlom in njegovim semenom.«
9 Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni mbeerothi, akawambia, “Kama Yahwe aishivyo, aliyeuokoa uhai wangu na kila shida,
David pa je odgovoril Rehábu in njegovemu bratu Baanáju, sinovoma Beeróčana Rimóna ter jima rekel: » Kakor živi Gospod, ki je mojo dušo odkupil od vseh nasprotnikov,
10 mtu mmoja aliponiambia, 'Tazama, Sauli amekufa,' akifikiri alileta habari njema, nilimkamata na kumwua huko Siklagi. Huo ndio ujira niliompa kwa habari yake.
ko mi je nekdo povedal, rekoč: ›Glej, Savel je mrtev, ‹ misleč, da je prinesel dobre novice, sem ga prijel in ga usmrtil v Ciklágu. Mislil je, da mu bom dal nagrado za njegove novice.
11 Namna gani, mtu mwovu anapomwua mwenye haki kitandi mwake ndani ya nyumba, Je nisiitake damu yake kutoka katika mikono yenu, na kuwaondoa duniani?”
Koliko mnogo bolj, ko sta zlobneža umorila pravično osebo v njegovi lastni hiši, na njegovi postelji? Mar ne bom torej sedaj zahteval njegovo kri iz vajine roke in vaju vzel proč z zemlje?«
12 Kisha Daudi akawaagiza vijana, nao wakawaua wakakata mikono na miguu yao na kuwatundika kando ya bwawa huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ishboshethi na kukizika katika kaburi la Abneri katika Hebroni.
David je svojim mladeničem zapovedal in so ju ubili ter odsekali njuni roki in njuna stopala in ju obesili gor nad ribnik v Hebrónu. Toda vzeli so glavo Iš Bošeta in jo pokopali v Abnêrjevem mavzoleju v Hebrónu.