< 2 Samweli 4 >

1 Ikawa Ishboshethi, mwana wa Sauli, aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, mikono yake ikadhoofika, na Israeli yote ikataabika.
And when Saul's son heard that Abner was dead in Hebron, his hands were enfeebled, and all Israel was troubled.
2 Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa wakuu wa vikosi vya askari. Mmoja wao alikuwa Baana na mwingine alikuwa Rekabu, wana wa Rimoni Mbeerothi wa wana wa Benjamini(kwa maana Berothi ilihesabiwa kuwa sehemu ya Benjamini,
And Saul's son had two men, captains of bands: the name of the one was Baanah, and the name of the other Rechab, the sons of Rimmon the Beerothite, of the children of Benjamin; for Beeroth also was reckoned to Benjamin.
3 na Waberothi walikimbilia Gitaimu na wamekuwa wakiishi pale hadi sasa).
And the Beerothites had fled to Gittaim, and were sojourners there until this day.
4 Basi Yonathani, mwana wa Sauli, alikuwa na mwana mlemavu wa miguu. Alikuwa na umri wa miaka mitano habari kuhusu Sauli na Yonathani ilipofika Yezreeli. Yaya wake akamchukua ili akimbie. Lakini wakati anakimbia, mwana wa Yonathani alianguka na akawa kirema. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.
And Jonathan Saul's son had a son that was lame of [his] feet. He was five years old when the news came of Saul and Jonathan out of Jizreel; and his nurse took him up and fled. And it came to pass, as she made haste to flee, that he fell, and became lame. And his name was Mephibosheth.
5 Hivyo wana wa Rimoni mbeerothi, Rekabu na Baana, wakasafiri mchana wakati wa jua kali mpaka nyumbani mwa Ishbothethi, yeye alikuwa amepumzika mchana.
And the sons of Rimmon the Beerothite, Rechab and Baanah, went and came in about the heat of the day into the house of Ishbosheth, who was taking his noonday rest.
6 Mwanamke aliyekuwa akililinda lango alisinzia wakati akipepeta ngano, Rekabu na Baana waliingia ndani polepole na wakampita.
And they came thither into the midst of the house, [as though] they would fetch wheat; and they smote him in the belly; and Rechab and Baanah his brother escaped.
7 Hivyo walipoingia ndani ya nyumba, walimpiga na kumuua wakati amelala chumbani mwake. Kisha wakakata kichwa chake na wakaondoka nacho, wakasafiri njiani usiku kucha mpaka Araba.
They came into the house, as he lay on his bed in his bedchamber, and they smote him, and slew him, and beheaded him; and they took his head, and went by the way of the plain all night.
8 Wakaleta kichwa cha Ishboshethi kwa Daudi huko Hebroni, nao wakamwambia mfalme, “Tazama, hiki ni kichwa cha Ishboshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyekuwa akiutafuta uhai wako. Leo Yahwe amemlipia kisasi bwana wetu mfalme dhidi ya Sauli na uzao wake.”
And they brought the head of Ishbosheth to David in Hebron, and said to the king, Behold the head of Ishbosheth the son of Saul, thine enemy who sought thy life; and Jehovah has given to my lord the king to be avenged this day of Saul and of his seed.
9 Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni mbeerothi, akawambia, “Kama Yahwe aishivyo, aliyeuokoa uhai wangu na kila shida,
Then David answered Rechab and Baanah his brother, the sons of Rimmon the Beerothite, and said to them, [As] Jehovah liveth, who has redeemed my soul out of all distress,
10 mtu mmoja aliponiambia, 'Tazama, Sauli amekufa,' akifikiri alileta habari njema, nilimkamata na kumwua huko Siklagi. Huo ndio ujira niliompa kwa habari yake.
when one told me, saying, Behold, Saul is dead! and he was in his own sight a messenger of good, I took hold of him, and slew him in Ziklag — to whom forsooth I should give a reward for his good tidings:
11 Namna gani, mtu mwovu anapomwua mwenye haki kitandi mwake ndani ya nyumba, Je nisiitake damu yake kutoka katika mikono yenu, na kuwaondoa duniani?”
how much more, when wicked men have slain a righteous person in his own house upon his bed? and should I not now demand his blood of your hand, and take you away from the earth?
12 Kisha Daudi akawaagiza vijana, nao wakawaua wakakata mikono na miguu yao na kuwatundika kando ya bwawa huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ishboshethi na kukizika katika kaburi la Abneri katika Hebroni.
And David commanded his young men, and they slew them, and cut off their hands and their feet, and hanged [them] up over the pool in Hebron. But they took the head of Ishbosheth, and buried it in the sepulchre of Abner in Hebron.

< 2 Samweli 4 >