< 2 Samweli 24 >
1 Kisha hasira ya Yahwe ikawaka dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi kinyume chao kusema, “Nenda, ukawahesabu Israeli na Yuda.”
Et la fureur du Seigneur recommença à s’irriter contre Israël, et il excita parmi eux, David, disant: Va, dénombre Israël et Juda.
2 Mfalme akamwambia Yoabu, jemedari wa jeshi, aliyekuwa pamoja naye, “Nenda upite katika kabila zote za Israeli, toka Dani mpaka Beersheba, uwahesabu watu wote, ili niweze kujua idadi kamili ya watu wanaofaa kwa vita.”
Le roi dit donc à Joab, prince de son armée: Parcours toutes les tribus d’Israël, depuis Dan jusqu’à Bersabée, et dénombrez tout le peuple, afin que j’en sache le nombre.
3 Yoabu akamwambia mfalme, “Yahwe Mungu wako na aizidishe hesabu ya watu mara mia, na macho ya bwana wangu mfalme yaone ikifanyika. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme analitaka jambo hili?
Et Joab répondit au roi: Que le Seigneur votre Dieu multiplie votre peuple encore autant qu’il est maintenant, et que de nouveau, il le centuple en la présence de mon seigneur le roi: mais que veut faire mon seigneur le roi par une chose de cette nature?
4 Walakini neno la mfalme lilikuwa la mwisho dhidi ya Yoabu na dhidhi ya majemedari wa jeshi. Hivyo Yoabu na majemedari wakatoka mbele ya mfalme kuwahesabu watu wa Israeli.
Mais la parole du roi l’emporta sur les paroles de Joab et des princes de l’armée; et Joab sortit, et les princes des soldats, de la présence du roi, pour dénombrer le peuple d’Israël.
5 Wakavuka Yordani na kupiga kambi karibu na Aroeri, kusini mwa mji bondeni. Kisha wakasafiri kupitia Gadi mpaka Yazeri.
Et lorsqu’ils eurent passé le Jourdain, ils vinrent à Aroër, à la droite de la ville qui est dans la vallée de Gad,
6 Wakaja Gileadi na nchi ya Tahtimu Hodshi, kisha Dani, Jaani na karibu kuelekea Sidoni.
Puis, par Jazer ils passèrent en Galaad, et dans la terre inférieure d’Hodsi; et ils vinrent dans les forêts de Dan. Tournant ensuite près de Sidon,
7 Wakafika ngome ya Tiro na miji yote ya Wahivi na Wakanaani. Kisha wakaenda Negebu katika Yuda huko Beersheba.
Ils passèrent près des murailles de Tyr, et de toute la terre de l’Hévéen et du Chananéen, et ils vinrent au midi de Juda, à Bersabée.
8 Walipokuwa wamepita katika nchi yote, wakarejea Yerusalemu mwishoni mwa miezi tisa na siku ishirini.
Et, toute la terre examinée, ils se trouvèrent, après neuf mois et vingt jours, à Jérusalem.
9 Ndipo Yoabu alipotoa taarifa ya hesabu kamili kwa mfalme kuhusu watu wawezao kupigana vita. Katika Israeli kulikuwa na watu 800, 000 jasiri wawezao kutoa upanga, na wale wa Yuda walikuwa watu 500, 000.
Joab donc donna le dénombrement du peuple au roi, et il se trouva d’Israël huit cent mille hommes forts, qui pouvaient tirer l’épée; et de Juda, cinq cent mille combattants.
10 Ndipo moyo wa Daudi ukamchoma alipokuwa amewahesabu watu. Hivyo akamwambia Yahwe, “Kwa kufanya hivi nimetenda dhambi sana. Sasa, Yahwe, uiondoe hatia ya mtumishi wako, kwani nimetenda kwa upumbavu.”
Mais le cœur de David fut pris de remords, après que le peuple eut été dénombré, et David dit au Seigneur: J’ai beaucoup péché en cette action; mais je vous prie. Seigneur, écartez l’iniquité de votre serviteur, parce que j’ai agi tout à fait en insensé.
11 Daudi alipoinuka asubuhi, neno la Yahwe likamjia nabii Gadi, mwonaji wa Daudi, kusema,
C’est pourquoi David se leva le matin, et la parole du Seigneur fut adressée à Gad, le prophète et le voyant de David, disant:
12 Nenda umwambie Daudi; 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: “Ninakupa mambo matatu. Uchague mojawapo.”
Va, et parle à David: Voici ce que dit le Seigneur: L’option de trois choses t’est donnée; choisis celle que tu voudras, afin que je te la fasse.
13 Hivyo Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je miaka mitatu ya njaa ije katika nchi yako? au miezi mitatu ukimbie kutoka kwa adui zako huku wakikufuatia? au kuwe na tauni ya siku tatu katika nchi yako? Amua sasa jibu gani nimrudishie aliyenituma.”
Lors donc que Gad fut venu vers David, il lui annonça, disant: Ou une famine vous viendra sur la terre durant sept ans; ou vous fuirez vos ennemis durant trois mois, et eux vous poursuivront; ou bien une peste sera pendant trois jours dans votre terre. Maintenant donc délibérez, et voyez quelle parole je dois porter en réponse à celui qui m’a envoyé.
14 Ndipo Daudi alipomwambia Gadi, “Nipo katika shida kubwa. Haya na tuanguke katika mikono ya Yahwe kuliko kuanguka katika mikono ya mwanadamu, kwani matendo yake ya rehema ni makuu sana.”
Et David répondit à Gad: Je suis dans une très grande angoisse, mais il vaut mieux que je tombe dans les mains du Seigneur (car ses miséricordes sont sans nombre), que dans les mains des hommes.
15 Hivyo akatuma tauni juu ya Israeli kuanzia asubuhi kwa muda ulioamriwa, na watu sabini na tano elfu kutoka Dani mpaka Beersheba wakafa.
Et le Seigneur envoya une peste en Israël, depuis le matin jusqu’au temps marqué; et il mourut d’entre le peuple, depuis Dan jusqu’à Bersabée, soixante dix mille hommes.
16 Malaika aliponyosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili kuuharibu, Yahwe akabadili nia yake kuhusu madhara, na akamwambia malaika aliyekuwa tiyari kuwaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako sasa.” Wakati huo malaika wa Yahwe alikuwa amesimama katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.
Et, lorsque l’ange du Seigneur eut étendu sa main sur Jérusalem pour la détruire, le Seigneur eut pitié de son affliction, et dit à l’ange qui frappait le peuple: Il suffit, maintenant retiens ta main. Or, l’ange du Seigneur était alors près de l’aire d’Aréuna, le Jébuséen.
17 Daudi alipomwona malaika aliyekuwa amewapiga watu, akamwambia Yahwe kusema, “Nimetenda dhambi, na nimetenda kwa upumbavu. Lakini kondoo hawa, wamefanya nini? Tafadhari, mkono wako na uniadhibu mimi na familia ya baba yangu!”
Et David dit au Seigneur, quand il vit l’ange tuant le peuple: C’est moi qui ai péché et qui ai agi iniquement: ceux-ci, qui sont les brebis, qu’ont-ils fait? Que votre main, je vous conjure, se tourne contre moi et contre la maison de mon père.
18 Kisha Gadi akaja siku hiyo kwa Daudi na kumwambia, “Kwea na ujenge madhabahu kwa ajili ya Yahwe katika kiwanja cha kupuria cha Arauna Myebusi.”
Or, Gad vint vers David en ce jour-là, et lui dit: Montez, et élevez au Seigneur un autel dans l’aire d’Aréuna, le Jébuséen.
19 Hivyo Daudi akakwea kama Gadi alivyomwelekeza kufanya, kama Yahwe alivyokuwa ameagiza.
Et David monta selon la parole de Gad, que lui avait ordonnée le Seigneur.
20 Arauna akatazama na kumwona mfalme na watumishi wake wakikaribia. Ndipo Arauna akaondoka na kumsujudia mfalme uso wake mpaka juu ya ardhi.
Et regardant, Aréuna aperçut le roi et ses serviteurs venir vers lui;
21 Kisha Arauna akasema, “Kwa nini bwana wangu mfalme amekuja kwangu, mtumishi wake? Daudi akajibu, “Kununua uwanja wako wa kupuria, ili nimjengee Yahwe madhabahu, ili kwamba tauni iondolewe kwa watu.”
Et il sortit et se prosterna devant le roi, le visage incliné vers la terre, et il dit: Quelle raison y a-t-il pour que mon seigneur le roi vienne vers son serviteur? David lui répondit: C’est pour acheter de toi l’aire et bâtir un autel au Seigneur, afin que cesse la tuerie qui ravage le peuple.
22 Arauna akamwambia Daudi, “Chukua liwe lako, bwana wangu mfalme. Ulifanyie lolote lolote lililojema machoni pako. Tazama, ng'ombe kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na miganda ya kupuria na nira kwa kuni.
Et Aréuna dit à David: Que mon seigneur le roi prenne, et qu’il offre comme il lui plaît: vous avez les bœufs pour l’holocauste, le char, et les jougs de bœufs, pour servir de bois.
23 Haya yote bwana wangu mfalme, mimi Arauna nakupa.” Kisha akamwambia mfalme, “Yahwe Mungu wako na awe nawe.”
Le roi Aréuna donna toutes ces choses au roi; et Aréuna dit au roi: Que le Seigneur votre Dieu reçoive votre vœu.
24 Mfalme akamwambia Arauna, “Hapana, nahimiza kukinunua kwa thamani yake. Sitatoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Yahwe chochote nisichokigharimia.” Hivyo Daudi akakinunua kiwanja cha kupuria na ng'ombe kwa shekeli hamsini za fedha.
Le roi, lui répondant, dit: Pas du tout comme vous voulez; mais j’achèterai de vous, selon le prix, et je n’offrirai point au Seigneur mon Dieu des holocaustes qui ne me coûtent rien. David donc acheta l’aire et les bœufs cinquante sicles d’argent.
25 Daudi akajenga madhabahu kwa Yahwe pale na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Hivyo wakamsihi Yahwe kwa niaba ya nchi, hivyo akaizuia tauni katika katika Israeli yote.
Et David bâtit là un autel au Seigneur, et il offrit des holocaustes et des sacrifices pacifiques. Et le Seigneur devint propice à la terre, et la plaie fut écartée d’Israël.