< 2 Samweli 4 >

1 Ikawa Ishboshethi, mwana wa Sauli, aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, mikono yake ikadhoofika, na Israeli yote ikataabika.
و چون پسر شاول شنید که ابنیر در حبرون مرده است دستهایش ضعیف شد، وتمامی اسرائیل پریشان گردیدند.۱
2 Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa wakuu wa vikosi vya askari. Mmoja wao alikuwa Baana na mwingine alikuwa Rekabu, wana wa Rimoni Mbeerothi wa wana wa Benjamini(kwa maana Berothi ilihesabiwa kuwa sehemu ya Benjamini,
و پسر شاول دو مرد داشت که سردار فوج بودند؛ اسم یکی بعنه و اسم دیگری ریکاب بود، پسران رمون بئیروتی از بنی بنیامین، زیرا که بئیروت با بنیامین محسوب بود.۲
3 na Waberothi walikimbilia Gitaimu na wamekuwa wakiishi pale hadi sasa).
و بئیروتیان به جتایم فرار کرده، در آنجا تا امروز غربت پذیرفتند.۳
4 Basi Yonathani, mwana wa Sauli, alikuwa na mwana mlemavu wa miguu. Alikuwa na umri wa miaka mitano habari kuhusu Sauli na Yonathani ilipofika Yezreeli. Yaya wake akamchukua ili akimbie. Lakini wakati anakimbia, mwana wa Yonathani alianguka na akawa kirema. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.
و یوناتان پسر شاول را پسری لنگ بود که هنگام رسیدن خبر شاول و یوناتان از یزرعیل، پنج ساله بود، و دایه‌اش او را برداشته، فرار کرد. وچون به فرار کردن تعجیل می‌نمود، او افتاد و لنگ شد و اسمش مفیبوشت بود.۴
5 Hivyo wana wa Rimoni mbeerothi, Rekabu na Baana, wakasafiri mchana wakati wa jua kali mpaka nyumbani mwa Ishbothethi, yeye alikuwa amepumzika mchana.
و ریکاب و بعنه، پسران رمون بئیروتی روانه شده، در وقت گرمای روز به خانه ایشبوشت داخل شدند و او به خواب ظهر بود.۵
6 Mwanamke aliyekuwa akililinda lango alisinzia wakati akipepeta ngano, Rekabu na Baana waliingia ndani polepole na wakampita.
پس به بهانه‌ای که گندم بگیرند در میان خانه داخل شده، به شکم او زدند و ریکاب و برادرش بعنه فرارکردند.۶
7 Hivyo walipoingia ndani ya nyumba, walimpiga na kumuua wakati amelala chumbani mwake. Kisha wakakata kichwa chake na wakaondoka nacho, wakasafiri njiani usiku kucha mpaka Araba.
و چون به خانه داخل شدند و او بربسترش در خوابگاه خود می‌خوابید، او را زدند وکشتند و سرش را از تن جدا کردند و سرش راگرفته، از راه عربه تمامی شب کوچ کردند.۷
8 Wakaleta kichwa cha Ishboshethi kwa Daudi huko Hebroni, nao wakamwambia mfalme, “Tazama, hiki ni kichwa cha Ishboshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyekuwa akiutafuta uhai wako. Leo Yahwe amemlipia kisasi bwana wetu mfalme dhidi ya Sauli na uzao wake.”
و سرایشبوشت را نزد داود به حبرون آورده، به پادشاه گفتند: «اینک سر دشمنت، ایشبوشت، پسرشاول، که قصد جان تو می‌داشت. و خداوندامروز انتقام آقای ما پادشاه را از شاول و ذریه‌اش کشیده است.»۸
9 Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni mbeerothi, akawambia, “Kama Yahwe aishivyo, aliyeuokoa uhai wangu na kila shida,
و داود ریکاب و برادرش بعنه، پسران رمون بئیروتی را جواب داده، به ایشان گفت: «قسم به حیات خداوند که جان مرا از هر تنگی فدیه داده است.۹
10 mtu mmoja aliponiambia, 'Tazama, Sauli amekufa,' akifikiri alileta habari njema, nilimkamata na kumwua huko Siklagi. Huo ndio ujira niliompa kwa habari yake.
وقتی که کسی مرا خبر داده، گفت که اینک شاول مرده است و گمان می‌برد که بشارت می‌آورد، او را گرفته، در صقلغ کشتم و این اجرت بشارت بود که به او دادم.۱۰
11 Namna gani, mtu mwovu anapomwua mwenye haki kitandi mwake ndani ya nyumba, Je nisiitake damu yake kutoka katika mikono yenu, na kuwaondoa duniani?”
پس چندمرتبه زیاده چون مردان شریر، شخص صالح رادر خانه‌اش بر بسترش بکشند، آیا خون او را ازدست شما مطالبه نکنم؟ و شما را از زمین هلاک نسازم؟»۱۱
12 Kisha Daudi akawaagiza vijana, nao wakawaua wakakata mikono na miguu yao na kuwatundika kando ya bwawa huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ishboshethi na kukizika katika kaburi la Abneri katika Hebroni.
پس داود خادمان خود را امر فرمودکه ایشان را کشتند و دست و پای ایشان را قطع نموده، بر برکه حبرون آویختند. اما سرایشبوشت را گرفته در قبر ابنیر در حبرون دفن کردند.۱۲

< 2 Samweli 4 >