< 2 Samweli 4 >

1 Ikawa Ishboshethi, mwana wa Sauli, aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, mikono yake ikadhoofika, na Israeli yote ikataabika.
When Ishbosheth, Saul's son, heard that Abner was dead in Hebron, his hands became weak, and all Israel was troubled.
2 Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa wakuu wa vikosi vya askari. Mmoja wao alikuwa Baana na mwingine alikuwa Rekabu, wana wa Rimoni Mbeerothi wa wana wa Benjamini(kwa maana Berothi ilihesabiwa kuwa sehemu ya Benjamini,
Now Saul's son had two men who were captains of groups of soldiers. The name of one was Baanah and the other Recab, sons of Rimmon the Beerothite of the people of Benjamin (for Beeroth is also considered part of Benjamin,
3 na Waberothi walikimbilia Gitaimu na wamekuwa wakiishi pale hadi sasa).
and the Beerothites fled to Gittaim and have been living there until this very time).
4 Basi Yonathani, mwana wa Sauli, alikuwa na mwana mlemavu wa miguu. Alikuwa na umri wa miaka mitano habari kuhusu Sauli na Yonathani ilipofika Yezreeli. Yaya wake akamchukua ili akimbie. Lakini wakati anakimbia, mwana wa Yonathani alianguka na akawa kirema. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.
Now Jonathan, Saul's son, had a son who was crippled in his feet. He was five years old when the news about Saul and Jonathan came from Jezreel. His nurse picked him up to flee. But as she was running, Jonathan's son fell and became lame. His name was Mephibosheth.
5 Hivyo wana wa Rimoni mbeerothi, Rekabu na Baana, wakasafiri mchana wakati wa jua kali mpaka nyumbani mwa Ishbothethi, yeye alikuwa amepumzika mchana.
So the sons of Rimmon the Beerothite, Recab and Baanah, traveled during the heat of the day to the house of Ishbosheth, as he was resting at noon.
6 Mwanamke aliyekuwa akililinda lango alisinzia wakati akipepeta ngano, Rekabu na Baana waliingia ndani polepole na wakampita.
The woman guarding the door had fallen asleep while sifting wheat, and Recab and Baanah walked in quietly and passed her.
7 Hivyo walipoingia ndani ya nyumba, walimpiga na kumuua wakati amelala chumbani mwake. Kisha wakakata kichwa chake na wakaondoka nacho, wakasafiri njiani usiku kucha mpaka Araba.
So after they entered the house, they attacked him and killed him as he was lying on his bed in his room. Then they cut off his head and carried it away, traveling on the road all night to the Arabah.
8 Wakaleta kichwa cha Ishboshethi kwa Daudi huko Hebroni, nao wakamwambia mfalme, “Tazama, hiki ni kichwa cha Ishboshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyekuwa akiutafuta uhai wako. Leo Yahwe amemlipia kisasi bwana wetu mfalme dhidi ya Sauli na uzao wake.”
They brought the head of Ishbosheth to David at Hebron, and they said to the king, “Look, this is the head of Ishbosheth son of Saul, your enemy, who sought your life. Today Yahweh has avenged our master the king against Saul and his descendants.”
9 Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni mbeerothi, akawambia, “Kama Yahwe aishivyo, aliyeuokoa uhai wangu na kila shida,
David answered Recab and Baanah his brother, the sons of Rimmon the Beerothite; he said to them, “As Yahweh lives, who delivered my life from every trouble,
10 mtu mmoja aliponiambia, 'Tazama, Sauli amekufa,' akifikiri alileta habari njema, nilimkamata na kumwua huko Siklagi. Huo ndio ujira niliompa kwa habari yake.
when someone told me, 'Look, Saul is dead,' thinking he was bringing good news, I seized him and killed him at Ziklag. That was the reward I gave him for his news.
11 Namna gani, mtu mwovu anapomwua mwenye haki kitandi mwake ndani ya nyumba, Je nisiitake damu yake kutoka katika mikono yenu, na kuwaondoa duniani?”
How much more, when wicked men have killed an innocent person in his own house on his bed, should I not now require his blood from your hand, and remove you from the earth?”
12 Kisha Daudi akawaagiza vijana, nao wakawaua wakakata mikono na miguu yao na kuwatundika kando ya bwawa huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ishboshethi na kukizika katika kaburi la Abneri katika Hebroni.
Then David gave orders to the young men, and they killed them and cut off their hands and feet and hung them up beside the pool at Hebron. But they took the head of Ishbosheth and buried it in the grave of Abner in Hebron.

< 2 Samweli 4 >